Matangazo
◼ Vichapo vya kutolea mnamo Oktoba: Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Novemba: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ikiwa mtu fulani anaonyesha kupendezwa wakati wa ziara za kurudia, itawezekana kumtolea uandikisho. Katika sehemu ya mwisho ya mwezi, tutagawa trakti Habari za Ufalme Na. 35. Desemba: Ugawaji wa trakti Habari za Ufalme Na. 35. Makutaniko ambayo yametembelea eneo lote na kuacha nakala moja ya trakti Habari za Ufalme Na. 35 kwa washiriki wa kila familia au nyumba wanaweza kutolea kitabu Ujuzi. Januari: Tafsiri ya Ulimwengu Mpya na pia kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
◼ Watu wanaoshirikiana na kutaniko fulani wanapaswa kutuma kupitia kutaniko uandikisho wowote au uandikisho mpya kwenye Mnara wa Mlinzi au kwenye Amkeni! kutia ndani na uandikisho wao.
◼ Sosaiti haihudumii maombi ya watu kibinafsi ya vichapo vya wahubiri. Mwangalizi-msimamizi atapanga kwamba tangazo litolewe kila mwezi kabla ya ombi la vichapo la kila mwezi la kutaniko halijatumwa kwenye Sosaiti. Hilo litawezesha wale wote wanaotamani kupata vifaa kwa matumizi yao wenyewe kumjulisha ndugu anayeshughulika na vitabu. Tafadhali kumbukeni ni vifaa gani vya kuomba kwenye ombi la pekee.
◼ Makala “Majibu kwa Maulizo Yenu” ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 1997 ilitutia moyo kuwa wenye busara kuhusu mahubiri pamoja na wahubiri wa jinsia tofauti. Kuna sababu nzuri ili kwamba wote waonyeshe uamuzi mzuri kwa upande huo. Hilo halimaanishi kwamba waangalizi wasafiri, au hata ndugu wengine, hawapaswi kuhubiri pamoja na dada. Badala yake, wazo la kulinda akilini ni kwamba si hekima kwamba ndugu fulani apitishe kikawaida wakati peke yake pamoja na mtu yule yule wa jinsia nyingine na ambaye si wa familia yake.
◼ Vichapo vipya vinavyopatikana:
Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele — Lingala
Mabuku ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! 1996 — Kiingereza, Kifaransa