Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 5/97 uku. 3
  • Majibu Kwa Maulizo Yenu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Majibu Kwa Maulizo Yenu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maktaba ya Jumba la Ufalme Inaweza Kutusaidia Namna Gani?
    Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Muvitumie Kuliko Kuvirundika
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Mpango Mpya Kuhusu Maktaba ya Jumba la Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Fanyeni Matumizi Mazuri ya Vitabu vya Zamani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 5/97 uku. 3

Majibu Kwa Maulizo Yenu

◼ Maktaba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi inapaswa kuwa na nini?

Uwingi wa kutosha wa vichapo vya kibiblia unatolewa kwa watu wa Mungu, kwa faida yao kubwa. Kwa kuwa hesabu ya kutosha ya wahubiri hawana vichapo vyote hivyo, maktaba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, kwenye Jumba la Ufalme, inawawezesha kufanya utafiti katika vichapo ambavyo hawangeweza labda kuchunguza kwa namna nyingine. Pia maktaba hiyo ingepaswa kutoshelezwa vizuri: tafsiri mbalimbali za Biblia, vitabu vya mwisho-mwisho vya Sosaiti, mkusanyo wa Huduma Yetu ya Ufalme na mabuku ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, na pia Fahirisi za vitabu (Index des publications). Kamusi nzuri ya kisasa inaweza pia kulindwa katika maktaba. Encyclopedia mbalimbali, vitabu vya ramani au vitabu vya mitajo juu ya sarufi au historia vinaweza kuwa vyenye manufaa. Hata hivyo, mradi wetu wa kwanza ungepaswa kuwa ni kuwa na vitabu vinavyotolewa na “mtumwa mwaminifu na mwenye akili.”​—Mt. 24:45.

Inaonekana mara nyingi kwamba vitabu vilivyo na mambo yanayobishiwa viwekwe katika maktaba ya vitabu vya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Haingefaa kuweka ndani vitabu vya mahaba, vitabu vya maelezo yanayoichamba Biblia, na vitabu vya falsafa au vinavyoeleza uchawi. Maktaba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ingepaswa kuwa tu na vitabu vitakavyowasaidia wale wanaovichunguza kuendelea kufanya maendeleo kwa upande wa kiroho.​—1 Tim. 4:15.

Ni mwangalizi wa shule ndiye msimamizi wa maktaba, hata ikiwa ndugu mwingine anaweza kuchaguliwa ili kumsaidia kutumikia daraka hilo. Angepaswa kuangalia ili kwamba maktaba iwe na vichapo vyote, vitabu vipya vikiongezwa mara tu vinapopatikana. Jina la kutaniko lililo lenye maktaba lingepaswa kuandikwa waziwazi katika kurasa za kwanza kwanza za kila kitabu. Miaka yote, vitabu vitachunguzwa ili kuona ikiwa inafaa kutengeneza vimoja kati yavyo au kuvibadili.

Kila mmoja anaweza kushiriki katika kutunza maktaba. Tungepaswa kuwa wangalifu wakati tunapotumikisha vitabu. Hatungepaswa kuruhusu watoto kucheza navyo na hatungepaswa kamwe kuandika jambo lolote juu yavyo. Taarifa iliyo wazi itawekwa iwezekanavyo juu ya maktaba ili kukumbusha kwamba vitabu havipaswi kutoka nje ya Jumba la Ufalme.

Kwa kuwa makutaniko mapya yanaundwa mara kwa mara, inawezekana kwamba maktaba nyingi hazina vitabu vyote. Wahubiri wamoja walio na vitabu vya zamani wangeweza kupanga kuvitolea kutaniko. Wazee wataamua labda kuomba uchapaji upya wa mabuku ya Mnara wa Mlinzi. Hivyo, maktaba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi itaonekana kuwa ya muhimu sana, ikiwezesha kila mmoja kuvumbua hazina zenye kufichwa za Neno la Mungu linalotoa ujuzi, hekima na akili.—Mez. 2:4-6.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine