Tuwaongoze Wanafunzi Kwenye Tengenezo La Yehova
1 “Ni ujumbe unaohubiriwa katika zaidi ya lugha 200. Ni ujumbe unaosikilizwa katika nchi zaidi ya 210. Ni ujumbe unaotolewa kwa watu wote, haidhuru mahali gani wanapoishi. Hiyo ni kampeni kubwa zaidi ya mahubiri ambayo haijafanywa kamwe ulimwenguni, ya ujumbe unaounganisha mamilioni ya wanadamu. Mashahidi wa Yehova wanatimiza kazi hiyo tangu zaidi ya karne moja!”
2 Ni kwa maneno hayo yanaanza maelezo ya kaseti vidio Les Témoins de Jéhovah — Un nom, une organisation. Inashikamana kujibu kwa maulizo yafuatayo: Mashahidi wa Yehova ni nani hakika? Jinsi gani utendaji wao unapangwa kitengenezo? kuongozwa? kugharimiwa? Inaonyesha waziwazi kwa wale wanaoitazama kwamba “Mashahidi wa Yehova wa ulimwenguni pote walijipanga kitengenezo na walipewa mazoezi ili kuwasaidia majirani zao kujenga imani yao katika Biblia” Voir dans vidéo-script na inawatia moyo kulithamini tengenezo la Mashahidi wa Yehova. Baada ya kuitazama kaseti hiyo, mwanafunzi mmoja wa kike alilia kwa shangwe na shukrani, na alisema: “Jinsi gani inawezekana kutokuelewa kwamba hili ni tengenezo la Mungu wa kweli Yehova?”—Ona 1 Wakorintho 14:24, 25.
3 Mwanamke mmoja tangu siku nyingi, alijifunza Biblia kwa kukatiza-katiza, lakini hakufikia kukubali kwamba Utatu Mtakatifu ni fundisho la uongo. Baadaye walimwonyesha kaseti na pia mume wake. Walishangazwa sana na filamu hiyo na waliitazama mara mbili jioni hiyohiyo. Wakati wa funzo lifuatalo, mwanamke alionyesha tamaa yake ya kuwa Shahidi. Alisema kwamba, mpaka sasa, akili yake ilikuwa inakazwa juu ya imani yake katika Utatu Mtakatifu na kwamba alikuwa anasahau kutazama tengenezo letu na wale wanaoliunda. Kaseti ilimuwezesha kuelewa kwamba alipata tengenezo la Mungu. Alitaka kuanza kuhubiri nyumba kwa nyumba bila kungoja. Walimfasiria ni hatua gani mbalimbali za kufikia ili kuwa mhubiri asiyebatizwa, baadaye alisema: “Haya twende” Alijiuzulu (kuachana) na kanisa lake, akaanza kuhubiri na alikuja kuwa stadi sana katika hoja za kutupilia mbali fundisho la Utatu Mtakatifu.
4 Inajulikana vizuri kwamba wanafunzi wa Biblia wanafanya zaidi maendeleo ya kiroho na wanakua zaidi haraka kuelekea ukomavu wanapotambua tengenezo la Yehova na wanapojiunga nalo. Jambo la maana, baada ya wanafunzi 3,000 kubatizwa kwenye Pentekote, “wakaendelea kujitoa wenyewe kwa fundisho la mitume na kushirikiana.” (Mdo. 2:42, nota, TUM) Ni jambo la lazima sana kwamba tuwasaidie wanafunzi kufanya vivyo hivyo leo. Jinsi gani?
5 Tutimize Daraka Letu: Wale wote wanaofanya wanafunzi wanapaswa kutambua kwamba wana daraka la kuongoza wanafunzi wa Biblia kwenye tengenezo la Mungu. (1 Tim. 4:16) Kila funzo lingepaswa kuwa hatua ya zaidi kuelekea siku yenye furaha ambako mwanafunzi mpya ataonyesha wakfu wa utu wake kwa Yehova kwa njia ya ubatizo wa maji. Mojawapo ya maulizo ambayo watamuuliza wakati wa sherehe ya ubatizo ni: “Je! unaelewa kwamba kwa kujiweka wakfu kwa Mungu na kwa kubatizwa unajitambulisha kuwa Shahidi wa Yehova na unajiunga na tengenezo la kimungu, linaloongozwa na roho takatifu?” Ni jambo la muhimu hivyo kwamba aelewe kwamba hawezi kumtumikia Mungu ikiwa hajiungi na kutaniko la kweli la Kikristo.—Mt. 24:45-47; Yn. 6:68; 2 Kor. 5:20.
6 Tuendelee kuzungumzia mwanafunzi juu ya kutaniko letu na tengenezo la ulimwenguni pote la Mashahidi wa Yehova. Tufanye hivyo kila juma na hilo, tangu tu funzo la kwanza. Tangu mwanzoni, tumualike mwanafunzi kwenye mikutano na tuendelee kufanya hivyo.—Ufu. 22:17.
7 Tutumie Vyombo Tunavyotolewa: Vitabu bora tulivyo navyo ili kuongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani ni broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? na kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Vichapo hivyo viwili vinakazia ulazima wa kujiunga na kutaniko. Tunasoma yafuatayo mwishoni mwa somo la 5 la broshua Anataka: “Unahitaji kuendelea kujifunza juu ya Yehova na kutii matakwa yake. Kuhuzuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova mahali unapoishi kutakusaidia kufanya hivyo.” Kitabu Ujuzi kinatia mwanafunzi moyo mara nyingi kuhudhuria kwenye mikutano. Kwenye sura 5, fungu 22, kinatoa mwaliko huu: “Mashahidi wa Yehova . . . wanakuhimiza kwa uchangamfu ushiriki nao katika kumwabudu Mungu ‘katika roho na kweli.’ (Yn. 4:24)” Tunasoma kwenye sura 12, fungu 16: “Uendelezapo funzo hili na kufanya desturi yako iwe kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova, bila shaka imani yako itatiwa nguvu hata zaidi.” Sura 16, fungu 20, inasema: “Fanya liwe zoea lako kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova.” Inaongeza: “Hili litakusaidia uelewe kisha utumie ujuzi juu ya Mungu maishani mwako na litakuletea furaha. Kuwa sehemu ya udugu wa Kikristo wa ulimwenguni pote kutakusaidia uendelee kuwa karibu na Yehova.” Sura 17 inafasiria kirefu jinsi tunaweza kupata usalama wa kweli kati ya watu wa Mungu. Tunapojifunza pamoja na watu, tunalo daraka la kutokeza sehemu hizo za kitabu.
8 Broshua Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote ni chombo chema sana kilichotolewa ili kwamba watu wafahamiane na tengenezo pekee lionekanalo ambalo Yehova anatumia siku zetu ili kutimiza mapenzi yake. Maelezo marefu kilicho nayo kuhusu huduma yetu, mikutano na tengenezo yatamtia msomaji moyo kujiunga nasi ili kuabudu Mungu. Baada tu ya kuanzisha funzo la Biblia, tunatiwa moyo kutoa kwa mwanafunzi nakala moja ya broshua hiyo ili aweze kuisoma mwenyewe. Si lazima kujifunza yenyewe pamoja naye kama tulivyokuwa tukifanya mbele.
9 Kaseti vidio fulani zinazotolewa na Sosaiti ni vyombo bora kabisa ili kuongoza wanafunzi kwenye tengenezo la Yehova. Ingekuwa vizuri kwamba waweze kutazama kaseti zifuatazo: (1) La Société du Monde Nouveau en action inarudulia filamu ya 1954 inayotokeza hali nzuri ya akili, matokeo na upendo unaochea tengenezo la Yehova; (2) Unis grâce à l’enseignement divin inaonyesha amani na umoja unaoonyeshwa wakati wa makusanyiko ya kimataifa katika Ulaya ya Mashariki, katika Amerika ya Kusini, katika Afrika na katika Asia; (3) Jusqu’aux extrémités de la terre inaadhimisha miaka 50 ya Gileadi, Shule ya Kibiblia ya Sosaiti Watchtower, na inaonyesha daraka ambalo wamishonari walitimza katika utendaji wa ulimwenguni pote wa mahubiri; (4) La fermeté des Témoins de Jéhovah face à la persécution nazie inaeleza habari ya uhodari na ushindi wa Mashahidi kuelekea mateso yenye jeuri yaliyotokezwa na Hitler; na bila shaka, (5) Les Témoins de Jéhovah — Un nom, une organisation.
10 Tuwawekee Miradi Hatua kwa Hatua kwa Ajili ya Mikutano: Imetupasa kufasiria wanafunzi kwamba tunahitaji sana mafundisho ya pekee yanayotolewa kwa njia ya funzo la Biblia la nyumbani na pia mazungumzo ya kikundi, wakati wa mikutano ya kutaniko. (Yn. 6:45) Mtu mpya anapaswa kufanya maendeleo katika ujuzi wake iwe wa Maandiko kama vile wa tengenezo. Njia moja ya kufikia hilo ni kuhudhuria kwenye mikutano. (Ebr. 10:23-25) Tangu tu mwanzo, tumualike mtu kwenye mikutano ya kutaniko. Watu wanaopendezwa tangu hivi karibuni na ukweli wanaanza kuhudhuria kwenye mikutano kabla hata ya kuwa na funzo la Biblia la kawaida. Ni kweli kwamba tunatamani kutoa mfano mzuri kwa kuwako sisi wenyewe kwa ukawaida.— Lk. 6:40; Flp. 3:17.
11 Tutoe vya kutosha habari juu ya mikutano na juu ya namna inavyoendeshwa ili kwamba mwanafunzi ajisikie vizuri kwenye mikutano. Watu wamoja wanakosa sana starehe wanapokwenda mahali fulani kwa mara ya kwanza; kwa hiyo ni jambo lenye manufaa kumshindikiza mwanafunzi kwenye Jumba la Ufalme anapohudhuria kwenye mkutano wake wa kwanza. Atajisikia mwenye starehe zaidi ikiwa tupo pamoja naye wakati atakapozungumza kwa kujuana na washiriki wa kutaniko. Zaidi ya yote, tuwe wakaribishaji wageni wenye kustahili: mwalikwa wetu anapaswa kujisikia kwamba anakaribishwa vizuri na kuwa mwenye starehe.—Mt. 7:12; Flp. 2:1-4.
12 Tumtie mwanafunzi moyo kuhudhuria kwenye kusanyiko la pekee la siku moja, kwenye kusanyiko la mzunguko au kwenye kusanyiko la wilaya tangu tu moja litakapofanyika. Labda tunaweza kwenda pamoja naye.
13 Tutokeze Shukrani: Tunasoma katika kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, uku. 92: “Kama mazungumzo yako na watu wenye kupendezwa yanaonyesha kwamba unathamini sana sana tengenezo la Yehova, itakuwa rahisi zaidi kwao wasitawishe uthamini na wataongozwa wafanye maendeleo makubwa zaidi katika kupata kumjua Yehova.” Tuseme sikuzote juu ya kutaniko letu katika maneno yenye kusifika, kamwe kwa namna yenye kuvunja moyo. (Zab. 84:10; 133:1, 3b) Katika sala tunazotoa wakati wa funzo, tuseme juu ya kutaniko na juu ya ulazima kwa mwanafunzi kujiunga kwa ukawaida nalo.—Efe. 1:15-17.
14 Bila shaka kwamba tunataka kuona wapya wanaonyesha shukrani ya kwelikweli kwa ajili ya ushirika wenye kupendeza na usalama wa kiroho tunaopata kati ya watu wa Mungu. (1 Tim. 3:15; 1 Pt. 2:17; 5:9) Tufanye yote tuwezayo ili kuongoza wanafunzi wa Neno la Mungu kwenye tengenezo la Yehova.
[Caption on page 3]
Wanafunzi wanafanya maendeleo haraka zaidi kwa upande wa kiroho wanapoliona wenyewe tengenezo
[Caption on page 4]
Tusingoje ili kuwaalika wanafunzi kwenye mikutano