Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/03 uku. 5
  • Mpango Mpya Kuhusu Maktaba ya Jumba la Ufalme

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mpango Mpya Kuhusu Maktaba ya Jumba la Ufalme
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maktaba ya Jumba la Ufalme Inaweza Kutusaidia Namna Gani?
    Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Majibu Kwa Maulizo Yenu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Muvitumie Kuliko Kuvirundika
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Fasi Yetu ya Ibada
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 2/03 uku. 5

Mpango Mpya Kuhusu Maktaba ya Jumba la Ufalme

Kwa miaka mingi sasa, makutaniko ulimwenguni pote yamefaidika kwa kutumia maktaba ya Jumba la Ufalme layo, iliyoitwa hapo mbele maktaba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Wakati uliopita, lilionwa kuwa jambo la lazima kwamba kila kutaniko liwe na maktaba yalo. Hata hivyo, kwa kuwa Majumba ya Ufalme mengi sasa yanatumiwa na zaidi ya kutaniko moja, mengine ya makutaniko hayo yakiwa ya lugha ya kigeni, linaonekana kuwa jambo bora zaidi kuwa na maktaba yenye vifaa vya kutosha na yenye kuongezewa vichapo vya kisasa kwa ajili ya kila kikundi cha lugha katika kila Jumba la Ufalme. Katika Majumba ya Ufalme yaliyo na zaidi ya sehemu moja wanapokaa wasikilizaji, kila sehemu inapaswa kuwa na maktaba kwa ajili ya kila kikundi cha lugha kinachofanyia mikutano hapo.

Inatazamiwa kwamba mpango huo utasaidia kulinda nafasi na kupunguza gharama. Zaidi ya hayo, yaelekea kwamba kuchanga maktaba za makutaniko mawili au zaidi kutatokeza maktaba bora zaidi. Maktaba zinapotiwa pamoja, nakala mbili-mbili za vitabu zinaweza kuwekwa akiba na kutumiwa baadaye Majumba ya Ufalme mapya yanapojengwa. Ikiwa Jumba la Ufalme lina kompyuta iliyo na vichapo vya Watchtower kwenye CD-ROM, wengine wanaweza kuona chombo hicho kuwa chenye mafaa sana.

Kuhusu kila maktaba ya Jumba la Ufalme, ndugu moja, hasa mmoja wa waangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, atatumika kuwa msimamizi wa maktaba. Anapaswa kuongeza hatua kwa hatua vichapo vinavyofaa kwenye maktaba, akitia alama sahihi kwenye kifuniko cha ndani cha kila kichapo ili kuonyesha kwamba ni cha maktaba ya Jumba la Ufalme. Angalau mara moja kwa mwaka, anapaswa kufanya uchunguzi wa maktaba ili kuona ikiwa hakuna kichapo kinachokosekana katika maktaba na kuhakikisha kwamba vichapo viko katika hali nzuri. Vichapo vya maktaba hizo havipaswi kupelekwa nje ya Jumba la Ufalme.

Maktaba ya Jumba la Ufalme inaendelea kuthaminiwa sana na wale wote wanaoshirikiana na kutaniko. Na tuonyeshe kwamba sisi binafsi tunathamini uandalizi huo kwa kuutunza na kuutumia ili kutafuta “maarifa kwa Mungu.”—Mez. 2:5.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine