Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/98 uku. 1
  • Ni Vizuri Kwetu Kuwako Sikuzote!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ni Vizuri Kwetu Kuwako Sikuzote!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sababu Gani Tunapaswa Kukusanyika Pamoja Ili Kuabudu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Utapata Faida Gani Kama Unaenda ku Mikutano ya Mashahidi wa Yehova?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Programu ya Familia—Mikutano ya Kutaniko
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Jinsi ya kupata furaha nyingi zaidi kutokana na mikutano
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 8/98 uku. 1

Ni Vizuri Kwetu Kuwako Sikuzote!

1 Muda wa makumi mengi ya miaka, haikuwezekana kwa ndugu zetu wengi wa Ulaya ya Mashariki kukusanyika peupe. Fikiria furaha yao siku ilipowezekana kufanya hivyo katika uhuru wote, marufuku yalipoondolewa!

2 Mwangalizi mmoja wa mzunguko aliandika hivi kuhusu kutaniko moja alilozuru: “Siku ya Pili jioni, baada ya mimi tu kufika, chombo cha kupasha moto kiliharibika. Nje kulikuwa theluji, na katika jumba hali-joto ilikuwa yenye digrii za Selsio 5. Ndugu walivaa makoti, shali (écharpe), mifuko ya mikono, kofia na viatu vikubwa. Hakuna mtu ambaye angaliweza kufuata katika Biblia, kwa kuwa haikuwezekana kufungua kurasa. Jukwani, nikiwa katika koti langu, nilikauka kwa baridi hadi mifupani na niliona pumzi yangu kila wakati niliposema. Lakini jambo lililonigusa moyoni ni kwamba sikusikia hata neno moja la nung’uniko. Wote walisema kwamba walikuwa wenye furaha kuwako!” Kukosa mkutano hakukuja hata akilini mwa ndugu hao!

3 Je! Sisi Tunafikiri Kama Wao? Je! tunapenda furaha ya kukutana pamoja kwa uhuru kila juma? Au tunahudhuria mikutano tu hali zinapokuwa zenye kufaa? Linaweza kuwa jambo gumu kuhudhuria kikawaida na inaweza kuwa kwamba hatukuhudhuria kwa sababu nzuri. Hata hivyo, tufikiri juu ya wale ambao, kati yetu, wanajua umaana wa mikutano na ambao huwako karibu sikuzote, ujapokuwa umri wao, matatizo makubwa ya afya, ulemavu wa kimwili, saa za kazi zenye kuchosha na madaraka makubwa. Tuige mifano hiyo myema!​—Ona Luka 2:37. 

4 Tufanye yawe mazoea yetu kutegemeza ibada ya kweli kwa kuhudhuria mikutano yote, tangu funzo la kitabu dogo hadi makusanyiko ya wilaya makubwa. Kwa nini tuchukue mikutano hiyo kwa uzito? Kwa kuwa kukusanyika ni amri ya kimungu. Lakini kuna sababu zingine za maana. Sote tunahitaji faida za kufunzwa na Mungu, na pia msaada wa roho takatifu. Na hayo ndiyo mambo tunayopokea kwenye mikutano. (Mt. 18:20) Zaidi ya hayo, tunajengwa kupitia vitia-moyo tunavyobadilishana na ndugu na dada zetu.​—Ebr. 10:24, 25.

5 Wakati wa mgeuko-sura, Petro alisema: “Mfunzi, ni vizuri kwetu kuwa hapa.” (Lk. 9:33) Tungepaswa kuwa na hisia iyohiyo kuhusiana na mikutano yetu ya Kikristo. Ndiyo, ni vizuri kwetu kuwako sikuzote!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine