Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/99 uku. 3-4
  • Kupainia—Matumizi Yenye Hekima ya Wakati Wetu!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kupainia—Matumizi Yenye Hekima ya Wakati Wetu!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tutafute Mapainia Wasaidizi 100,000
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Je! Tutafanya Hilo Tena?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Baraka Zinazotokana na
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Mradi Unaofaa kwa Ajili ya Mwaka Mpya wa Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 4/99 uku. 3-4

Kupainia​—Matumizi Yenye Hekima ya Wakati Wetu!

1 ‘Mimi tayari nina mambo mengi sana ya kufanya [Meaning: have too much to do]! Je! lingekuwa kweli jambo lenye hekima kwangu kuanza upainia wakati huu?’ Hivyo ndivyo alivyofikiri dada mmoja, aliposikiliza mzee painia akitoa hotuba kwenye mkusanyiko wa mzunguko; hotuba hiyo ilikuwa yenye kichwa “Kusonga Mbele Katika Huduma ya Painia.” Ndugu mmoja kijana kati ya wasikilizaji wa mkusanyiko huohuo alifikiri, ‘Yeye apataje wakati wa kupainia? Mimi si mzee, lakini tayari maisha yangu yamekwisha kujaa shughuli!’

2 Kadiri mzee huyo alivyoendelea kuzungumza juu ya baraka za kuwa painia, yeye alihoji mapainia wengi kutoka mzunguko; mapainia hao walieleza marekebisho waliyolazimika kufanya ili kupainia na jinsi Yehova alivyobariki sana jitihada zao. Mmoja alikuwa kilema, mwingine alikuwa na mwenzi asiyeamini, na yule mwingine alikuwa ameacha kazi-maisha ya ulimwengu lakini mshahara wake ulitosha kwa ajili ya mahitaji yake ya msingi. Waliposikia jinsi mapainia hao walivyofaulu kwa msaada wa Yehova, ndugu yule na dada yule kati ya wasikilizaji walianza kuchunguza upya mafikiri yao na hali zao wenyewe. Tunakualika ufanye hivyo pia, zaidi kwa kuwa saa zenye kupunguzwa zinazoombwa kwa mapainia sasa zaweza kutimizwa na wahubiri wengi zaidi wa habari njema.

3 Tunajua kwamba Yehova ndiye Muumba na Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote mzima na kwamba sisi twapata uhai wetu kwake. (Dan. 4:​17; Mdo. 17:28) Ni wazi kwetu kwamba Yehova ni mwenye kutumia tengenezo moja pekee. Tunalo pendeleo la kutumika kwa uaminifu-mshikamanifu pamoja na tengenezo hilo, tukitegemeza “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” katika kutoa ushahidi wa Ufalme kabla ya mwisho kuja. (Mt. 24:45; 25:40; 1 Pet. 2:9) Huku tukiwa wenye kuendelea zaidi sana katika “siku za mwisho,” tunatambua kwamba wakati ambao katika huo habari njema yapasa ihubiriwe waisha haraka. (2 Tim. 3:1) Wakati huohuo, twahitaji kutegemeza familia zetu kimwili. (1 Tim. 5:8) Mshahara wa mtu haulekei kutoa riziki yenye kutosha kama ilivyokuwa wakati uliopita. Huenda afya yetu isiwe kama ilivyozoea kuwa. Na kwa kusema kweli, twataka kuwa na wakati kidogo na mali ya kutumia kwa ajili yetu wenyewe. (Mhu. 3:​12, 13) Hivyo, twaweza kujiuliza ikiwa kuitikia mwito wa kupainia kwaweza kuwa jambo lenye hekima.

4 Ni daraka la kila mmoja wetu binafsi kuchunguza hali zetu wenyewe kwa makini na kuamua ikiwa tunaweza kupainia. (Rom. 14:12; Gal. 6:5) Ni jambo lenye kutia moyo kufikiria hesabu zenye kuongezeka za wale walioitikia mwito wa kupainia. Ijapokuwa mikazo na matatizo ya siku hizi za mwisho, ripoti ya utumishi iliyotangazwa katika Kitabu-Mwaka 1999 yaonyesha kwamba karibu watu 700,000 kati ya watu wa Yehova ulimwenguni pote ni wenye kusonga mbele katika huduma ya painia. Iwe kwamba wanatumika chini ya hali ngumu za kiuchumi, kwamba wanakosewa na magari ya usafirishaji, kwamba wanapata matatizo ya afya au kwamba wanapata matatizo na magumu mengine, ndugu na dada hao hawafi moyo katika kufanya lililo bora, na jambo hilo ni lenye kusifika. (Gal. 6:9) Wamekubali pendekezo la Yehova la kumjaribu yeye. (Mal. 3:​10) Wao huhisi kwamba kupainia ni matumizi yenye hekima sana ya wakati wao mchache na mali zao na kwamba Yehova amewabariki kwelikweli kwa kuwa wamefanya marekebisho yenye kuhitajika ili kuingia na kubaki katika kazi ya painia.

5 Mapainia Ni Wenye Kubarikiwa: Dada mmoja katika Cameroon aliye na binti mdogo sana afasiria: “Tangu kuzaliwa kwake, binti yangu amekuwa sikuzote akinisindikiza katika huduma. Hata kabla ya kujifunza kutembea, nilikuwa nikimbeba mgongoni, nikimfunga salama kwa kipande cha nguo. Asubuhi moja katika huduma, nilisimama kwenye meza ya biashara kando ya barabara. Mtoto wangu aliniacha, akichukua magazeti kadhaa katika mfuko wangu. Alitembea kuelekea meza nyingine iliyokuwa karibu na hapo. Ingawa yeye hangeweza kusema mengi, yeye alivuta uangalifu wa mwanamke mmoja na akapendekeza gazeti. Mwanamke huyo alishangaa tu kuona mtoto mdogo kama huyo akishiriki katika utendaji huo. Alikubali gazeti na funzo la Biblia bila kusita!”

6 Katika kuitikia mwito kwa ajili ya mapainia wasaidizi wengi zaidi, mzee mmoja na baba wa familia katika Zambia, ambaye alikuwa na kazi ya kimwili ya wakati wote, aliamua kuwa painia msaidizi ijapokuwa programu yake yenye shughuli nyingi. Yeye alitaka kutoa kielelezo kwa kutaniko na kwa familia yake. Kwenye pindi fulani, yeye angeweza kuegesha gari lake kando ya barabara na kupiga bendi (kaseti) ya kitabu Siri ya Kupata Furaya ya Familia. Alialika wapita-njia waje upande huo na kusikiliza yale yaliyokuwa yakisomwa kwa sauti kubwa. Katika njia hiyo, yeye aliweza kuachia watu vitabu Furaha ya Familia 16 na Ujuzi 13, na akaanzisha mafunzo mawili ya Biblia.

7 Roho nzuri ya upainia ilionwa pia katika nchi jirani, yaani Zimbabwe. Mnamo Aprili 1998, kutaniko moja lenye wahubiri 117 liliripoti mapainia wasaidizi 70 na mapainia wa kawaida 9. Kutaniko lingine lenye wahubiri 94 lilikuwa na mapainia wasaidizi 58 walioripoti. Kutaniko lingine pia lenye wahubiri 126 liliripoti kwamba 58 waliamua kuwa mapainia wasaidizi pamoja na wale mapainia wa kawaida 4. Mwaka wa utumishi uliopita ulithibitika kuwa wenye kutokeza sana katika Zimbabwe. Ingawa walishughulishwa sana na mambo ya familia, utendaji wa kutaniko, na ujenzi wa tawi, akina ndugu huko walikaza fikira juu ya kupitisha wakati wao kwa hekima katika huduma.

8 Mapainia hutambua kwamba kuanza kazi ya upainia na kudumu katika hiyo havitegemei nguvu zao wenyewe. Wao ni wa kwanza kukubali kwamba yoyote wanayoweza kufanya yawezekana kwa sababu wao ‘hutegemea nguvu ambazo Mungu hutoa.’ (1 Pet. 4:​11) Imani yao huwawezesha kuendeleza huduma yao kila siku. Badala ya kutafuta raha yao na hali njema yao wenyewe, mapainia wenye matokeo hutambua kwamba ili kuendelea, “kushindana sana” kwaweza kutakwa, lakini wao hupata baraka nyingi kama matokeo.​—1 Thes. 2:2.

9 Kielelezo cha Paulo Chastahili Kuigwa: Biblia yatoa habari ya mambo ambayo mtume Paulo alitimiza katika huduma na msaada mzuri alioutolea watu wengi. Hata hivyo, Paulo alikuwa mwenye shughuli sana. Yeye alivumilia mnyanyaso na matatizo ya kimwili ili ahubiri habari njema na kutia nguvu makutaniko. Alivumilia pia tatizo kali la afya. (2 Kor. 11:21-​29; 12:​7-​10) Alikuwa mwenye nia thabiti ya kupitisha wakati wake kwa hekima. Yeye alikubali kwamba alifanya kazi yake yote kwa msaada wa Yehova. (Flp. 4:​13) Hakuna mtu hata mmoja kati ya wale Paulo aliowasaidia ambaye anaweza kuwa na sababu ya kusema kwamba wakati wake na jitihada zake katika utumishi wa Yehova vilipotezwa bure au kwamba vingeweza kutumiwa kwa njia bora zaidi. Ndiyo, sisi tungali wenye kufaidika leo kutokana na kutumia wakati vizuri kwa Paulo! Twathamini kama nini shauri lake lenye kupuliziwa linalotusaidia tupambanue mambo ya kuwekwa pa nafasi ya kwanza na kushikamana na kweli katika nyakati hizi ngumu!

10 ‘Wakati ubakio kwa ajili ya kuhubiri habari njema umepunguzwa’ sasa kuliko wakati mwingine wowote. (1 Kor. 7:​29; Mt. 24:14) Kwa hiyo, ni jambo lenye kufaa kujiuliza: ‘Ikiwa kesho maisha yangu yangekwisha bila kutazamiwa, je! ningeweza kumwambia Yehova kwamba nimetumia wakati wangu kwa hekima?’ (Yak. 4:​14) Kwa nini usiseme na Yehova katika sala sasa, huku ukimhakikishia kwamba wataka kutumia wakati wako kwa hekima ukiwa mmoja wa Mashahidi wake? (Zab. 90:12) Mwombe Yehova akusaidia ufanye maisha yako kuwa rahisi. Hata ingawa huenda ulikuwa umeamua kutopainia hapo mbele, je! yawezekana kwamba sasa umetambua ya kuwa kupainia kwafaa kwa maisha yako?

11 Tumia Vizuri Zaidi Hali Zako: Ni jambo lenye kueleweka kwamba, kwa sababu ya hali, si wote wenye kutaka walio na uwezo wa kupanga saa 70 kwa mwezi ili kutumika kuwa mapainia wa kawaida. Hata hivyo, wahubiri wengi hupanga kutoa saa 50 kwa mwezi katika hudumu wakiwa mapainia wasaidizi mara nyingi iwezekanavyo au kwa kuendelea. Ikiwa hali zako hazikuruhusu kuwa painia msaidizi au wa kawaida sasa, jipe moyo. Endelea kusali ili hali zako zibadilike. Wakati huohuo, ikiwa marekebisho hayawezekani, pata burudisho kwa kujua kwamba Yehova apendezwa na yote uwezayo kufanya kwa moyo wote katika utumishi wake. (Mt. 13:23) Yeye afahamu kwamba wewe ni mwenye kusimama kwa uthabiti upande wake na kwamba unajitahidi sana kuwa mhubiri mwaminifu asiyeacha mwezi upite bila kufaidika na nafasi za kutoa ushahidi. Huenda unaweza kufanya maendeleo katika kunoa ufundi wako wa kutoa ushahidi, huku ukitumika ili kuwa mhubiri na mfundishaji bora wa habari njema.​—1 Tim. 4:​16.

12 Kwa kuwa “siku kubwa ya BWANA, yenye kuogopesha” inakaribia sana, tunahitaji kutumia wakati wenye kubaki kwa hekima ikiwa twataka kumaliza kazi tuliyoamuriwa kufanya. (Yoe. 2:​31) Shetani anajua kwamba wakati wake ni mfupi na, sasa kuliko wakati mwingine wowote, yeye anajaribu yote awezayo ili kufanya maisha yetu yawe magumu na kufanya iwe vigumu kwetu kukaza fikira juu ya mambo yaliyo ya lazima kwelikweli. (Flp. 1:​10; Ufu. 12:12) Usidharau jambo la kwamba Mungu anapendezwa nawe. Yehova aweza kukusaidia ufanye maisha yako kuwa rahisi na kufanya yote uwezayo katika huduma. (Zab. 145:16) Kwa furaha, wengi ni wenye kutambua, wanapochunguza upya hali zao, kwamba wanaweza kujiunga kwenye mstari wa mapainia wasaidizi au wa kawaida. Ndiyo, mapainia hupata kutosheka kwenye kina kirefu katika kutumia wakati wao kwa hekima. Je! utakuwa mmoja wao?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine