Mikutano Ya Utumishi Ya Mei
Juma Toka Mei 5
Wimbo 100
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo ya Huduma Yetu ya Ufalme. Taja mawazo kutokana na magazeti ya mwisho mwisho juu yayo inaomba kuzungumzia.
Dak. 15: “Umati Mkubwa Unaongezwa.” Kwa maulizo na majibu. Chunguzeni upya madokezo makuu ambayo yanapatikana katika Mnara wa Mlinzi wa Agosti 15, 1993, kur. 12-17.
Dak. 18: “Tusaidie Watu Wasio na Ujuzi Kuelewa.” Kwa maulizo na majibu. Chunguzeni sehemu fulani za pekee za broshua Anataka: ufundi wa kujifunza uliorahisishwa, maulizo ya akili, picha zinazovutia, mitajo mingi ya Biblia. Kazieni kwamba mradi ni kuanzisha mafunzo ya Biblia yatakayoongoza baadaye kwenye kitabu Ujuzi. Onyesho linalofanywa na mhubiri mwenye uwezo wa kuanzisha funzo kwa kutumia ufundi unaopendekezwa katika fungu 4. Watie moyo wazazi wote wa kusanyiko kujifunza broshua pamoja na watoto wao.
Wimbo 130 na sala ya mwisho.
Juma Toka Mei 12
Wimbo 107
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Hali ya akaunti. Kulingana na wakati uliyopo, eleza kwa kifupi mambo fulani yaliyoonwa ya mahali kuhusiana na uangushaji wa broshua Anataka na matumizi yake ili kuanzisha mafunzo ya Biblia.
Dak. 15: “Tuwaongoze Wanafunzi Kwenye Tengenezo la Yehova.” (Maf.1-6) Kwa maulizo na majibu. Someni mafungu 5-6 na maandiko yanayotolewa kwa mitajo. Elezeni mambo yaliyoonwa yaliyotokea mahali penu yanayoonyesha jinsi wanafunzi wa Biblia walivyoitikia walipoona kaseti vidio Les Témoins de Jéhovah — Un nom, une organisation.
Dak. 20: “Tufundishe Wengine Yale Mungu Anataka Kwetu.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji ya mafungu 1-4. Onyesho la kielelezo la fungu 5 katika vikao vinne tofauti: barabarani, mlangoni, katika mtaa wa kibiashara na katika shamba la wanyama. Sema kwa kila mmoja kufikiri kujipatia jioni hii kabla ya kuondoka Jumba la Ufalme broshua na magazeti kwa ajili ya mahubiri.
Wimbo 126 na sala ya mwisho.
Juma Toka Mei 19
Wimbo 113
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Sema kwamba bado kungali wakati wa kujaza ombi kwa ajili ya kuwa painia msaidizi mnamo Mei. Chunguza Majibu kwa maulizo yenu na julisha kutaniko kwamba mnahitaji vitabu fulani ili kujazia maktaba ya Jumba la Ufalme.
Dak. 15: “Tuwaongoze Wanafunzi Kwenye Tengenezo la Yehova.” (Maf. 7-14) Kwa maulizo na majibu. Omba kwa mwalimu mwenye uwezo kuonyesha jinsi ya kuwa na mazungumzo ya kirafiki na ya wazi pamoja na mwanafunzi juu ya umuhimu wa kuhudhuria kwenye mikutano.
Dak. 15: Tutumie Kikamilifu Vitabu Vyetu. Hotuba inayotolewa na mzee. Kulingana na ripoti, makutaniko yanaomba mara nyingi magazeti mengi zaidi kuliko yale ambayo yanaangusha kila mwezi. Karibu nusu hayahesabiwi kwenye ripoti za utumishi. (Toa hesabu zilizorekodiwa katika kutaniko.) Magazeti hayo yanakuwaje? Mengi yanaishia kwenye ubao wa maktaba au yanatupwa. Jinsi gani kuepuka hilo? Kila mhubiri angepaswa kukadiria kwa makini yale anayohitaji na kuomba tu yale ataweza kuangusha. Tujizoeze kutolea magazeti kwa wale wote tunaokutana nao. Tusitupetupe namba za zamani. Tushiriki kwa ukawaida katika siku ya magazeti.
Wimbo 128 na sala ya mwisho.
Juma Toka Mei 26
Wimbo 121
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kumbusha kila mmoja kwamba inafaa kutoa ripoti ya Mei. Toa majina ya mapainia wasaidizi mnamo Juni. Kazia mipango ya ziada iliyochukuliwa mahali penu kwa ajili ya mikutano ya mahubiri. Katika Juni, tutafanya bidii ya pekee ili kurudi kuwaona wale ambao tuliachia broshua. Mradi ni kuanzisha mafunzo. Fanya kwa kifupi madokezo fulani juu ya namna ya kuuliza kwa busara jina na anwani ya watu ambao tunatolea ushuhuda wa vivi hivi. Ungeweza kwanza kutoa majina yako na anwani na kuuliza ni kwenye namba gani ya simu unaweza kumwita. Alika wasikilizaji kutoa madokezo mengine yaliyoonekana kuwa yenye matokeo.
Dak. 15: “Kwa Nini Wanafanya Hivyo?” Mzee anazungumza makala pamoja na mapainia wa kawaida wawili au watatu. (Ikiwa haiwezekani, omba kwa wahubiri ambao mara kwa mara ni mapainia wasaidizi.) Toa mawazo ya lazima ya makala “Mapainia Hutoa na Kupokea Baraka,” iliyotolewa katika Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1994. Uliza kwa kila mmoja kusema kwa nini amekuwa painia. Sema kwa mapainia kueleza mambo yaliyoonwa yanayoonyesha namna ambayo walibarikiwa hatimaye.
Dak. 20: “Je! Wewe Sikuzote ni Mtumwa wa Mojawapo ya Desturi za Mababu?” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji na kuambatanisha mambo kulingana na mahitaji ya pekee ya kutaniko.
Wimbo 129 na sala ya mwisho.