Mikutano Ya Utumishi Ya Machi
Juma Toka Machi 2
Wimbo 166
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “Mashahidi wa Yehova: Waeneza-evangeli wa Kweli.” Kwa maulizo na majibu. Rudilieni kisanduku cha Mnara wa Mlinzi wa Septemba 1, 1992, uku. 19.
Dak. 20: “Tualike Yeyote Aliye na Kiu.” Rudilieni makala na onyesheni katika mambo gani mautoaji yanayodokezwa yamefanywa ili kuamsha kupendezwa kwa wasikilizaji na kuwachochea. Onyesho likifanywa na mtu mwenye umri mkubwa kwa msingi wa maf. 2-3 au 4-5 na lingine likifanywa na mhubiri kijana kwa msingi wa fu. 6
Wimbo 208 na sala ya mwisho.
Juma Toka Machi 9
Wimbo 96
Dak. 10: Matangazo. Hali ya akaunti.
Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 20: “Tuhubiri Watu wa Lugha Zote na Dini Zote.” (maf. 1-10) Kwa maulizo na majibu. Fanyeni orodha ya lugha zinazozungumzwa zaidi sana katika eneo lenu na onyesheni vichapo vinavyoambatana vilivyo katika stoki ya kutaniko. Onyesho, kwa msingi wa fu. 10, likionyesha utumiaji wa broshua Une bonne nouvelle pour toutes les nations.
Wimbo 220 na sala ya mwisho.
Juma Toka Machi 16
Wimbo 75
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 12: Kwa Nini Tunahitaji Kuhudhuria Kwenye Mikutano ya Kutaniko. Mzee mmoja anachunguza mambo makuu ya Mnara wa Mlinzi wa Agosti 15, 1993, kur. 8-11, na anatia mkazo juu ya ulazima wa kuhudhuria kikawaida kwenye mikutano yote.
Dak. 18: “Tuhubiri Watu wa Lugha Zote na Dini Zote.” (maf. 11-27) Kwa maulizo na majibu. Onyesheni dini zisizo za Kikristo zinazozoewa katika eneo. Onyesho likifanywa na mhubiri mwenye ujuzi juu ya namna ya kumkaribia kwa mara ya kwanza mshiriki wa dini yenye kuenea zaidi katika eneo, iwe ni mbudha, mhindu, myahudi au mwislamu.
Dak. 10: “Yehova Ni Msaidiaji Wangu.” Hotuba changamfu na yenye kutia moyo ikitolewa na mzee.
Wimbo 15 na sala ya mwisho.
Juma Toka Machi 23
Wimbo 4
Dak. 10: Matangazo. Zungumzieni vichapo tutakavyotolea mnamo Aprili. Dokezeni wazo moja au mawili ili kutolea kitabu Ujuzi kwa msaada wa uku. 8 wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996. Kazieni kwamba mradi wetu ni kuanzisha mafunzo ya Biblia.
Dak. 15: “Ikiwa Utoaji Ni Wenye Matokeo, Utumieni!” Kwa maulizo na majibu. Omba mhubiri mmoja au wawili wenye ujuzi waseme kwa kifupi, kutoka mahali pao, mautoaji ambayo wanaendelea kutumia kwa sababu ya urahisi wayo na matokeo yaliyopatikana. Baadaye, wahubiri wengine watajulisha matangulizi yaliyodokezwa karibuni katika Huduma Yetu ya Ufalme wanayoyaona kuwa yenye matokeo.
Dak. 20: Tujizoeze Kutoa Ujumbe. Hotuba fupi ikitegemea kitabu Kiongozi cha Shule, kur. 98-9, maf. 8-9. Tieni mkazo juu ya ulazima wa kuchunguza mautoaji yetu na kutafuta njia za kuwa wenye matokeo zaidi. Dada wawili wanaonyesha namna wanavyofikiri juu ya yale waliyosema kwenye mlango na wanazungumzia yale ambayo wangeweza kuboresha. Wanafanya pia kipindi kifupi cha mazoezi ili kujaribu utangulizi watakaotumia wakati ujao na wanabadilishana madokezo yafaayo. Ndugu anayeongoza sehemu hii anamalizia kwa kutia moyo wahubiri wote wachunguze mautoaji yao na kujizoeza.
Wimbo 103 na sala ya mwisho.
Juma Toka Machi 30
Kutaniko litatayarisha programu yalo lenyewe, itakayotia ndani habari juu ya mwadhimisho wa Ukumbusho Siku ya Posho, Aprili 11, 1998. Mtapata habari zenye kufaa katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1996.