Tutolee Magazeti Siku Ya Posho Ya 1 Na Ya 3 Ya Kila Mwezi
1 Tangu miaka 118, Mnara wa Mlinzi, kama vile mwanasheria mwenye uwezo, linatetea kweli na mafundisho ya kibiblia. Liliweza hivyo kupata kutumainiwa na mamilioni ya wasomaji wenye shukrani. Sikuzote ni chombo cha kwanza kinachotumiwa na mtumwa mwaminifu na mwenye akili ili kutangaza Ufalme uliowekwa na Yehova na kugawanya chakula cha kiroho ‘kwa wakati ufaao.’—Mt. 24:14, 45.
2 Tangu kutangazwa kwalo Oktoba 1, 1919 kwa jina l’Âge d’or, leo Amkeni!, gazeti hilo linakazia ulazima wa kuamsha watu kuhusu maana ya matukio ya ulimwengu. Linazungumzia makala mbalimbali na zenye kutenda kazi zinazojitofautisha kwa hali yayo ya usawaziko na uchambuzi wa mambo kwa undani. Makala hizo zinavutia uangalifu wa msomaji juu ya ujumbe ulio wa maana zaidi wa gazeti hilo, kwamba matukio ya ulimwengu yanatimiza unabii mbalimbali wa Biblia, unaotangaza kwamba tunaishi siku za mwisho na kwamba, karibuni, Ufalme wa Mungu utamimina baraka za milele juu ya wale wanaofanya mapenzi ya Mungu.
3 Kwa sasa, Mnara wa Mlinzi linatangazwa katika lugha 125 na kuchapwa nakala 20,980,000 kila mwezi na halafu Amkeni! linatangazwa katika lugha 82 na kutolewa kila mwezi nakala 18,350,000. Katika eneo letu, Mnara wa Mlinzi katika rangi linatolewa katika Lingala, Swahili na Tshiluba na kunapatikana chapa katika Kiluba, Kirundi, Monokutuba na Otetela. Mwaka jana, kila mhubiri aliangusha kwa wastani gazeti 0.3 kila mwezi. Tunaweza kufanya nini ili kuongeza uangushaji wa magazeti katika eneo letu?
4 Kwanza kabisa, tunapaswa kutambua kwamba uangushaji wa vichapo ni wa muhimu pia kama vile mahubiri ya mdomoni. Baadaye, tunapaswa kujiwekea mradi wa kuangusha sehemu ya kutosha ya magazeti kila mwezi. Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1994 lilikuwa na dokezo lifuatalo: “Wahubiri wanaweza kuwa na mradi wa magazeti 10 hivi kila mwezi, ikitegemea hali zao; huenda mapainia wakajitahidi kufikia 90.”
5 Ili kufikia miradi hiyo, kila kutaniko lingepaswa kupanga siku ya magazeti, hasa Siku ya Posho ya kwanza na ya tatu ya kila mwezi. Ikiwa kukutana kwa ajili ya utumishi kunapangwa kila asubuhi, kisha-mchana na mwanzoni mwa jioni, matokeo yatakuwa ni kampeni yenye kutegemezwa. Wapi tunaweza kutolea magazeti?
6 Mahali panapotembelewa zaidi na watu panafaa vizuri zaidi. Tunaweza kusimama kwenye njia panda ya barabara nyingi na kutolea magazeti kwa wapita-njia. Maduka makubwa, maduka madogo na nafasi za soko ni pia mahali pafaapo ili kutolea magazeti. Mapainia wamoja wanatolea magazeti hata katika nyumba za pombe na wanapata matokeo mazuri.
7 Tunaweza pia kutolea magazeti kwa washiriki wasioamini wa familia yetu, kwa marafiki zetu, kwa majirani zetu au kwa wafanyakazi wenzetu. Tufanye pia kwamba kila mwanafunzi wa Biblia awe na nakala yake ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Wanafunzi wa Biblia wanaweza kuwa sehemu ya njia yetu ya magazeti zaidi ya watu wengine.
8 Kwa kuwa tunaruhusiwa kuhubiri peupe, tutumie uwezekano wote tunaotolewa. Vichapo vinasema vizuri zaidi na kuliko vile tunaweza kusema kwa dakika chache. Ili kupata matokeo mazuri, tunapaswa kusoma magazeti mbele ya wakati, kutafuta habari inayoweza kupendeza tabaka hii au ile ya watu, kusema kwa kifupi na wazi, kusema polepole, kuwa na kicheko cha urafiki, kuwa mwenye shauku na mchangamfu, kufanya utoaji wenye kusimamia gazeti moja tu ijapokuwa tunatolea mengi. Wakati toleo halikubaliwi, inafaa kukatiza utoaji kwa kumaliza kwa maneno ya kirafiki na kwa maoni yafaayo.
9 Ni kweli kwamba tunaathiriwa (tunaguswa) na matatizo ya kiuchumi. Hata hivyo, ikiwa tunajikaza sikuzote kuwa na magazeti pamoja nasi mahali popote tunapokwenda na ikiwa tunayatolea kwa matokeo, bidii yetu bila shaka itabarikiwa na itatuletea shangwe kubwa. Tupange basi mambo ili kuangusha hivyo magazeti Siku ya Posho ya kwanza na ya tatu ya kila mwezi. Ikiwa agizo la kutaniko letu ni dhaifu, tulirekebishe kulingana na mradi huo mpya kupatana na agizo la kila mhubiri.
10 Wazee wanaombwa kuzingatia moyoni mpango huo. Wakati wa ziara zao katika makutaniko, waangalizi wasafiri wataangalia ili kupanga ugawaji wa magazeti Siku ya Posho ya juma la pekee. Ikiwa kila mhubiri anaazimia kwa imara kuangusha magazeti kila mwezi, tutagusa wakaaji zaidi wa eneo letu, na vichapo hivyo vitafanya kazi nafasi yetu.
11 Tusiwe na haya ya kutolea magazeti kila mahali na kwa wakati wowote. Wamishonari na pia ndugu wazee-wazee wa Baraza linaloongoza wanafanya kazi hiyo kwa shangwe tangu miaka mingi. Kielelezo chao kinatutia sote moyo. Kwa mfano wa mtume Paulo, tunataka kuweza kusema: “Sioni haya kwa habari njema; kwa sababu ni uwezo wa Mungu hata wokovu kwa kila mutu anayeamini.” — Rom. 1:16, ZSB.