Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/05 uku. 3
  • Sasa Ndio Wakati wa Kuhubiri!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sasa Ndio Wakati wa Kuhubiri!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Unaweza Kuwa Painia Kabisa!”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Je, Unaweza Kuingia Katika “Mlango Mkubwa Unaoongoza Kwenye Utendaji”?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Je, mlango uongozao kwenye upainia umefunguka sasa kwa ajili yako?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Je, Ulikuwa Painia wa Kawaida Hapo Mbele?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 8/05 uku. 3

Sasa Ndio Wakati wa Kuhubiri!

1 “Mwogopeni Mungu na kumpa utukufu.” Chini ya uongozi wa kimalaika, ujumbe huu ni wenye kutangazwa “kwa kila taifa na kabila na lugha na watu.” Kwa nini? “Kwa kuwa saa ya hukumu yake [Mungu] imefika.” Leo, tunaishi katika ‘saa hiyo ya hukumu,’ ambayo itafikia upeo kwenye uharibifu wa mfumo huu wa mambo. Ni jambo la maana kwa watu ‘kumwabudu Yeye aliyefanya mbingu na dunia na bahari na chemchemi za maji.’ Hakuna kazi nyingine ya umaana au uharaka inayofanywa leo inayoweza kulinganishwa na kutangaza “habari njema ya milele.” Ndiyo, sasa ndio wakati wa kuhubiri!—Ufu. 14:6, 7.

2 Mnamo miaka kumi iliyopita, watumishi wa Yehova wametumia karibu saa bilioni 12 katika kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. Wengi wamefanya marekebisho katika maisha yao ili kushiriki kikamili zaidi katika kazi ya mavuno ya kiroho. (Mt. 9:37, 38) Kwa mfano mwaka uliopita, wastani wa wahubiri zaidi ya 850,000 kila mwezi walitumikia wakiwa mapainia. Mapainia wa kawaida wanaombwa kutumia wastani wa saa 70 kila mwezi katika kazi ya kuhubiri. Kuhusu mapainia wasaidizi, kiwango ni cha saa 50.

3 Jinsi ya Kupainia: Kwa kuwa wanajua kwamba “wakati uliobaki umepungua,” mapainia wanajitahidi kurahisisha maisha yao. (1 Kor. 7:29, 31) Wanatafuta njia za kupunguza gharama zao ili waweze kutumia wakati mchache katika kazi ya kimwili. Kwa mfano, mapainia fulani wamehamia katika makao madogo. Wengine wameondoa vitu vya kimwili visivyo vya lazima. (Mt. 6:19-21) Mara nyingi, wanapaswa pia kujitilia mipaka kuhusu ufuatiaji wa mambo ya kibinafsi. Wanafanya yote hayo wakiwa na mradi wa kutumia wakati zaidi na kutoa uangalifu mwingi kwenye huduma. (Efe. 5:15, 16) Wakiwa na subira, roho ya kujinyima, na wakimtegemea Yehova kupitia sala, wahubiri wengi wameweza kufanya mpango unaofaa unaowawezesha kupainia.

4 Je, unaweza kupainia? Kwa nini usiwaulize mapainia ambao wamefanikiwa wakuelezee siri ya kufanikiwa kwao? Tumika pamoja nao katika huduma ya shambani, na ushiriki furaha yao. Soma makala zinazohusu utumishi wa painia ambazo zimetokea katika vichapo vyetu. Jitilie miradi yenye kufaa kwa ajili yako; miradi inayoweza kuwa kama mawe ya kukanyagia ili ufikie kuwa painia. Ikiwa kuna vizuizi ambavyo kwa sasa vinakuzuia usiwe painia, zungumza na Yehova katika sala ukitaja vizuizi hivyo, na umwombe akusaidie upate suluhisho.—Met. 16:3.

5 Baraka na Furaha: Kuwa painia kunaboresha ufundi wetu mbalimbali wa kutumia Neno la Mungu, jambo ambalo linatuletea furaha nyingi. Dada mmoja kijana aliye painia alisema hivi: “Kuwa na uwezo wa kulitumia sawasawa Neno la Mungu la kweli ni baraka kweli. Unapofanya upainia, unatumia sana Biblia. Sasa ninapoenda nyumba kwa nyumba, ninaweza kufikiria maandiko yanayofaa kwa ajili ya kila mwenye nyumba”—2 Tim. 2:15.

6 Kuwa painia kunatutolea pia ufundi mwingi mbalimbali unaoweza kuboresha maisha yetu. Unaweza kusaidia vijana kujifunza jinsi ya kupangia wakati wao kwa hekima, jinsi ya kutumia fedha, na jinsi ya kupatana na watu. Wengi, kwa sababu ya kuwa mapainia, wanasitawisha mtazamo wa kiroho zaidi kuhusu maisha. (Efe. 4:13) Zaidi ya hiyo, mara nyingi mapainia wanakuwa na pendeleo la kuona mkono wa Yehova ukitenda kwa faida yao.—Mdo. 11:21; Flp. 4:11-13.

7 Labda moja ya baraka kubwa zaidi za kuwa painia ni kwamba kunatusaidia tumkaribie sana Yehova. Hilo linaweza kututegemeza wakati wa majaribu. Dada mmoja aliyevumilia kipindi cha magumu makali alisema: “Uhusiano wa karibu ambao nimesitawisha pamoja na Yehova kupitia upainia ulinisaidia kuvumilia magumu yote hayo.” Aliongeza: “Ninajisikia kuwa na furaha sana kwa kuwa nimetumia maisha yangu katika kumtumikia Yehova katika utumishi wa wakati wote. Hilo lilinisaidia kujitoa katika njia ambayo sikuwazia kuwa ningeweza.” (Mdo. 20:35) Nasi vilevile na tupate baraka nyingi kadiri tunavyofanya tuwezayo katika kazi ya maana sana ya kuhubiri.—Met. 10:22.

[Maulizo ya Funzo]

1. Kwa nini sasa ndio wakati wa kuhubiri?

2. Jinsi gani watumishi wa Yehova wanaonyesha kwamba wanatambua uharaka wa wakati tunamoishi?

3. Ni marekebisho gani ambayo mara nyingi wahubiri wanahitaji kufanya ili kupainia?

4. Ni hatua gani zenye kufaa zinazoweza kukusaidia kufikia mradi wa kupainia?

5. Namna gani kuwa painia kunatusaidia kuboresha ufundi wetu katika huduma?

6. Utumishi wa painia unamfanya mtu ajifunze mambo gani?

7. Jinsi gani kupainia kunatusaidia tumkaribie Yehova?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine