Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/99 uku. 8
  • Fanyeni Matumizi Mazuri ya Vitabu vya Zamani

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Fanyeni Matumizi Mazuri ya Vitabu vya Zamani
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Muvitumie Kuliko Kuvirundika
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Majibu Kwa Maulizo Yenu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 1/99 uku. 8

Fanyeni Matumizi Mazuri ya Vitabu vya Zamani

1 Katika pande zote za dunia, wanadamu wameweka akibani katika maktaba mamilioni ya vitabu vya zamani. Hata hivyo, vitabu hivyo vimekuwa na faida gani yenye kudumu kwa jamii ya kibinadamu? (Mhu. 12:12) Vichapo vinavyokazia uangalifu juu ya Ufalme wa Mungu na juu ya yale ambayo utaletea ainabinadamu ni vyenye thamani zaidi sana. Makutaniko mengi yana vitabu hivyo mbalimbali vilivyotangazwa kabla ya 1985 katika stoki. Mnamo Januari tutatolea watu vitabu hivyo vya zamani.

2 Vina Thamani Halisi: Japo wengine kati yetu huenda wakaona kwamba vitabu hivyo si vya kisasa kwa kulinganisha na vichapo vyetu vipya-vipya, tunapaswa kukumbuka kwamba ukweli wa Kimaandiko unapatikana ndani yavyo. Ujumbe wa Ufalme vinavyoueleza bado ni wenye manufaa leo, na ikiwa unafuatwa, unaweza kuokoa uhai. (Yn. 17:3) Kwa hiyo, tungepaswa kufanya jitihada zaida ili kutumia vizuri vitabu hivyo vya zamani.

3 Jambo lililoonwa la mwanamke aliyerithi kutoka kwa nyanya yake hesabu fulani ya vichapo vya zamani vya Watch Tower ni lenye kutia mkazo juu ya thamani yavyo. Shahidi mmoja alimwuliza mwanamke huyo ikiwa alijua thamani ya vichapo hivyo. Mwanamke akajibu: “Kwa hakika, sijui thamani yake halisi, lakini nawezaje kupata kujua?” Mwanamke huyo alikubali funzo la Biblia, akaja katika kweli, na baadaye akaja kuthamini maktaba ya nyanya yake. Mkusanyo huo wa vitabu vya zamani ulithibitika kuwa urithi wenye thamani kama nini![1]

4 Tuvitolee Watu: Zaidi ya kupendekeza vitabu vya zamani kutoka nyumba hadi nyumba, hakikisheni kwamba mnavitolea watu mnapofanya ziara za kurudia kwa wale mnaojua kuwa wenye kufurahia kusoma vichapo vyetu, kutia ndani wale wanaofanya uandikishaji kwa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! na ambao wako katika njia yako ya ugawaji wa magazeti. Kwa wale wanaojifunza Biblia pamoja nawe, vitabu vya zamani vyenye kuchaguliwa vinaweza kutoa ujuzi wa msingi utakaopanua uelewevu wao wa kweli. Usisahau kujipatia kila kitabu cha zamani usichokuwa nacho katika mkusanyo wako binafsi. Katika njia hiyo, utakusanya maktaba ya kitheokrasi yenye thamani, inayoweza kutumiwa ili kutajirisha vipindi vyako vya funzo la binafsi.

5 Badala ya kuweka vitabu vyetu vya zamani katika stoki, acheni tuvitumie vizuri ili kuchochea watu tunaokutana nao ‘waogope Mungu na kushika amri zake.’​—Mhu. 12:13.

[DO NOT SET] References

1. w97 4/1 26

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine