Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/98 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Ya Septemba

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mikutano Ya Utumishi Ya Septemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 9/98 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Ya Septemba

Juma Toka Septemba 7

Wimbo 216

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Sema juu ya ripoti ya utumishi wa kutaniko wa Agosti.

Dak. 15: “Je! Mwezi wa Septemba Utabaki Katika Historia?” Kwa maulizo na majibu. Tia moyo wahubiri wote washiriki katika huduma mnamo Septemba na kila mwezi wa mwaka mpya huu wa utumishi.

Dak. 20: “Tutumie Broshua Ili Kugusa Akili na Moyo.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Sema kifupi juu ya broshua zilizochapishwa kadiri miaka ilivyopita ili kutolea watu habari kuhusu maswali ya kibiblia ya maana. (Ona Index des publications de la Société 1986-1990, kurasa 298-302.) Kwa wakati mrefu zaidi, simulia juu ya broshua na sema ni watu gani wanaweza kupendezwa na kila moja. Panga onyesho moja au mawili.

Wimbo 191 na sala ya mwisho.

Juma Toka Septemba 14

Wimbo 127

Dak. 10: Matangazo. Hali ya akaunti. Sema juu ya mradi tulio nao: kwamba wahubiri wote washiriki katika huduma ya shambani mnamo Septemba.

Dak. 15: Mahitaji ya Kutaniko. Tafadhali, zungumzeni juu ya barua kuhusu Majumba ya Ufalme.

Dak. 20: “Vijana​—Tumieni kwa Faida Kipindi Chenu cha Kusoma Shuleni.” Kwa maulizo na majibu. Tia ndani mawazo yenye kufaa kutoka Amkeni! (ya Kifaransa) ya Aprili 8, 1992, kurasa 17-​19, na Mnara wa Mlinzi wa Julai 15, 1991, kurasa 23-6.

Wimbo 37 na sala ya mwisho.

Juma Toka Septemba 21

Wimbo 163

Dak. 10: Matangazo. Alika wahudhuriaji waeleze kwa kifupi namna ya kupata jina na anwani ya mtu tuliyemtolea ushahidi barabarani, katika shamba la wanyama, au mahali pengine ili kuendeleza kupendezwa. Toa kifupi cha “Programu ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja Lijalo.”

Dak. 35: “Tazamo Linalosonga Mbele juu ya Kazi ya Haraka ya Kufanya Wanafunzi.” Kwa maulizo na majibu. Someni mafungu 5, 10 na 11. Sema namna kazi ya mafunzo ya Biblia inavyosonga mbele katika kutaniko lenu. Tia moyo wote wanaoongoza mafunzo wasome tena nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996 ili kuwa wafundishaji bora. Chunguzeni mafungu 5 na 25 ya nyongeza hiyo.

Wimbo 108 na sala ya mwisho.

Juma Toka Septemba 28

Wimbo 65

Dak. 12: Matangazo. Kumbusha wahubiri wote watoe ripoti zao za utumishi wa Septemba. Viongozi wa funzo la kitabu watahakikisha kwamba kila mshiriki wa kikundi chao amefanya hivyo, ili kwamba ripoti zote zikusanywe kwa ajili ya Octoba 6. Simulia juu ya vichapo vya kutolea mwezi huu wa Septemba. Fanyeni onyesho fupi lenye kutokeza ulizo “Kwa nini tulitumie jina la Mungu?” Toa jibu kwa msaada wa kitabu Ujuzi, sura 3, fu. 6.

Dak. 15: “Waangalizi Wanaoongoza​—Mwangalizi-msimamizi.” titre à vérifier Hotuba yenye kutolewa na mwangalizi-msimamizi. Baada ya kueleza madaraka yake, anashukuru kutaniko kwa kushirikiana na wazee wanaolichunga kundi.

Dak. 18: Saidieni Watoto Wenu Shuleni. Mzee mmoja anasimulia na baba au mama wawili au watatu ambao watoto wao huenda shuleni. Simulia kifupi juu ya matatizo fulani ambayo watoto hukutana nayo kikawaida shuleni, kama yale yanayozungumziwa katika Amkeni! ya Agosti 8, 1994, kur. 5-7. Kisha, kwa msaada wa kur. 8-10, zungumzeni juu ya jinsi wazazi wawezavyo kulinda watoto na kuwa na uhusiano mzuri pamoja na walimu.

Wimbo 24 na sala ya mwisho.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine