Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
Sehemu 8: Kuongoza Wanafunzi Kwenye Tengenezo
1 Mradi wetu tunapoongoza mafunzo ya Biblia si kufundisha tu mafundisho yanayohusu imani lakini pia kusaidia wanafunzi wawe sehemu ya kutaniko la Kikristo. (Zek. 8:23) Broshua Mashahidi wa Yehova Wao Ni Nani? Wanaamini Nini? inaweza kutusaidia kufanya hivyo. Uwatolee wanafunzi wapya wa Biblia nakala moja ya broshua hiyo, na uwatie moyo waisome. Zaidi ya hilo, kila juma kwenye funzo la Biblia chukua dakika chache ili mjifunze jambo moja kuhusu tengenezo la Yehova.
2 Mikutano ya Kutaniko: Njia kubwa ambayo katika hiyo wanafunzi wa Biblia wanafikia kuthamini tengenezo la Yehova ni kwa kushiriki pamoja nasi kwenye mikutano ya kutaniko. (1 Kor. 14:24, 25) Hata hivyo, unaweza kuanza kuwasaidia wafahamiane na mikutano kwa kuwafafanulia mikutano mitano ya kila juma, ukizungumzia mkutano mmoja mmoja. Uwaelezee kichwa cha hotuba ya watu wote itakayotolewa. Waonyeshe habari itakayochunguzwa kwenye Funzo la Mnara wa Mlinzi na kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko. Zungumzia Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi. Unapokuwa na mgawo kwenye shule, labda unaweza kufanya mazoezi pamoja nao. Shiriki pamoja nao mambo makuu yaliyotolewa kwenye mikutano. Tumia picha katika vichapo vyetu ili kuwasaidia waone yale yanayofanyika. Kuanzia tu na funzo la kwanza uwaalike kuhudhuria mikutano.
3 Wakati Ukumbusho unapokaribia, mikusanyiko, na ziara ya mwangalizi wa mzunguko, chukua dakika chache ili kueleza na kuongeza shauku yao kuhusu mipango hiyo. Hatua kwa hatua jibu maulizo kama haya: Kwa nini sisi tunaitwa Mashahidi wa Yehova? Kwa nini tunaita mahali petu pa kukusanyikia Majumba ya Ufalme? Watumishi wa huduma na wazee wana madaraka gani? Kazi ya kuhubiri na maeneo ya kuhubiria yanapangwa namna gani? Vichapo vyetu vinachapichwa namna gani? Tengenezo linapata fedha namna gani? Ni nini madaraka ya Ofisi ya tawi na pia Baraza Linaloongoza katika kuongoza kazi?
4 Vidio Zenye Kufundisha: Njia nyingine ambayo katika hiyo wanafunzi wa Biblia wanaweza kuona tengenezo nzuri la Yehova ni kupitia vidio zetu. Vidio hizo zinaweza kuwapeleka Mpaka Miisho ya Dunia, kuwafanya wafahamiane na Ushirika Mzima wa Ndugu Ulimwenguni Pote, na kuwaonyesha jinsi Tunavyoungana Kupitia Mafundisho ya Kimungu. Mwanamke mmoja ambaye aliwahi kupokea magazeti yetu na vichapo vingine kwa miaka mitano alitoa machozi alipotazama vidio Les Témoins de Jéhovah : un nom, une organisation. Hilo lilimfanya afikie kutumainia Mashahidi waliokuwa wakimtembelea, lakini baada ya kutazama vidio hiyo, alihisi kwamba angepaswa kutumainia tengenezo pia. Funzo la kawaida likaanzishwa pamoja naye, na juma lifuatalo, alihudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme.
5 Kwa kutumia dakika chache kila juma pamoja na wanafunzi na kwa kutumia vyombo tunavyotolewa, tunaweza kuongoza hatua kwa hatua wanafunzi wa Biblia kwenye tengenezo lile moja ambalo Yehova anatumia leo.
[Maulizo ya Funzo]
1. Kwa nini ni jambo lenye faida kujifunza jambo moja kuhusu tengenezo la Yehova kila juma kwenye funzo la Biblia?
2. Namna gani unaweza kutia moyo wanafunzi wa Biblia kuhudhuria mikutano ya kutaniko?
3. Ni mambo gani yanayohusu tengenezo ambayo tunaweza kuzungumzia?
4, 5. Namna gani vidio zetu zinaweza kusaidia wanafunzi wa Biblia wathamini tengenezo?