Mwadhimisho wa Ulimwenguni Pote wa Kifo cha Kristo
1 Yehova ametupatia zawadi nyingi. Jumla [W sum total 2]ya wema wake na fadhili-upendo wake inaelezwa wazi [vividly]kuwa “zawadi yake ya bure isiyoelezeka.” Ndiyo, “fadhili isiyostahiliwa ya Mungu” ni ya ajabu sana hivi kwamba inapita uwezo wetu wa kueleza.—2 Kor. 9:14, 15.[1]
2 Zawadi Kubwa Zaidi: Yesu Kristo, Mkombozi wa binadamu, ndiyo zawadi kubwa kuliko zote. Katika kuonyesha upendo wake mkubwa kwa ulimwengu wa binadamu, Yehova alitoa Mwana wake mpendwa na mzaliwa-pekee. (Yn. 3:16) Baraka isiyostahiliwa kama hiyo yastahili mwadhimisho wa ulimwenguni pote! Wakati gani na jinsi gani? Jioni ya Aprili 1, 1999, Wakristo ulimwenguni pote wataadhimisha Mlo wa Jioni wa Bwana, huku wakiadhimisha Ukumbusho wa dhabihu hiyo kubwa kuliko zote.—1 Kor. 11:20, 23-26.
3 Kristo alikufa kwa ajili yetu hata “tulipokuwa tungali watenda-dhambi,” nasi twaweza kuonyesha shukrani yetu binafsi kwa kuadhimisha Ukumbusho wa kifo chake na kwa kualika wengine wawe pamoja nasi kwenye tukio hilo la maana sana.—Rom. 5:8.
4 Tukio la Maana Zaidi: Kwanza, mwadhimisho wa kifo cha Kristo wakazia jambo la kwamba yeye alitegemeza kikamili enzi kuu ya Mungu. Unatukumbusha pia kwamba tunaweza kufurahia msimamo safi mbele ya Yehova kwa kudhihirisha imani katika dhabihu ya Yesu, na hivyo kuwa na hakika ya wokovu. (Mdo. 4:12) Kwa kweli, hilo ndilo tukio la maana zaidi mwakani!
5 Tunaonyesha upendo kwa majirani zetu kwa kuwaalika waadhimishe Mlo wa Jioni wa Bwana pamoja nasi. Bado faida za fidia zapatikana kwa mamilioni wanaojifunza thamani yake yenye kuzidi. (Flp. 3:8) Wale wanaodhihirisha imani katika dhabihu ya Kristo wanaweza kupata tumaini thabiti la uhai udumuo milele.—Yn. 17:3.
6 Majira ya Ukumbusho yanatutolea nafasi za pekee za kuonyesha uthamini kuelekea fadhili isiyostahiliwa ya Mungu inayozidi. Huo ni wakati bora wa kushiriki kwa bidii katika kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu. Faida kubwa zinangojea wale wote wanaofikiri kwa njia ya sala juu ya zawadi ya bure ya Yehova isiyoelezeka na wanaofanya mipango ili waweko kwenye mwadhimisho wa Mlo wa Jioni wa Bwana utakaofanyika mwaka huu!
[DO NOT SET] References
1. w93 12/1 28