Namna ya Kuwasaidia Watu Ambao Hawako Tayari Kujifunza Kitabu Biblia Inafundisha
1. Ni kila mutu atapendezwa kwa mara ya kwanza na kitabu Biblia Inafundisha? Eleza.
1 Ili mutu fulani akuwe Shahidi wa Yehova, anapaswa kujifunza mambo ambayo Biblia inafundisha. Lakini, watu fulani ni wa dini zisizo za Kikristo na hawaone kama Biblia ni Neno la Mungu. Wengine hawaamini kama Mungu iko na wanazarau Biblia. Ni vichapo gani vimesaidia watu ambao kwa mara ya kwanza hawakuwa tayari kujifunza kitabu Biblia Inafundisha? Wahubiri wa inchi karibu 20 wametoa mashauri yanayopatikana hapa chini.
2. Ikiwa mutu fulani anatuambia haamini kama Mungu iko, tunapaswa kwanza kujua nini, na sababu gani?
2 Watu Ambao Hawaamini Kama Mungu Iko: Ikiwa mutu anatuambia haamini kama Mungu iko, ni lazima kujua kwanza sababu gani anasema hivyo. Je, ni kwa sababu anaamini fundisho la mageuzi? Ao ni kwa sababu anaona watu wanaonea wengine ao ni kwa sababu ya unafiki wa watu wa dini? Ao mutu huyo anatoka katika inchi ambayo inakataza mambo ya Mungu? Pengine hakatae kabisa kama Mungu iko, lakini haone sababu ya kuamini kama Mungu iko. Wahubiri wengi wanaona ni vizuri kuuliza ulizo kama vile, “tangu wakati gani unaamini hivyo?” Kuuliza hivyo kunaweza kumuchochea mutu ajieleze. Kisha wanamusikiliza bila kumukatiza. Wakati tunajua sababu gani mutu huyo haamini kama Mungu iko, tutajua namna ya kumujibu na tutajua ni kichapo gani tunaweza kumutolea.—Met. 18:13.
3. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaheshimu mutu na mambo ambayo anaamini?
3 Wakati wa kumujibu, tuwe waangalifu ili mutu huyo asijisikie kuwa hatuheshimu mawazo yake. Muhubiri mumoja wa États-Unis anatoa shauri hili: “Ni lazima sana kuheshimu uhuru wa watu wa kuchagua mambo wataamini. Kuliko kutafuta kubishana, ni vizuri kuuliza maulizo ambayo yatawafanya watu wafikiri na wajiamulie wenyewe.” Mwangalizi mumoja wa wilaya alisema hivi: Kisha kumuachia mwenye-nyumba nafasi ya kujieleza, ninamuuliza hivi mbele ya kumujibu: “Je, umekwisha kufikiria wazo hili?”
4. Namna gani tunaweza kuwasaidia watu wa dini ya Buddha?
4 Watu wengi wa dini ya Buddha, tangu kuzaliwa, hawana wazo kama Mungu iko. Wahubiri fulani wa Uingereza wanafurahia kutumia broshua La paix et le bonheur durables : comment les trouver wakati wanahubiria watu kama hao. Kisha kuchunguza maneno ya utangulizi, wanazungumuzia sehemu yenye kichwa « Existe-t-il vraiment un Créateur Très-Haut ? » kisha wanazungumuzia sehemu yenye kichwa « Un guide bénéfique pour tous les humains. » Kisha, wanaweza kumutolea kitabu Biblia Inafundisha na wanamuambia mwenye-nyumba hivi: “Hata kama hauamini kwamba Mungu iko, kujifunza Biblia ni kwa lazima kwa sababu inatoa muongozo muzuri sana.” Ndugu mumoja painia huko États-Unis anahubiri katika eneo la watu ambao wanazungumuza luga ya Kichina. Ndugu huyo anasema hivi: “Katika eneo letu watu wengi wanafurahia kusoma. Kwa hiyo, wakati tunawaachia kichapo, wanamaliza kukisoma chote mbele tuwatembelee tena. Lakini hawaone maana ya kujifunza Biblia. Ndiyo maana ninafurahia kuwatolea watu broshua Habari Njema wakati ninawatembelea kwa mara ya kwanza kwa sababu imeandikwa kwa njia yenye kuchochea mazungumuzo.” Mwangalizi mumoja wa muzunguko wa États-Unis mwenye kutumikia katika eneo linalozungumuza luga ya Kichina anasema kama inawezekana kumuachia mutu kitabu Biblia Inafundisha wakati unamutembelea kwa mara ya kwanza. Lakini, inaweza kuwa vizuri kuanza kujifunza sura ya 2, inayozungumuzia Biblia, kuliko kujifunza sura ya 1, inayozungumuzia Mungu.
5. Sababu gani ni lazima kuwa muvumilivu?
5 Inaomba muda murefu ili kusaidia mutu fulani aamini kama Mungu iko; kwa hiyo, ni lazima kuwa muvumilivu. Inawezekana mazungumuzo yetu ya kwanza hayatatosha kumusaidia mutu akubali kama kuna Muumbaji. Lakini, pengine kisha muda fulani atatambua kama inawezekana Mungu iko ao anaweza kusema kama anaelewa sababu gani watu fulani wanaamini hivyo.
6. Sababu gani watu fulani hawapendezwe na Biblia?
6 Watu Ambao Hawapendezwe na Biblia ao Hawaiamini: Mara mingi, inawezekana mutu akubali kama Mungu iko, lakini anakosa kupendezwa na mambo ambayo Biblia inafundisha, kwa sababu haamini kama Biblia ni Neno la Mungu. Pengine anaishi katika inchi ambamo Wakristo hawajulikane sana na anaona kama Biblia ni kitabu cha Wakristo. Ao inawezekana anaishi katika inchi ambazo zinajiita kuwa za Kikristo lakini watu hawafuate kabisa mafundisho ya Biblia. Hilo linamufanya awaze kama Biblia haiwezi kumusaidia. Namna gani tunaweza kusaidia watu kama hao wapendezwe na Biblia na waitike kujifunza kitabu Biblia Inafundisha?
7. Tunaweza kufanya nini ili kuchochea watu wapendezwe na Biblia?
7 Biro ya tawi ya Grèce iliandika hivi: “Njia muzuri ya kuwasaidia watu ambao hawapendezwe na Biblia ni kuwafungulia Biblia mara moja na kuwaonyesha mambo Biblia inasema. Wahubiri wengi wametambua kama ujumbe wa Biblia una nguvu sana ya kuchochea moyo wa mutu kuliko hata maneno ambayo wanaweza kusema. (Ebr. 4:12) Wakati watu wengi wanaona jina la Mungu katika Biblia, wanakuwa na hamu ya kujifunza Biblia zaidi.” Biro ya tawi ya India iliandika hivi: “Wahindu wengi wanapenda kabisa kujua kweli juu ya uzima na kifo. Pia wanapendezwa sana na ahadi ya Biblia inayosema kama katika dunia mupya watu hawatabaguana.” Mara nyingi wahubiri wanazungumuza na watu matatizo yanayohangaisha watu katika eneo, jambo hilo linawapatia nafasi ya kuonyesha katika Biblia mambo ambayo Ufalme wa Mungu utafanya ili kumaliza matatizo hayo.
8. Tunaweza kuwaambia nini watu ambao hawapendezwe na Biblia kwa sababu ya mwenendo wa Wakristo wa uongo?
8 Ikiwa watu fulani hawapendezwe na Biblia kwa sababu ya mwenendo wa Wakristo wa uongo, ni vizuri kuwajulisha kama Wakristo hao hawaishi kulingana na mafundisho ya Biblia. Biro ya tawi ya India iliandika tena hivi: “Wakati fulani, ni lazima tusaidie watu watambue kama makanisa hayafuate mambo Biblia inafundisha.” Wahubiri wa India walisema kama mara nyingi Wahindu wanafurahia sana sehemu ya 4 ya broshua Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, sehemu ambayo inaeleza namna makanisa yamejaribu kuliharibu Neno la Mungu. Ndugu mumoja painia katika Brezil anazoea kuuliza watu hivi: “Sababu gani usijifunze zaidi mambo ambayo Biblia inafundisha? Watu wengi wanafanya hivyo bila kupendelea dini yao. Ukifanya hivyo, wewe pia unaweza kushangazwa na mambo utakayojifunza.”
9. Sababu gani hatupaswe kuvunjika moyo wakati mutu fulani ambaye tunatembelea kwa mara ya kwanza hapendezwe na Biblia?
9 Yehova anachunguza moyo wa kila mutu. (1 Sam. 16:7; Met. 21:2) Wale walio na moyo muzuri anawavuta na kuwafanya wakuwe Wakristo wa kweli. (Yoh 6:44) Kuna watu wengi kama hao ambao hawajafundishwa Neno la Mungu ao wanajua tu mambo madogo sana juu ya Biblia. Kwa kuwahubiri, tunawapatia nafasi ya kuokolewa na kujua kabisa kweli. (1 Tim. 2:4) Kwa hiyo, ikiwa kwa mara ya kwanza tunawatembelea watu, na hawapendezwe na mambo Biblia inafundisha, tusivunjike moyo! Tumia kichapo kimoja kati ya vichapo vya luga yako ili kuwafanya wapendezwe na Biblia. Kisha unaweza sasa kuanza kujifunza naye kitabu tunachotumia leo ili kujifunza na watu Biblia, ni kusema, Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
[Box on page 4]
Ikiwa mutu anasema Mungu haiko, unaweza kumuuliza hivi:
• “Unaamini hivyo tangu wakati gani?” Hilo litakusaidia kujua sababu.
• Ikiwa ni wa dini ya Buddha, tumia broshua La paix et le bonheur durables : comment les trouver, ukurasa wa 9-12.
• Ikiwa anaamini fundisho la mageuzi, unaweza kutumia vichapo hivi:
Amuka!, kwenye habari zenye kichwa “Kitu Hiki Kilijifanya Chenyewe?”
Video Maajabu ya Uumbaji Yanafunua Utukufu wa Mungu
Broshua Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, sehemu ya 4; Uhai—Ulitokana na Muumba?; na Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai
• Ikiwa mutu anasema Mungu haiko kwa sababu anaona watu wanaonea wengine ao kwa sababu ya mateso, unaweza kutumia vichapo hivi:
Kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali?, sura ya 10
Broshua Je, Kweli Mungu Anatujali?, sehemu ya 6; na Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?, sehemu ya 6
• Ikiwa musikilizaji wako anaanza kukubali wazo la kwamba Mungu iko, munaweza kuanza kujifunza naye mara moja kitabu Biblia Inafundisha. Inaweza kuwa muzuri kuanza na sura ya 2 ao sura ingine yenye kumufurahisha.
[Box on page 5]
Ikiwa mutu haamini Biblia:
• Muchunguze naye sura ya 17 na ya 18 ya kitabu La vie : comment est-elle apparue ? Évolution ou création ?
• Kwa Wahindu, tumia broshua Pourquoi adorer Dieu en amour et en vérité ?
• Kwa Wayahudi, tumia broshua Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, ukurasa wa 3-11.
• Zungumuzia faida za kufuata kanuni za Biblia. Ili kumusaidia aone faida hizo, unaweza kutumia vichapo hivi:
Habari zenye kichwa “Musaada kwa Familia” zilizo katika Amuka!
Video La Bible : une force dans votre vie
Broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu!, somo la 9 na la 11; Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, ukurasa wa 22-26; na AJinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, sehemu ya 2
Kwa watu wa dini ya Buddha, tumia broshua La voie qui mène à la paix et au bonheur, ukurasa wa 3-7.
Kwa Waislamu, tumia broshua Imani ya Kweli siri ya kuwa na maisha yenye furaha, sehemu ya 3.
Ikiwa unahubiri katika eneo ambamo watu wana mawazo mabaya juu ya Biblia, ni vizuri uepuke kutaja Biblia, unaweza kutaja Biblia ukisha kuwatembelea mara nyingi.
• Ili kumufasiria namna unabii mbalimbali wa Biblia unatimizwa, tumia vichapo hivi:
Video La Bible : un récit historique exact, des prophéties dignes de foi
Broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, ukurasa wa 27-29
• Ikiwa mutu anataka kujua mambo Biblia inafundisha juu ya habari fulani, ni vizuri kuanza mazungumuzo bila kukawia katika kitabu Biblia Inafundisha.
[Box on page 6]
Ikiwa mutu anasema: “Mimi siamini kama Mungu iko,” unaweza kusema:
• “Ninaweza kukuelezea kwa kifupi mambo yaliyonisaidia niamini kama Muumbaji iko?” Kisha, zungumuzia habari zilizo katika kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 390-392, ao fanya mipango ili kumuletea kichapo kilichokusaidia.
• “Lakini, ikiwa Mungu iko, ungependa akuwe mutu wa namna gani?” Watu wengi wanajibu kwa kusema kama wangependa kumukaribia Mungu mwenye upendo, mwenye haki, na mwenye rehema, Mungu mwenye hana ubaguzi. Umuonyeshe katika Biblia sifa hizo za Mungu. (Inawezekana hata kutumia sura ya 1 ya kitabu Biblia Inafundisha, kuanzia fungu la 6.)
Ikiwa mutu anasema: “Mimi siamini Biblia,” unaweza kumuambia:
• “Watu wengi hawaamini Biblia. Watu fulani wanawaza kama Biblia inapinga sayansi ao kama haiwezekane kutumikisha mashauri ya Biblia. Kisha umuulize hivi: umekwisha kusoma sehemu fulani za Biblia? [Acha mutu ajibu. Kisha umuonyeshe maneno ya utangulizi kwenye ukurasa wa 3 wa broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, na umuachie broshua hiyo.] Watu wengi hawaamini Biblia kwa sababu watu wa dini hawaishi kulingana na mafundisho ya Biblia. Wakati nitakutembelea tena, nitapenda tuzungumuzie mufano wenye kupatikana kwenye ukurasa wa 4 na wa 5.”
• “Watu wengi wana mawazo kama yako. Ninaweza kukuonyesha mambo fulani yenye kushangaza juu ya Biblia? [Soma Ayubu 26:7 ao Isaya 40:22. Maandiko hayo yanaonyesha kama wakati Biblia inazungumuzia mambo ya sayansi inasema kweli.] Tena Biblia ina mashauri mazuri yanayoweza kusaidia familia. Siku ingine nitakuonyesha mufano fulani.”
• “Aksanti kwa kuniambia mawazo yako. Ikiwa Mungu angewaandikia wanadamu kitabu, unawaza angewaandikia mambo gani?” Kisha umuonyeshe katika Biblia mambo fulani yanayopatana na jibu lake.