Kwa Nini Wanafanya Hivyo?
1 Kuhusu Kristo, ilitabiriwa kwamba ‘juhudi kwa ajili ya nyumba ya Mungu ingemla.’ (Zab. 69:9) Juhudi ya Yesu kwa ajili ya ibada ya kweli inayotolewa kwa Yehova ilimsukuma kuweka huduma yake pa nafasi ya kwanza. (Lk. 4:43; Yn. 18:37) Katika siku zetu, Mashahidi wa Yehova wanaonyesha katika huduma yao uharaka uleule wa kutoa ushuhuda juu ya ukweli. Mwaka wa nyuma, wahubiri 645,509 kwa wastani walijitoa kila mwezi katika aina moja au nyingine ya utumishi wa painia. Tukiwa waliojiweka wakfu kwa Mungu, tungepaswa sote kuchunguza katika sala ikiwa tunaweza kupanga programu yetu ili kuwa mapainia wasaidizi au wa kawaida.—Zab. 110:3; Muh. 12:1; Rom. 12:1.
2 Tunaishi katika mfumo wa mambo wenye uchoyo na wenye kupenda vitu vya kimwili; watu wengi wana magumu ya kuelewa kwamba wengine wanajitoa sana katika huduma ijapokuwa hilo haliwatolei faida yoyote ya kifedha wala utukufu wowote. Kwa nini mapainia wanafanya hivyo? Wanajua kwamba wanajitoa kabisa katika kazi ya kuokoa uhai. Wakiwa wenye kuchochewa na upendo wa kina kirefu kwa Yehova na kwa majirani wao, wanajisikia katika wajibu wa kutoa msaada wao ili kuokoa uhai wa watu. (Rom. 1:14-16; 1 Tim. 2:4; 4:16) Wenzi wa ndoa wawili mapainia walieleza hali hivi kwa kifupi: “Kwa nini sisi ni mapainia? Je! tungekuwa na sababu ya kweli ya kutoa kwa Mungu ikiwa sisi hatungekuwa mapainia?” La Tour de Garde, 15/02/83, p. 23, § 7.
3 Dada mwingine alizungumzia uamuzi wake wa kuanzisha utumishi wa painia: “Mume wangu na mimi tulifanya mipango ya kuishi kwa kutumia mshahara mmoja, lililomaanisha kuacha mambo yote yasiyohitajiwa. Hata hivyo, Yehova alitubariki sana, asituache kamwe tuwe masikini au wenye uhitaji. . . . Nimepata sababu ya kweli ya kuishi—ile ya kuwasaidia wale wenye uhitaji wapate kujua kwamba Yehova, Mungu wa kweli, hayuko mbali na wale wamtafutao.” La Tour de Garde, 1/08/92 p. 27. Wakiwa wenye kutambua kwamba wakati unasonga mbele, mapainia wanaridhika na mambo ya lazima ili kuishi huku wakikusanya hazina za kweli za kiroho zitakazodumu milele.—1 Tim. 6:8, 18, 19.
4 Ikiwa hali yako inakuruhusu, kwa nini usijiunge na mamia ya maelfu ya akina ndugu na dada ulimwenguni ambao ni mapainia? Hilo litakuwezesha kushiriki shangwe yao.