Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 12/98 uku. 5-6
  • Kujikumbusha Kwa Kuandika Kwa Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kujikumbusha Kwa Kuandika Kwa Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Vichwa Vidogo
  • Jibu Kweli au Si Kweli kisha sentensi zifuatazo:
  • Jibu maulizo yafuatayo:
  • Jaza nafasi zilizo wazi katika sentensi zifuatazo:
  • Onyesha majibu ya kweli katika habari zifuatazo:
  • Patanisha habari zifuatazo na maandiko yanayolingana nazo: Mez. 8:​30; Mt. 19:13-​15; Ebr. 2:1; Yak. 4:​15; 1 Pet. 3:4
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 12/98 uku. 5-6

Kujikumbusha Kwa Kuandika Kwa Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Kujikumbusha vitabu vikiwa vyenye kufungwa kwa mambo yaliyozungumzwa kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma toka Septemba 7 mpaka lile la Desemba 21, 1998. Jibu juu ya karatasi nyingine maulizo mengi kadiri unavyoweza katika wakati uliogawiwa.

[Agizo: Wakati wa kujikumbusha, tumia tu Biblia. Mitajo inayotolewa kisha kila ulizo inatolewa ili kurahisisha utafiti wako mwenyewe. Namba za kurasa na mafungu hazionyeshwi kila mara kuhusu mitajo ya Mnara wa Mlinzi.]

Jibu Kweli au Si Kweli kisha sentensi zifuatazo:

1. Kwenye 2 Timotheo 1:6, ile “zawadi” huelekeza kwa uwezo wa kusema kwa lugha mbalimbali uliotolewa kwa Timotheo kupitia utendaji wa roho takatifu ya Mungu. [1, Usomaji wa Biblia wa kila juma; ona w85-F 5/1 uku. 16 fu. 15.]

2. Mkristo aliyekomaa ‘huzoeza nguvu zake za ufahamu ili kutofautisha lililo sahihi na lililo kosa pia’ kwa kufanya utumiaji wa ujuzi wowote alio nao juu ya Mungu uwe zoea lake. (Ebr. 5:​14) [4, Usomaji wa Biblia wa kila juma; ona w85-F 6/15 uku. 9 fu. 7.]

3. Ni wazi kwamba, ingawa Mashahidi wa Yehova wanaweza kusajiliwa (kuandikwa) na serikali kuwa shirika la kidini, idhini (ruhusa) ya kuendelea na ibada ya kweli haitokani na mwanadamu yeyote au serikali yoyote ya kibinadamu. [5, jv-SW uku. 696 fu. 1]

4. Yakobo mwandikaji wa Biblia ndiye yuleyule aliyekuwa msemaji kwa ajili ya “mitume na wazee” wakati wa uamuzi kuhusu tohara. (Mdo. 15:6, 13; Yak. 1:1) [7, si-SW uku. 248 maf. 2-3]

5. Ijapokuwa 1 Petro 5:​13 lasema kwamba Petro alikuwa Babuloni alipoandika barua yake ya kwanza, uthibitisho waonyesha kwamba jina Babuloni ni jina la kifumbo la Roma. [8, si-SW uku. 252 fu. 4]

6. Usemi “mpinga Kristo anakuja” kwenye 1 Yohana 2:​18 huelekeza kwa mtu binafsi. [10, Usomaji wa Biblia wa kila juma; ona rs-SW uku. 212 fu. 3.]

7. Mtengano uliotokea kutokana na hisia za Paulo kuelekea Marko, unaotajwa kwenye Matendo 15:36-​41, haukusuluhishwa kamwe. [11, ad uku. 970 fu. 4]

8. Kwa usahihi, kitabu cha Ufunuo kimewekwa mwishoni mwa Biblia kwa sababu kilikuwa kitabu cha mwisho kilichoandikwa na mtume Yohana. [12, si-SW uku. 263 fu. 1]

9. Bila kukosea, Ufunuo 13:11-​15 hutoa picha ya jinsi Serikali Kubwa ya Uingereza-Amerika ilivyokuja kuwa mdhamini mkuu na mpaji uhai kwa ule Ushirika wa Mataifa na mrithi wake, Umoja wa Mataifa. [16, Usomaji wa Biblia wa kila juma; ona w88-SW 12/15 uku. 19 fu. 3.]

10. Amri ya kupendana inayosimuliwa kwenye Yohana 13:34 ilikuwa “amri mpya” kwa sababu ilikuwa ya karibuni kuliko Sheria ya Musa. [15, jv-SW uku. 711 fu. 3]

Jibu maulizo yafuatayo:

11. Inamaanisha nini kwamba mwangalizi hapaswi kuwa “mpiga-watu”? (Tito 1:7) [2, Usomaji wa Biblia wa kila juma; ona w90-SW 9/1 uku. 27 fu. 21.]

12. Tunajuaje kwamba Loisi na Eunike wote wawili walimfundisha Timotheo kutoka katika Maandiko? [4, ad uku. 935 fu. 1]

13. Yesu alimaanisha nini aliposema, “Dhabihu na toleo hukutaka”? (Ebr. 10:5) [5, Usomaji wa Biblia wa kila juma; ona w96-SW 7/1 uku. 14 fu. 3.]

14. Wakristo wanawezaje ‘kuushinda ulimwengu’? (1 Yohana 5:3, 4) [10, si-SW uku. 258 fu. 12]

15. Usemi wa Petro ‘kuweka karibu akilini siku ya Yehova’ watia ndani nini? (2 Pet. 3:​12) [9, Usomaji wa Biblia wa kila juma; ona w97-SW 9/1 uku. 19 fu. 2.]

16. Usafi wa roho unatia ndani nini, na huo wawezaje kusaidia kulinda familia? (2 Kor. 7:1) [10, fy-SW uku. 46 fu. 14]

17. Kulingana na Ufunuo 1:7, wale waliomchoma Yesu watamwonaje ‘akija pamoja na mawingu’? [12, Usomaji wa Biblia wa kila juma; ona w93-SW 5/1 uku. 22 fu. 7.]

18. Wakristo wenye kulinda wanawezaje ‘kukazia uangalifu kwa wao wenyewe na kufuliza kuwa macho’? (Luka 21:34, 36) [16, jv-SW uku. 714 fu. 4]

19. Wale wanaofanyiza tengenezo moja la Kikristo la kweli leo hufikiaje uelewevu sahihi wa Neno la Mungu? [14, jv-SW uku. 708 fu. 3]

20. Ni matakwa gani ya Kimaandiko ambayo lile tengenezo moja la Kikristo la kweli linapaswa kutimiza katika siku za mwisho? [13, jv-SW uku. 706 fu. 3]

Jaza nafasi zilizo wazi katika sentensi zifuatazo:

21. Ni lazima mume na mke _________________________ kila mmoja kwa mwenzake, wakiweka akilini kwamba _________________________ ni wa maana kuliko sura ya nje. [1, fy-SW uku. 26 kisanduku cha kujikumbusha]

22. Barua ya Paulo kwa Waebrania inaonyesha kwamba zile sehemu mbalimbali za _________________________ zilikuwa kigezo kilichofanywa na Mungu kikielekezea kwenye mambo makubwa zaidi yaliyokuwa mbele, yote yakifikia upeo katika _________________________, ule utimizo wa Sheria. [6, si-SW uku. 247 fu. 23]

23. Kwenye 2 Petro 1:​5-8, mtume Petro apendekeza _________________________ ili kujenga sifa zile za kimungu ambazo hutuzuia tusiwe ama _________________________ ama _________________________. [9, si-SW uku. 255 fu. 9]

24. Waume na wake wanapowasiliana, _________________________ ni jambo la maana sana. [6, fy-SW uku. 36 fu. 21]

25. Maria mama ya Yesu alikuwa wa kabila la _________________________ na wa ukoo wa Daudi; kupitia yeye, Yesu alikuwa na haki ya _________________________ “kiti cha Ufalme cha Daudi baba yake.” (Luka 1:​32) [14, ad uku. 979 fu. 3]

Onyesha majibu ya kweli katika habari zifuatazo:

26. Wakati wa kifungo cha kwanza cha Paulo gerezani katika Rumi, (Onesiforo; Onesimo; Onani), mtumwa aliyetoroka nyumbani mwa (Philipo; Festo; Filemoni), alikuwa miongoni mwa wale waliosikiliza kuhubiri kwake. [2, si-SW uku. 242 fu. 2]

27. (Upendo; Staha; Ukaribishaji-wageni) linafasiriwa kuwa “kuwapa wengine ufikirio, kuwaheshimu.” [3, fy-SW uku. 30 fu. 7]

28. Kwenye Luka 14:28, Yesu ni mwenye kusimulia juu ya (kupanga kimbele; kutoponda fedha; kuepuka kukopa fedha). [8, fy-SW uku. 40 fu. 4]

29. “Ubwana” unaotajwa kwenye Yuda 8 laelekeza kwa (mamlaka ya Yesu; enzi kuu ya Yehova; mamlaka katika kutaniko la Kikristo yaliyotolewa na Mungu). [11, si-SW uku. 263 fu. 9]

30. Kwenye Ufunuo 11:11, zile “siku tatu na nusu,” ambazo katika hizo baki lenye kutiwa mafuta lilionekana kama maiti machoni pa maadui zalo, zaelekeza kwa (miaka mitatu na nusu; kipindi kifupi cha wakati; miezi mitatu na nusu). [15, Usomaji wa Biblia wa kila juma; ona re-SW uku. 167 fu. 21.]

Patanisha habari zifuatazo na maandiko yanayolingana nazo: Mez. 8:​30; Mt. 19:13-​15; Ebr. 2:1; Yak. 4:​15; 1 Pet. 3:4

31. Ili kukinza uvutano wa propaganda ya daima ambayo inatujia kutoka katika ulimwengu huu, tunapaswa “kukazia uangalifu zaidi kuliko ilivyo kawaida” Neno la Mungu kupitia mazoea mazuri ya kujifunza na ratiba nzuri ya usomaji wa Biblia. [3, Usomaji wa Biblia wa kila juma; ona w98-SW 1/1 uku. 7 fu. 9.]

32. Kila mara tunapofanya mipango kwa ajili ya wakati ujao, tunapaswa kufikiria katika sala jinsi inavyopatana na makusudi ya Mungu. [7, Usomaji wa Biblia wa kila juma; ona w97-SW 11/15 uku. 21 maf. 10-11.]

33. “Roho ya utulivu na ya upole” ya mke na mama Mkristo humpendeza si mume wake tu bali, jambo la maana zaidi, humpendeza Mungu. [8, Usomaji wa Biblia wa kila juma; ona w89-SW 5/15 uku. 19 fu. 12.]

34. Kwa kufuata kielelezo cha Yehova, baba mwema angepaswa kujitahidi kusitawisha uhusiano wenye shauku na wenye upendo pamoja na mtoto wake tangu tu mwanzo wa maisha ya mtoto. [13, fy-SW uku. 54 fu. 7]

35. Kwa kuwa Yesu hakuwa mwenye upendeleo katika kubariki watoto wadogo, hatupaswi kuona watoto wa kiume kuwa wa juu kuliko wale wa kike. [12, fy-SW uku. 52 fu. 4]

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine