Muumba Wetu Mtukufu Anatujali!
1 Katika jitihada yake ya kufikiri na Israeli lililokosa utii, Yehova aliuliza: “Je! wewe hukujua? hukusikia? Yeye [ni] Mungu wa milele, BWANA, Muumba [wa] miisho ya dunia.” (Isa. 40:28, UV) Tunamjua Muumba wetu Mtukufu, na tunaona jinsi anavyotujali kwa upendo. Hata hivyo, mamilioni ya watu hushakia kuwako kwake au huwa na wazo lisilopatana na yale yanayopatikana katika Biblia juu yake. Tunawezaje kuwasaidia?
2 Kitabu kipya Je! Kuna Muumba Anayekujali? kimeandikwa ili kusaidia watu hao. Kinavuta watu wenye akili nzuri wafikiri juu ya mambo ya hakika. Habari yenye kuvuta sana na maneno yenye kusadikisha yaliyo katika kitabu hicho vingepaswa kupendeza sana wale wanaokisoma.
3 Jua Vizuri Kitabu Muumba: Chunga akilini mawazo makuu ya msingi ya mambo yaliyomo. Sura 2 hadi 5 zinachunguza jinsi ulimwengu, uhai, na mwanadamu vilipata kuwako na yule aliye chanzo chavyo(W 1cause 1c)] . Sura 6 hadi 9 zinachunguza Biblia na Mtungaji wake; zinachunguza hasa ikiwa habari ya Mwanzo kuhusu uumbaji ni yenye kutegemeka. Sura 10 inatoa jibu lenye kutosheleza la moja ya maulizo yenye kutatanisha zaidi ambayo mwanadamu huuliza: “Ikiwa Muumba anajali, mbona wanadamu wanateseka sana?”
4 Jaribu Kufikiri na Wale Wanaoshakia: Kurasa 78-9 katika kitabu Muumba huonyesha hoja [Meaning: an argument (W argument 3b)] unayoweza kutumia ili usaidie wengine wafikie mkataa sahihi kuhusu Mungu. Waulize: “Je! ulimwengu ulikuwa na mwanzo?” Wengi watakubali kwamba ulikuwa nao. Ikiwa ni hivyo, uliza: “Je! mwanzo huo ulitokea bila kusababishwa au ulisababishwa?” Wengi hukubali kwamba ulisababishwa. Jambo hilo huongoza kwenye ulizo la mwisho: “Je! mwanzo wa ulimwengu ulisababishwa na kitu fulani cha milele au na mtu fulani wa milele?” Utangulizi huo waweza kuongoza wengi waone kwamba ni lazima kuweko Muumba.
5 Kitabu Muumba ndicho kitu watu wanachohitaji. Pendekeza kitabu hicho kwa washiriki wa familia yako, wafanyakazi wenzako, wanafunzi wenzako, na watu wengine unaowajua. Kichukue katika huduma kusudi ukiachie wale unaokutana nao ambao wanashakia kuwako kwa Mungu. Kadiri tunavyojua vizuri zaidi kitabu hicho, ndivyo upendo wetu kwa Muumba wetu huwa wenye nguvu zaidi, ukituchochea tuendelee kutembea kupatana na viwango vyake vya juu sana [W lofty 1a].—Efe. 5:1; Ufu. 4:11.