Habari Za Kitheokrasi
Angola: Mnamo Desemba, kilele kipya cha wahubiri 35 034 kilifikiwa.
Bangladesh: Kusanyiko la wilaya “Imani Katika Neno la Mungu” lililofanywa Dacca lilikusanya hudhurio kubwa zaidi la watu 142, na kulikuwako watu 14 waliobatizwa. Hilo linaonyesha zaidi ya mara mbili hesabu ya watu ambao wamepata kubatizwa mara moja wakati wowote Bangladesh.
Bénin: Kwenye makusanyiko ya wilaya “Imani Katika Neno la Mungu,” wahudhuriaji 15 633 walihesabiwa, na watu 403 walibatizwa. Ripoti ya Desemba inaonyesha hesabu ambayo haijafikiwa kamwe ya wahubiri 5 351.
Liberia: Mnamo Desemba, kusanyiko zuri ajabu lilifanywa Monrovia: watu 5 158 walihudhuria. Mwezi uohuo, wahubiri 2 127 walitoa ripoti, jambo linaloonyesha hesabu kubwa sana.
Madagascar: Ongezeko la asilimia 11 la hesabu ya wahubiri liliripotiwa mnamo Desemba kwa kulinganisha na mwaka uliopita, kwa sababu watu 9 226 walishiriki katika mahubiri.
Saint-Martin: Hesabu isiyolinganika ya wahubiri 265 mnamo Desemba, likiwa ni ongezeko la asilimia 10 kwa kulinganisha na wastani wa mwaka uliopita. Waliongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani 310.