Mikutano Ya Utumishi Ya Julai
TAARIFA: Huduma Yetu ya Ufalme itakuwa na programu ya mkutano wa utumishi kila juma wakati wa makusanyiko. Makutaniko yatafanya mabadiliko yanayohitajiwa kwenye programu hiyo kwa kufikiria jambo la kwamba yatahudhuria kwenye kusanyiko “Njia ya Mungu ya Maisha” na kwamba, kwenye mkutano wa utumishi utakaofanyika juma litakalofuata, yatajikumbusha mambo makuu ya programu kwa dakika 30. Kujikumbusha huko siku moja moja ya kusanyiko kutagawiwa kimbele kwa ndugu wawili au watatu wenye ustadi watakaoonyesha mawazo makuu. Kukiwa kumetayarishwa vizuri, kujikumbusha huko kutasaidia washiriki wa kutaniko wakumbuke mawazo ya maana, hivi kwamba wayatumie kibinafsi na katika mahubiri. Maelezo ya wasikilizaji na mambo yaliyoonwa yatakayorudiliwa yatakuwa mafupi na ya waziwazi.
Juma Toka Julai 6
Wimbo 223
Dak. 8: Matangazo. Matangazo yaliyochaguliwa ya Huduma Yetu ya Ufalme. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “ ‘Wenye Kuandaliwa Vifaa Kikamili kwa Ajili ya Kila Kazi Njema.’ ” Kwa maulizo na majibu. Toa kwa kifupi maelezo ya Mnara wa Mlinzi wa Februari 15, 1989, kur. 22-4.
Dak. 22: “Tuhubiri kwa ‘Watu wa Namna Zote.’ ” Mzee mmoja anaonyesha kwamba, ingawa tutatolea vitabu fulani vyenye kurasa 192 mnamo Julai, tunaweza kutolea vitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi au Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu hilo linapoonekana lenye kufaa. Mzee mmoja na wahubiri fulani wenye ustadi wanazungumzia madokezo yaliyopendekezwa. Sema kwa kifupi ni dini gani ambazo hupatikana katika eneo lenu na fasiria kwa nini tungepaswa kuwa tumetayarisha wazo fulani kwa ajili ya kuanzisha mazungumzo katika kila kisa. Fanyeni onyesho moja au mawili mafupi.
Wimbo 112 na sala ya mwisho.
Juma Toka Julai 13
Wimbo 209
Dak. 10: Matangazo. Hali ya akaunti.
Dak. 15: “Wanashughulika na Mali ya Bwana-Mkubwa.” Hotuba inayotolewa na mzee ambayo itarudilia habari ya nyongeza.
Dak. 20: “Sisi Sote Ni Wenye Manufaa kwa Ajili ya Kutimiza Kazi.” Kwa maulizo na majibu. Fasiria kwa nini wazee wanahitaji wenye kujipendea wengi ili kufanya kazi zinazohitajika. Simulia juu ya mahitaji ya kutaniko, kutia ndani usafishaji na utengenezaji wa Jumba la Ufalme, msaada kwa wagonjwa na watu wazee-wazee na mahubiri katika eneo lote. Alika wazee waseme namna wanavyothamini msaada ambao wengi hutoa kwa kujipendea. Onyesha kwamba jitihada za kila mmoja ni za maana sana.
Wimbo 153 na sala ya mwisho.
Juma Toka Julai 20
Wimbo 7
Dak. 10: Matangazo.
Dak. 20: Jitahidini. Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1986, kur. 10-14. Sema juu ya umaana wa utumishi wa painia wa kawaida na tia wahubiri moyo waanze utumishi huo Septemba 1.
Dak. 15: “Tutoe Ushahidi Kupitia Mwenendo Mzuri.” Kwa maulizo na majibu. Hoji vijana fulani wenye mfano mzuri. Watasema namna watu wengine walivyoguswa moyo ifaavyo na mwenendo wao wa Kikristo. Eleza jambo moja au mawili yaliyoonwa kutokana na Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1995, kur. 24-5.
Wimbo 170 na sala ya mwisho.
Juma Toka Julai 27
Wimbo 61
Dak. 10: Matangazo. Kumbusha kila mmoja atoe ripoti yake ya Julai.
Dak. 15: Namna ya Kufanya Njia ya Ugawaji wa Magazeti. Tia mkazo juu ya kile kinachohitajiwa: kuandika magazeti yote yaliyoachwa, kurudi katika majuma mawili yanayofuata, kutoa mawazo mapya ya namba za mwisho ili kuendeleza kupendezwa. Sema kwamba majirani, wafanyakazi wenzetu, wafanyabiashara, wafanyakazi wa vituo vya mafuta ya motokaa, nk. wanaweza kutiwa katika njia ya ugawaji. Pendekeza uandikishaji wa miezi sita kwa wale wanaoonyesha kupendezwa kwenye kudumu. Alika mhubiri mmoja au wawili waeleze jambo lililoonwa lenye kutia moyo kuhusiana na njia za ugawaji.
Dak. 20: Mapainia Husaidia Wengine. Hotuba inayotolewa na mwangalizi wa utumishi, ambayo wakati wa hiyo atazungumzia mpango ambao kupitia huo mapainia watatoa msaada wa kibinafsi kwa wahubiri. Fasiria kwamba programu za msaada zilikwisha kuanzishwa wakati wa zamani. (jv-SW uku 100) Wale wapya zaidi ya milioni moja waliobatizwa mnamo miaka mitatu iliyopita wanahitaji kuzoezwa. Programu “Mapainia Husaidia Wengine” inahitaji ustadi na mazoezi ya mapainia wa kawaida na wa pekee waliohudhuria kwenye Shule ya Mapainia. Kusudi ni kwamba kila painia asaidie wahubiri wawili kila mwaka wawe wenye ustadi zaidi katika huduma na watake kuishiriki zaidi na zaidi. Wale wanaopokea msaada huo hawana sababu yoyote ya kuhangaika; kusudi ni kutia moyo kwa upendo na wema. Programu hiyo ingepaswa kuwezesha mamia ya maelfu ya Wakristo kuwa wahudumu wenye matokeo zaidi.
Wimbo 207 na sala ya mwisho.