Habari Za Kitheokrasi
◼ Matawi ya visiwa fulani fulani vya sehemu mbalimbali za dunia yaliripoti vilele vipya vyenye kutokeza vya hesabu ya wahubiri mnamo Januari. Vinavyohusika, ni pamoja na Haïti, Martinique, Maurice, Ufilipino, Jamhuri ya Dominika, Taïwan na Trinidad.
◼ Katika Shelisheli, ongezeko la asilimia 18 kwa kulinganisha na wastani wa mwaka uliopita lilirekodiwa. Kwenye St. Maarten, lilikuwa la asilimia 16.
◼ Katika Hong Kong, wahubiri walitoa kwa wastani saa 12.7 katika mahubiri.
◼ Katika Taïwan, Jumba la Ufalme la kwanza lililojengwa kwa kufuata ujenzi wa haraka lilikamilishwa mnamo Februari.
◼ Kikundi cha watumishi wa kimataifa kilisaidia Halmashauri ya Ujenzi ya Bujumbura, Burundi, kujenga Jumba la Ufalme la kwanza ambalo kazi zake zilikamilishwa mwishoni mwa Aprili 1998.