Je! Twaweza Kutolea Watu Kitabu Muumba?
Mwaka uliopita, tulifurahi sote kupokea kitabu Je! Kuna Muumba Anayekujali? Hicho ni kitabu kilichoandikwa kipekee ili kusaidia wale ambao, ingawa ni wenye elimu sana katika mambo ya kimwili, huenda hawaamini kuwako kwa Mungu. Kitabu hicho chatimiza uhitaji wenye kuongezeka siku baada ya siku.
Kwa sababu zenye kufaa, toleo la mwezi la vichapo huonyesha kwa kawaida vichapo vyenye kupendeza watu wengi zaidi. Je! jambo hilo lamaanisha kwamba tungepaswa kujizuiza kutolea watu kitabu Muumba? Hata kidogo! Kitabu hicho chaweza kupendekezwa wakati wowote mwakani kwa watu wasioamini kuwako kwa Mungu na ambao wanaweza kufaidika nacho. Hicho chaweza pia kutolewa kwa watu ambao huamini kuwako kwa Mungu lakini hawana wazo halisi kuhusu yeye ni nani au kuhusu sifa zake na makusudi yake. Kwa hiyo, unatiwa moyo kuchukua nakala katika mfuko wako wa mahubiri na kuwa tayari kuitolea mtu yeyote unayefikiri kwamba atapendezwa kuisoma.