Tujizoeze Kujua Ndugu Zetu
1 Kulingana na Biblia, rafiki wa kweli huambatana na mtu kuliko ndugu; urafiki wake na uaminifu wake ni vya wakati wote, naye humsaidia mwenziwe wakati wa taabu. (Mez. 17:17; 18:24) Hatutawakosa marafiki wa jinsi hiyo katika kutaniko ikiwa tunajitahidi kujizoeza kujuana na kupendana.—Yn. 13:35.
2 Nafasi nzuri za kujua ndugu zetu vizuri zaidi hupatikana kabla na baada ya mikutano. Kwa nini tusifike mapema na kubaki wakati kidogo baada ya mikutano ili kufurahia ushirika mchangumfu na wenye kuchochea? Tukaribie ndugu mbalimbali ili kuongea nao, zaidi wazee-wazee wenye uzoefu, vijana au wengine wanaohisi haya.
3 Tuanzishe Mazungumzo: Tusiwasalimu ndugu zetu kwa kupita tu. Tunaweza kuanzisha mazungumzo kwa kusema jambo lililoonwa katika mahubiri, wazo lenye kupendeza lililozungumziwa katika gazeti la karibuni, au kuhusu mkutano unaotoka tu kumalizika. Tutajifunza mengi kuhusu ndugu zetu kwa kuwasikiliza, kwa kuwatia moyo waseme juu ya mambo yao yaliyoonwa na mambo wanayojifunza. Kuuliza tu mtu jinsi alivyokuja kumjua Yehova kunaweza kutufunulia mambo mengi. Wengine wamepita katika magumu yaliyotia nguvu imani yao, lakini wengine ni wenye kuvumilia sasa hali ambazo wengi hawangeweza kufikiria. Tukitambua hilo, tutatenda kama marafiki wa kweli walio wepesi kuona mahitaji ya wengine na kufanya jambo fulani.
4 Tuwe Wenye Kuthamini Ndugu Zetu: Baada ya kifo cha binti wake mdogo, dada mmoja alipata ugumu wa kuimba nyimbo za Ufalme zilizohusu ufufuo. Yeye akumbuka: “Pindi moja, dada mmoja aliyekuwa akiketi katika safu nyingine aliniona nikilia. Alinijia, akanikumbatia, na kuimba nami sehemu ya wimbo iliyobaki. Nilihisi nimejaa upendo kwa akina ndugu na dada na nikafurahi sana kwamba tulienda mikutanoni, nikitambua kwamba huko ndiko tunakopata msaada, huko kwenye Jumba la Ufalme.”[1] Tunapaswa kuwathamini ndugu zetu kwa kuwapa burudisho wanapolihitaji na kitia-moyo nyakati zote.—Ebr. 10:24, 25.
5 Wakati ulimwengu sasa unapokuwa wenye kulemea zaidi na zaidi, acheni tuazimie kujizoeza kujua ndugu zetu vizuri zaidi. Kubadilishana vitia-moyo vyenye kutoka moyoni kutakuwa baraka kwa wote.—Rom. 1:11, 12.
[DO NOT SET] Reference 1. w95 12/1 16 ¶8.