Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/98 uku. 3-6
  • Utumishi Wa Painia: Je! Ni Wako?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Utumishi Wa Painia: Je! Ni Wako?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kazi ya Upainia Inatia Nguvu Uhusiano Wetu Pamoja na Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • “Unaweza Kuwa Painia Kabisa!”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 8/98 uku. 3-6

Utumishi Wa Painia: Je! Ni Wako?

1 “Siwezi kuwazia nikifanya jambo jingine lolote. Hakika siwezi kuwazia chochote ambacho kingeleta shangwe kama hiyo.” (w97-SW 10/15 18) Ni nani aliyesema hivyo? Shahidi wa Yehova mmoja kati ya mamia ya maelfu ambao kwa furaha wamefanya utumishi wa wakati wote kuwa kazi yao ya maisha. Je! umekwisha kujiuliza katika sala ikiwa utumishi wa painia ni wako? Kwa kuwa tumejitoa kikamili kwa Yehova, tungepaswa bila shaka kufikiri ili kujua ikiwa hatungeweza kupitisha wakati mwingi zaidi tukieneza habari njema ya Ufalme. Kwa kusudi hilo, acheni tuchunguze maulizo fulani ambayo wengi hujiuliza kuhusu utumishi wa painia.

ULIZO 1 : “Inasemwa kwamba kila mtu hawezi kuwa painia. Ninaweza kujua namna gani ikiwa utumishi huo ni wangu?”

2 Jibu hutegemea hali yetu na madaraka yetu ya kibiblia. Afya na hali ya sasa ya wengi haviwaruhusu kutoa saa 90 kila mwezi kwa mahubiri. Kwa mfano, dada waaminifu wengi ni wake na mama Wakristo. Wanashiriki katika mahubiri mara kwa mara kadiri wawezavyo na kadiri hali yao inavyowaruhusu kufanya hivyo. Nafasi inapojitokeza, wao huwa mapainia wasaidizi muda wa mwezi mmoja au zaidi kila mwaka, wakivuna furaha zinazotokana na kushiriki sana katika utumishi. (Gal. 6:9) Hata ikiwa haiwezekani kwao kuwa mapainia wa wakati wote papo hapo, wanasitawisha roho ya upainia, na wahubiri hao wenye bidii wa habari njema ni baraka kwa kutaniko.

3 Kwa upande mwingine, ndugu zetu na dada zetu wengi walio na madaraka machache vya kutosha wamepanga mambo yao ili kuwa mapainia kwa kuchunguza upya mambo wanayoweka pa nafasi ya kwanza. Namna gani wewe? Je! wewe ni kijana Mkristo aliyemaliza shule? Je! wewe ni mke wa mume anayepata riziki ili kutosheleza inavyostahili mahitaji ya familia? Je! wewe ni mwenye kuoa bila mtoto chini ya utunzaji wako? Je! wewe ni mwenye kustaafu kazi ya kimwili? Kuwa painia au la ni uamuzi ambao kila mmoja anapaswa kuchukua yeye mwenyewe. Ulizo ni hili: je! unaweza kupanga maisha yako ili uwe painia?

4 Shetani anatumia mfumo wa mambo wake ili kushambulia maisha yetu kwa vikengeusha-fikira na kutudidimisha katika ubinafsi. Ikiwa tunaazimia kutokuwa sehemu ya ulimwengu, Yehova atatusaidia tuendelee kuweka faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza na kukubali mapendeleo ya utumishi ya kitheokrasi yote yanayotolewa kwetu. Ikiwa tunaweza kupanga mambo yetu ili kuwa mapainia, kwa nini tusifanye hivyo?

ULIZO 2 : “Ninawezaje kuwa hakika kwamba nitafaulu kifedha nikiwa katika utumishi wa wakati wote?”

5 Inafaa kukubali kwamba, katika nchi nyingi, saa zinazopitishwa kazini kila juma ili kupata kinachoitwa mahitaji ya lazima ya maisha zinaongezeka kadiri miaka inavyopita. Hata hivyo, wengi ni mapainia tangu miaka makumi kadhaa, na Yehova anaendelea kuwategemeza. Ili kufaulu katika utumishi wa painia, inafaa kuonyesha imani na roho ya kujinyima. (Mt. 17:20) Zaburi 34:10 inatuhakikishia kwamba ‘wao wanaotafuta BWANA [Yehova, NW] hawatakosa kitu cho chote kilicho chema.’ Yeyote anayeanza utumishi wa painia anapaswa kufanya hivyo akiwa na uhakika kamili kwamba Yehova atatosheleza mahitaji yake. Hivyo ndivyo anavyofanyia tayari mapainia waaminifu mahali pote duniani! (Zab. 37:25) Ni wazi kwamba, kulingana na kanuni zinazotolewa kwenye 2 Wathesalonike 3:8, 10 na kwenye 1 Timotheo 5:8, mapainia hawapaswi kungojea kwamba wengine wawategemeze kifedha.

6 Yeyote anayeazimia kuanza utumishi wa painia anapaswa kufuata shauri la Yesu: ‘Kuketi kwanza na kupiga hesabu ya gharama.’ (Lk. 14:28) Kutenda kwa njia hiyo ni kuonyesha hekima ifaayo. Simulia na wale ambao ni mapainia waliofaulu muda wa miaka mingi. Waulize namna Yehova anavyowategemeza. Mwangalizi wa mzunguko wenu ni painia stadi ambaye atakuwa mwenye furaha kukutolea mashauri ili kufaulu katika utumishi wa wakati wote.

7 Tusipojiweka mikononi mwa Yehova, haiwezikani kwa kweli kuhakikisha ukweli wa ahadi ya Yesu inayopatikana kwenye Mathayo 6:33. Dada mmoja painia mwaminifu alisema: “Tulipofika kwenye mgawo wetu mpya na mwenzangu tukiwa mapainia, tulikuwa na mboga kidogo tu, pakiti ya siagi, bila pesa. Tulimaliza chakula cha jioni na kusema, ‘Sasa hatuna chochote kwa ajili ya kesho.’ Tulisali kuhusu jambo hilo, tukalala. Mapema asubuhi iliyofuata Shahidi mmoja wa huko alikuja na kujitambulisha, akisema, ‘Nilisali kwamba Yehova alete mapainia. Sasa naweza kuandamana nanyi kwa sehemu kubwa ya siku, lakini kwa kuwa naishi mbali mashambani, itanibidi nile chakula cha mchana pamoja nanyi, kwa hiyo nimeleta chakula hiki tule sisi sote.’ Chakula hicho kilikuwa nyama nyingi na mboga nyingi.” Hakuna jambo la kushangaza kwamba Yesu alituhakikishia kwamba tunaweza ‘kukoma kuhangaikia nafsi zetu’! Kisha, akaongeza: “Nani kati yenu kwa kuhangaika aweza kuongeza dhiraa moja kwenye muda wake wa uhai?”​—Mt. 6:25, 27.

8 Ulimwengu wenye kutuzunguka unakuwa zaidi na zaidi wenye kupenda mambo ya kimwili. Tunapata mikazo yenye nguvu zaidi na zaidi ili kufanya kama wanavyofanya wengine wote. Hata hivyo, ikiwa kwa unyenyekevu tunathamini huduma ya wakati wote, tutaridhika na mambo machache ya kimwili. (1 Tim. 6:8) Mapainia wanaoishi maisha ya kawaida na yenye kupangwa vizuri wanao wakati mwingi zaidi wa kutoa katika huduma, wanapata furaha kubwa zaidi na ni wenye nguvu zaidi kiroho kwa kuwa wanafundisha wengine kweli. Hata ikiwa hawatafuti kuishi maisha ya kujinyima raha kabisa, maoni yao yenye usawaziko juu ya hali yao ya kiuchumi yanawawezesha kupata faida za utumishi wa painia.

9 Ikiwa sisi tunajua kwamba tunaishi siku za mwisho na kwamba wakati unakuwa mfupi kwa ulimwengu huu mwovu, tutachochewa kiroho ili tujinyime mambo inavyohitajiwa kusudi tutumie nafasi zote za kuhubiri habari njema. Kwa kuangalia hali yetu ya kifedha kwa jicho jingine (à défaut de mieux) na kwa kuweka mambo mikononi mwa Yehova, tutaona labda kwamba tunaweza kuanza utumishi wa wakati wote. Hata kama inafaa tuache tamaa fulani za mambo ya kimwili ili kuwa mapainia, tutafaidika na baraka tele za Yehova.​—Zab. 145:16.

ULIZO 3 : “Nikiwa tineja, kwa nini ningepaswa kufikiria utumishi wa painia kama chaguo la maisha?”

10 Unapokuwa ukikamilisha miaka yako ya mwisho ya shule, kama ilivyo kawaida unafikiria wakati wako ujao. Unataka wakati ujao ulio hakika, wenye furaha na wenye kutosheleza kweli kweli. Inawezekana kwamba washauri watoao mwongozo wa shule wanakuchochea ujitoe katika kazi ya maisha yenye kuleta fedha nyingi ambayo inaomba miaka mingi ya masomo kwenye chuo kikuu. Dhamiri yako iliyozoezwa vema inakuambia kwamba ungepaswa kujitayarisha kumtumikia Yehova kwa wakati wote iwezekanavyo. (Mhu. 12:1) Labda unatarajia pia kuoa na kuwa na familia. Utafanya nini?

11 Maamuzi utakayochukua kwenye kipindi hicho cha maisha yatakuwa na matokeo juu ya wakati wako ujao. Ikiwa wewe tayari ni Shahidi wa Yehova aliye wakfu na mwenye kubatizwa, umejitoa kwa Yehova kwa nafsi yako yote. (Ebr. 10:7) Nafasi ya kwanza itakapojitokeza, uwe painia msaidizi muda wa mwezi mmoja au zaidi. Hivyo, utaonja furaha na madaraka vinavyotokana na utumishi wa painia wa kawaida, na utakuwa labda na wazo kamili zaidi juu ya jinsi utakavyotumia maisha yako. Kisha, badala ya kuziba nafasi iliyo wazi inayotokezwa na mwisho wa masomo kwa kufanya kazi ya kimwili ya wakati wote, kwa nini usianze utumishi wa painia wa kawaida? Baadhi ya wale waliongoja kabla ya kuwa mapainia hujuta kuona hawakuanza mapema.

12 Ikiwa wewe ni kijana, tumia uwezekano ulio nao wa kubaki mseja na pata faida ambazo huo hutoa kwa ajili ya mahubiri ya wakati wote. Ikiwa unatamani kuoa siku fulani, hauwezi kuweka msingi bora kwa ajili ya ndoa isipokuwa unaanza kwanza utumishi wa painia wa kawaida. Kadiri unavyokua na kukomaa kiroho, labda utachagua kufanya utumishi wa painia kuwa kazi yako ya maisha pamoja na mtu aliye na tamaa iyohiyo na ambaye utaoana naye. Mapainia fulani wenye kuoana waliwekwa katika utumishi wa mzunguko au kuwa wamishonari. Namna hiyo ya maisha ni yenye kutosheleza kweli kweli!

13 Iwe kwamba wewe ni painia kwa wakati mfupi au mrefu, utakuwa umekamilisha elimu yako na kupata mazoezi yasiyolinganika ambayo hayawezi kutolewa na utendaji mwingine wowote duniani. Utumishi wa painia unatufundisha kujitia nidhamu, kupanga mambo yetu, kuwa na mwenendo mzuri pamoja na watu, kumtegemea Yehova na kusitawisha uvumilivu na fadhili, sifa zenye mafaa ili kuchukua madaraka makubwa zaidi.

14 Wanadamu hawajapata kuishi mashakani wakati wowote kama ilivyo leo. Isipokuwa yale anayoahidi Yehova, mambo yenye kudumu ni machache. Kwa kuwa wakati ujao uko wazi kabisa mbele yako, ni wakati gani bora kuliko huu utakaoupata ili kufikiri kwa uzito juu ya jinsi utakavyoishi maisha yako katika miaka ijayo? Fikiria [weigh; E-SW dict.] kwa uangalifu pendeleo la kuwa painia. Hautajuta kamwe kuwa umefanya utumishi huo kuwa kazi yako ya maisha.

ULIZO 4 : “Je! sitakuwa mara kwa mara chini ya mkazo ili kufikia kiwango cha saa kinachoombwa? Itakuwaje ikiwa mimi sifikii mradi?”

15 Mtu anapojaza ombi la kukubaliwa kama painia wa kawaida, anapaswa kujibu ulizo lifuatalo: “Je! umepanga mambo yako ili kufikia kwa kweli kiwango kinachoombwa cha saa 1 000 kwa mwaka?” Ili kufikia kiwango hicho, inafaa kutoa kwa wastani saa tatu kwa siku katika mahubiri. Hilo linaomba bila shaka programu nzuri na kujitia nidhamu. Baada ya miezi michache, mapainia wengi wanafikia kusitawisha matumizi ya wakati yenye kutumika na yaliyo hakika.

16 Hata hivyo, Mhubiri 9:11 linasema bila kukosea: ‘Wakati na [tukio lisiloonwa kimbele hu]wapata wote.’ Ugonjwa mkali au hali nyingine isiyotazamiwa vinaweza kumzuia painia asifikie mradi wake. Ikiwa tatizo halidumu na kwamba linatukia mwanzoni mwa mwaka wa utumishi, programu yenye bidii zaidi inaweza kutosha ili kukomboa wakati uliopotea. Lakini namna gani ikiwa tatizo kali linatukia, kwamba kunabaki tu miezi michache katika mwaka wa utumishi na kwamba painia hawezi tena kukomboa kuchelewa?

17 Ikiwa wewe ni mgonjwa kwa miezi michache au ikiwa, kwa sababu yenye kulazimisha isiyotokana na mapenzi yako, hauwezi kufikia mradi wa saa, unaweza kuzungumza na mshiriki mmoja wa halmashauri ya utumishi ya kutaniko na kumfasiria hali yako. Ikiwa wazee wanafikiri kwamba lingekuwa jambo lenye akili kukuruhusu uendelee na utumishi wako bila kujisumbua ili kukomboa wakati uliopotea, wanaweza kuchukua uamuzi kwa ajili ya hilo. Mwandishi atajulisha kwenye kadi ya utendaji ya mhubiri kwamba haulazimiki kukomboa kuchelewa. Hiyo si likizo, lakini badala yake ni wonyesho wa wema, kuhusiana na hali yako.​—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 1987, uku. 3, fu. 7.

18 Mapainia wenye ustadi hujiwekea akiba ya saa tangu mwanzo wa mwaka wa utumishi. Wanatoa nafasi ya kwanza kwa utumishi wao wa painia, na wakati mwingine wanaona kuwa jambo la lazima kupunguza utendaji mbalimbali wenye umaana mdogo. Ikiwa painia anachelewa kwa sababu ya kupanga mambo vibaya au kwa sababu hakujitia nidhamu ili kuheshimu programu yake, angepaswa kujisikia mwenye kulazimika kukomboa kuchelewa kwake bila kutumaini kufaidika na mpango wa pekee.

19 Wakati mwingine, inatokea kwamba hali ya painia inapatwa na badiliko lisiloweza kuepukika. Labda hataweza kufikia kiwango cha saa kinachoombwa kwa muda wa kipindi kirefu cha wakati kwa sababu ya matatizo yenye kudumu ya afya, madaraka makubwa zaidi ya kifamilia, nk. Katika hali hiyo, njia ya hekima ni kuwa tena mhubiri, huku akifanya utumishi wa painia msaidizi kila wakati hilo linapowezekana. Hakuna mpango wowote uliotayarishwa ili kuwezesha mtu fulani abaki kwenye orodha ya mapainia ikiwa hali yake haimruhusu tena kufikia mradi unaoombwa.

20 Tunatumaini kwamba mpango kwa ajili ya kutoa uangalifu wa pekee kwa wale wanaotimiza matakwa utachochea wengi zaidi waanze utumishi huo bila kujisumbua isivyofaa. Hilo lingepaswa pia kutia moyo wale walio tayari katika utumishi wa wakati wote waendelee na kazi yao hiyo ya maisha. Tunatamani kwamba mapainia wafaulu katika utumishi wao.

ULIZO 5 : “Ninapenda kutimiza jambo fulani na niwe mwenye furaha kufanya hivyo. Je! utumishi wa painia utanipa uradhi huo?”

21 Furaha ya kweli hutegemea zaidi uhusiano wetu wa karibu na wa kibinafsi pamoja na Yehova na uhakika wetu kwamba tunamtumikia kwa uaminifu. Yesu alivumilia mti wa mateso “kwa ajili ya shangwe iliyowekwa mbele yake.” (Ebr. 12:2) Kufanya mapenzi ya Mungu kulimletea furaha. (Zab. 40:8) Katika mfumo wa mambo wa sasa, tunaweza kupata furaha ya kweli ikiwa sehemu kubwa ya utendaji wetu mbalimbali inahusiana na ibada tunayomtolea Yehova. Miradi ya kiroho inatufanya tuwe na azimio kwa kuwa tunao uhakika kamili kwamba tunafanya yaliyo sawa. Furaha hupatikana kwa kutoa, na hatujui njia bora ya kujitoa kwa wengine isipokuwa kwa kuwafundisha njia ya kupata uhai udumuo milele katika ulimwengu mpya wa Mungu.​—Mdo. 20:35.

22 Painia aliyetajwa katika fungu la kwanza alisema hivyo kwa maneno haya: “Je! kwaweza kuwa na shangwe kubwa kuliko kuona mtu fulani unayejifunza naye akiwa msifaji wa Yehova mwenye bidii? Inasisimua na kutia nguvu imani kuona jinsi Neno la Mungu lilivyo na nguvu katika kuchochea watu wafanye mabadiliko katika maisha yao ili kumpendeza Yehova.” (Ona Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 15, 1997, kurasa 18-23.) Hivyo, ni nini linalokufanya uwe mwenye furaha? Ikiwa, badala ya kuchagua anasa za wakati kidogo za ulimwengu, unapendelea kufanya jitihada za kudumu na zenye kustahili, utumishi wa painia utakuletea hisia yenye kupendeza sana ya kufanya jambo fulani lenye mafaa litakalokufanya uwe mwenye furaha kweli kweli.

ULIZO 6 : “Kwa kuwa si takwa kuwa painia ili kupata uhai wa milele, si ni kwangu mwenyewe kuamua ikiwa nitakuwa painia au la?”

23 Ni kweli, uamzi wa kuwa painia ni wakoI’ve transposed. Ni Yehova peke yake awezaye kuamua juu ya hali yako ya kibinafsi. (Rom. 14:4) Anataka kwa haki umtumikie kwa moyo wako wote, kwa nafsi yako yote, kwa roho yako yote na kwa nguvu zako zote. (Mk. 12:30; Gal. 6:4, 5) Yeye hupenda mpaji mchangamfu, anayemtumikia kwa furaha, si kwa kujuta wala kwa kulazimishwa. (2 Kor. 9:7; Kol. 3:23) Unapaswa kuwa na tamaa ya kutumika kwa wakati wote kwa sababu ya upendo kwa Yehova na kwa jirani. (Mt. 9:36-38; Mk. 12:30, 31) Ikiwa hivyo ndivyo unavyohisi, basi utumishi wa painia unastahili uufikirie kwa uzito.

24 Tunatumaini kwamba yale yaliyosemwa hapa yatakusaidia upime uwezekano wako wa kuwa painia. Je! unaweza kupanga mambo yako ili uwe painia wa kawaida? Hapa chini utapata kalenda yenye kichwa “Programu ya Juma ya Painia.” Fikiria programu itakayofaa kwako na itakayokuwezesha kutoa kwa wastani saa 23 kila juma katika mahubiri. Kisha uwe na imani katika Yehova na umtumaini yeye. Kwa msaada wake, unaweza kufaulu! Yeye aliahidi: “[Nita]wamwangia ninyi baraka hata pahali hapatakuwa kuipokea.”​—Mal. 3:10.      

25 Tunauliza basi ulizo hili: “Utumishi wa painia: je! ni wako?” Ikiwa unaweza kujibu “ndiyo,” jiwekee tarehe ya kuanza utumishi wa painia wa kawaida bila kukawia, na uwe hakika kwamba Yehova atakubariki kwa kukupatia maisha yenye furaha!

[Box on page 6]

Programu ya Juma ya Painia

SIKU YA KWANZASIKU YA PILISIKU YA TATUSIKU YA NNESIKU YA TANOSIKU YA POSHOSIKU YA YENGA

AsubuhiAsubuhiAsubuhiAsubuhiAsubuhiAsubuhiAsubuhi

mahubirimahubirimahubirimahubirimahubirimahubirimahubiri

AlasiriAlasiriAlasiriAlasiriAlasiriAlasiriAlasiri

mahubirimahubirimahubirimahubirimahubirimahubirimahubiri

JioniJioniJioniJioniJioniJioniJioni

mahubirimahubirimahubirimahubirimahubirimahubirimahubiri

Andika kwa kalamu ya risasi programu ya kila siku ya juma.

Panga kutoa kwa ujumla saa 23 kila juma katika mahubiri. Jumla ya Saa za Juma ____________________

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine