Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 5/10 uku. 3-5
  • “Unaweza Kuwa Painia Kabisa!”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Unaweza Kuwa Painia Kabisa!”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Utumishi Wa Painia: Je! Ni Wako?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Sasa Ndio Wakati wa Kuhubiri!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Kazi ya Upainia Inatia Nguvu Uhusiano Wetu Pamoja na Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Je, Ulikuwa Painia wa Kawaida Hapo Mbele?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 5/10 uku. 3-5

“Unaweza Kuwa Painia Kabisa!”

1. Dada mmoja alisema nini kuhusu utumishi wake wa upainia?

1 “Singeweza kupata kazi nyingine yoyote ambayo ingeniletea furaha nyingi ao baraka nyingi za kiroho.” Hivyo ndivyo alivyosema Kathe B. Palm. Kwa muda wa miaka mingi, alihubiri akiwa painia aliyejitoa kwa ajili ya wengine kuanzia upande mmoja mpaka upande mwingine wa Chili, Amerika Kusini. Kwa kufikiria maisha yenye baraka nyingi ya wale wanaofanya utumishi wa wakati wote, labda mutu fulani amekwisha kukuambia hivi: “Unaweza kuwa painia kabisa!”

2. Eleza kwa nini tunapata furaha nyingi tunapojitoa katika kazi za kiroho.

2 Njia ya Maisha Yenye Kufurahisha: Yesu, aliye Mfano wetu alipata furaha ya kweli katika kufanya mapenzi ya Baba yake. (Yoh. 4:34) Kwa hiyo, kwa moyo wote Yesu aliwafundisha wafuasi wake kwamba furaha ya kweli inatokana na kufanya kazi zinazohusiana na ibada ya Yehova. Tunatosheka katika maisha yetu ikiwa tunashugulikia sana kazi zinazotufanya tukubaliwe na Yehova. Pia, furaha yetu inaongezeka tunapotumia wakati mwingi, nguvu nyingi, na mali yetu ili kusaidia wengine.—Mdo. 20:31, 35.

3. Tunaweza kupata furaha gani tunapotumia wakati mwingi katika kazi ya kuhubiri?

3 Kadiri tunavyotumia wakati mwingi katika mahubiri, ndivyo tunavyopata nafasi nyingi zaidi za kupata furaha ya kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia. Hata mahali ambapo wasikilizaji wanaonekana kwamba hawapendezwi na ujumbe wetu, tunapopata uzoefu na ufundi katika mahubiri, tunaweza kuona kwamba eneo letu ni lenye matokeo mazuri zaidi kuliko tulivyowazia hapo mbele. Mapainia wanaweza kutumia mambo wanayojifunza kwenye Shule ya Utumishi wa Painia, shule wanayohuzuria wakiisha kufanya kazi ya upainia kwa karibu mwaka mmoja. (2 Tim. 2:15) Tunapoendelea katika kazi ya upainia, tunaweza kuwa wenye kupanda vizuri mbegu za kweli ambazo zitazaa matunda wakati ujao.—Mhu. 11:6.

4. Vijana wanaokaribia kumaliza masomo wanapaswa kufikiria nini?

4 Vijana: Ikiwa munakaribia kumaliza masomo ya sekondari, je, mumekwisha kufikiria kwa uangalifu wakati wenu ujao? Kwa sasa, kazi za masomo zinawachukua wakati mwingi. Namna gani mutatumia wakati wenu kisha kumaliza masomo? Kuliko kufuatia kazi ya kimwili, kwa nini musifikirie katika sala mradi wa kuwa painia wa kawaida? Ufundi mutakaopata—kwa kuhubiria watu wa malezi tofauti-tofauti, kwa kushinda mambo muliyoona kuwa magumu, kwa kupanga programu yenu vizuri na kuiheshimu, na munapojua kufundisha—utawaletea faida muda wote wa maisha.

5. Namna gani wazazi na ndugu na dada katika kutaniko wanaweza kuchochea wengine wafanye kazi ya upainia?

5 Wazazi, je, munatimiza daraka lenu kwa kuwasaidia watoto wenu wajiwekee mradi wa kufanya utumishi wa wakati wote? Kupitia maneno yenu na mfano wenu mzuri, munaweza kuwasaidia sana watie mambo ya Ufalme pa nafasi ya kwanza. (Mt. 6:33) Ray, aliyeanza kazi ya upainia alipomaliza masomo ya sekondari, anakumbuka: “Sikuzote, mama yangu aliona kwamba kazi ya upainia inaleta furaha nyingi katika maisha.” Wote katika kutaniko wanaweza kuchochea wengine wafanye kazi ya upainia kwa kuwatia moyo na kuwategemeza. Jose, anayekaa Hispania, anasema hivi: “Ndugu na dada wa kutaniko langu waliona upainia kuwa kazi nzuri zaidi kwa vijana. Maelezo yao, kupendezwa kwao na kazi ya upainia, na msaada walionitolea, vilifanya iwe rahisi kwangu kuanza kazi ya upainia.”

6. Tunaweza kufanya nini ikiwa kwa sasa hatuna nia ya kufanya kazi ya upainia?

6 Kushinda Vizuizi: Lakini, namna gani ukisema, ‘Sina nia ya kufanya kazi ya upainia.’ Ikiwa hivyo ndivyo unavyofikiri, sali kwa Yehova kuhusu jinsi unavyojisikia na kumwambia, ‘Sijui ikiwa ninaweza kuweza kazi ya upainia, lakini ninataka kufanya mambo yanayokupendeza.’ (Zab. 62:8; Met. 23:26) Kisha, tafuta mwongozo wake kupitia Neno na tengenezo lake. Mapainia wa kawaida wengi ‘walionja’ upainia kwa kufanya kazi ya upainia msaidizi na furaha waliyopata iliwachochea waanze utumishi wa wakati wote.—Zab. 34:8.

7. Namna gani tunaweza kushinda mashaka ya kwamba hatuwezi kueneza saa 70 zinazoombwa kila mwezi?

7 Namna gani ikiwa una mashaka kwamba hauwezi kueneza saa 70 zinazoombwa kwa painia kila mwezi? Unaweza kuzungumza na mapainia walio katika hali zilizo sawa na zako. (Met. 15:22) Kisha andika programu mbalimbali zinazowezekana. Unaweza kuona kwamba kujinunulia wakati wa kuhubiri kwa kuacha kazi zisizo za lazima ni rahisi zaidi kuliko jinsi ulivyowazia kwanza.—Efe. 5:15, 16.

8. Kwa nini tuchunguze hali zetu mara kwa mara?

8 Chunguza Tena Hali Zako: Hali za kila mmoja wetu zinabadilika mara nyingi. Ni vizuri uchunguze hali zako mara kwa mara. Kwa mfano, je, unakaribia kuacha kazi kwa sababu ya uzee? Randy, aliyeacha kazi mbele ya kuzeeka sana anasema hivi: “Uamuzi huo uliniwezesha kuanza upainia wa kawaida pamoja na muke wangu, na ulitusaidia kupata nafasi ya kuhama na kutumikia mahali ambapo uhitaji ulikuwa mkubwa zaidi. Nimepata baraka nyingi sana kutokana na uamuzi huo, lakini baraka kubwa zaidi kupita zote ni kuwa na zamiri safi.”

9. Waume na wake zao wanapaswa kufikiria nini?

9 Kisha kuchunguza hali zao kwa uangalifu, waume fulani na wake zao wameona kwamba si vizuri wote wawili wafanye kazi inayowachukua wakati wote. Kwa kweli, hilo linaomba kufanya maisha ya familia yawe rahisi, lakini kufanya hivyo kunaleta baraka nyingi. John, ambaye muke wake aliacha hivi karibuni kazi inayomchukua wakati wote ili kupanua utumishi wake anasema hivi: “Jambo linaloniletea furaha zaidi ni kujua kwamba muke wangu yuko katika utumishi wa Yehova wakati wa mchana.”

10. Ni nini kinachochochea Wakristo wafikirie kufanya kazi ya upainia?

10 Njia ya Kuonyesha Upendo na Imani: Yehova amefanya kazi ya kuhubiri iwe kazi ya maana sana ambayo kila mmoja wetu anaweza kufanya. Karibuni ulimwengu huu utaharibiwa, na wale tu wanaoliitia jina la Yehova ndio wataokolewa. (Rom. 10:13) Kumpenda Yehova kwa moyo wote na kuonyesha shukrani kwa ajili ya yale ambayo ametufanyia kutatuchochea tutii amri ya kuhubiri kwa bidii ambayo Mwana wake ametoa. (Mt. 28:19, 20; 1 Yoh. 5:3) Pia, kuamini kwamba tunaishi katika siku za mwisho kutatuchochea kufanya yote tuwezayo katika kazi ya kuhubiri kunapokuwa kungali wakati, kuliko kutumia ulimwengu kwa ukamili.—1 Kor. 7:29-31.

11. Uone namna gani ikiwa mutu fulani anakuambia kwamba unaweza kuwa painia kabisa?

11 Kazi ya upainia wa kawaida haimaanishi tu kupitisha saa nyingi katika mahubiri; ni njia ya kuonyesha kwamba tumejitoa kwa Mungu. Kwa hiyo ikiwa mutu fulani anakuambia kwamba unaweza kuwa painia kabisa, uone kwamba anakusifu. Na ufikirie katika sala jinsi unavyoweza kufanya ili kujiunga na wale wanaofanya sehemu hii ya utumishi yenye kuleta furaha.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 4]

Wazazi, je, munatimiza daraka lenu kwa kuwasaidia watoto wenu wajiwekee mradi wa kufanya utumishi wa wakati wote?

[Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 5]

Yehova amefanya kazi ya kuhubiri iwe kazi ya maana sana ambayo kila mmoja wetu anaweza kufanya.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine