Tunaweza Kufanya Kazi Kubwa Zaidi
1 Kazi za ajabu zilitambulisha huduma ya Yesu Kristo. Yeye alilisha kimuujiza maelfu ya watu, aliponya wengi, na alirudisha wengine kwenye uhai. (Mt. 8:1-17; 14:14-21; Yn. 11:38-44) Utendaji wake ulivuta uangalifu wa taifa zima. Hata hivyo, usiku wa mwisho kabla ya kifo chake, yeye aliwaambia wafuasi wake waaminifu: “Yeye ambaye hudhihirisha imani katika mimi, huyo pia atafanya kazi ambazo mimi hufanya; naye atafanya kazi kubwa zaidi ya hizi.” (Yn. 14:12) Tunawezaje kufanya kazi “kubwa zaidi”?
2 Kwa Kutembelea Eneo Kubwa Zaidi: Eneo la utendaji la Yesu lilikomea Palestina; lakini aliwaambia wanafunzi wa mapema kwamba wawe mashahidi wake “hadi sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia,” yaani mbali kupita mahali ambapo yeye mwenyewe alihubiri. (Mdo. 1:8) Kazi ya kuhubiri aliyoanzisha ni yenye kutimizwa ulimwenguni pote leo, ni kusema katika mabara 232. (Mt. 24:14) Je! tunashiriki kikamili katika kazi hiyo kwa kutembelea eneo lote la kutaniko letu?
3 Kwa Kufikia Watu Wengi Zaidi: Wanafunzi ambao Yesu aliachia kazi ya kuhubiri walikuwa wachache vya kutosha. Hata hivyo, kwa sababu ya mahubiri yao yenye bidii, nafsi zipatazo elfu tatu zilikubali kweli na kubatizwa kwenye Pentekoste 33 W.K. (Mdo. 2:1-11, 37-41) Kukusanywa kwa wale ‘walio na mwelekeo ufaao kwa ajili ya uhai udumuo milele’ kumeendelea hadi wakati wetu, ambapo tunabatiza kwa wastani watu zaidi ya 1 000 kwa siku. (Mdo. 13:48) Je! tunafanya yote tuwezayo ili kufikia watu wenye moyo mnyofu mahali popote wanapopatikana na kukomaza kupendezwa haraka iwezekanavyo?
4 Kwa Kuhubiri Wakati Mrefu Zaidi: Huduma ya kidunia ya Yesu ilidumu miaka mitatu na nusu tu. Wengi wetu tumekuwa tukihubiri wakati mrefu zaidi kuliko huo. Bila kujali ni kwa wakati gani tutaruhusiwa kuendelea kuhubiri, sisi ni wenye shukrani kwa kusaidia mwanafunzi fulani mpya aanze kutembea kwenye njia iongozayo kwenye uhai. (Mt. 7:14) Je! kila mwezi tunayo mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana?—1 Kor. 15:58.
5 Tukiwa wanafunzi wa kweli wa Yesu, tunaweza kuwa hakika kwamba, kwa msaada wake, tutaendelea kufanya kazi kubwa zaidi.—Mt. 28:19, 20.