Majibu Kwa Maulizo Yenu
◼ Katika nini tunapaswa kujionyesha wenye busara tunapokuwa na mtu wa jinsia nyingine katika mpango wa huduma yetu?
Tunazo sababu zote za kuamini kwamba ndugu na dada zetu wanataka kuwa na mwenendo unaolingana na kanuni za adili za hali ya juu iwezekanavyo. Ole ni kwamba, tunaishi katika ulimwengu mchafu ndani yake kila kitu kinaruhusiwa na vizuizi vya adili vinakuwa haba. Ni kwa sababu hiyo, hata ikiwa tuna maoni mazuri, imetupasa kila mara kuwa waangalifu ili kutoleta suto (haya) wala kutenda kwa namna iliyopotoka. Hilo ni kweli hasa katika mpango wa mahubiri.
Katika mahubiri, tunakutana mara nyingi na watu wa jinsia nyingine wanaoonyesha kupendezwa na ukweli kunakoonekana kuwa kunyofu. Ikiwa tunahubiri wenyewe na kwamba mtu wa jinsia nyingine ni mwenyewe pia nyumbani kwake, kwa ujumla itakuwa vizuri kutoa ushuhuda mlangoni na kutokuingia nyumbani mwake. Ikiwa kuna kupendezwa, tutaweza kuchukua mipango ili kurudi kumuona tukishindikizwa na mhubiri mwingine au kwa wakati ambao wakaaji wengine wa nyumbani watakapokuwapo. Ikiwa haiwezekani, itakuwa ni kutenda kwa hekima kufanya atembelewe upya na mtu wa jinsia yake. Mashauri hayo yanahusu pia mafunzo ya Biblia yanayoongozwa pamoja na mtu wa jinsia nyingine.—Mt. 10:16.
Busara inahitajiwa pia wakati tunapochagua mshiriki kwa ajili ya mahubiri. Ijapokuwa wahubiri wawili wa jinsia tofauti wanaweza kupatana ili kuhubiri pamoja mara kwa mara, ni vizuri zaidi wajiunge na kikundi. Kwa ujumla, kupitisha wakati mwenyewe pamoja na mtu wa jinsia nyingine asiyekuwa mwenzi wetu wa ndoa si hekima, hata katika mpango wa huduma. Kwa hiyo, ndugu anayeshughulika na kugawa kikundi ataonyesha uamuzi wa hekima kwa kuchanga wahubiri, kutia ndani na matineja.
Kwa kuwa sikuzote na busara, ‘hatutatoa sababu yoyote ya kukwaza’ wala kwa sisi wenyewe wala kwa wengine.—2 Kor. 6:3.