Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/04 uku. 1
  • “Washikamanifu Wote, Mpendeni Yehova”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Washikamanifu Wote, Mpendeni Yehova”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Endeleeni Kufanya Hivi kwa Kunikumbuka Mimi” Kifo cha Yesu Kitaazimishwa Tarehe 2 mwezi wa 4
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Saidia Wengine Wafaidike na Fidia Ukumbusho wa Kifo cha Kristo Utaadhimishwa Mnamo Aprili 12
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Yehova Anabariki Bidii Yetu ya Kuhuzuria Ukumbusho
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • ‘Muendelee Kufanya Hivi’ Tutafanya Ukumbusho Tarehe 5 Mwezi wa 4
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 3/04 uku. 1

“Washikamanifu Wote, Mpendeni Yehova”

Kifo cha Yesu Kitaadhimishwa Aprili 4

1 Miaka iliyopita, wakati Ukrainia ilipokuwa chini ya utawala wa Kikomunisti, wenye mamlaka walichunguza kwa kuvizia akina ndugu—hasa wakati ambapo siku ya Chakula cha Jioni cha Bwana ilipokaribia—kwa kuwa walitumaini kugundua mahali ambapo mkutano ulipangwa kufanyika. Kwa kawaida, hilo lilikuwa tatizo kwa kuwa wenye mamlaka walijua karibu tarehe ya mwadhimisho huo. Akina ndugu wangefanya nini? Nyumba ya dada mmoja ilikuwa na chumba cha chini ya ardhi ambacho kilikuwa kimejaa maji. Kwa kuwa wenye mamlaka hawangetazamia kikundi cha watu kukusanyika katika chumba chenye kujaa maji, akina ndugu walijenga jukwaa lililoinuka juu ya maji yenye kufika kwenye magoti. Ingawa walipaswa kukaa wenye kuchutama juu ya jukwaa hilo lililokaribiana na dari, kutaniko liliadhimisha Ukumbusho kwa furaha bila kusumbuliwa na mtu yeyote.

2 Azimio la ndugu zetu Waukrainia la kutii amri ya kukumbuka kifo cha Yesu lilikuwa wonyesho wa kustaajabisha wa upendo wao kwa Mungu. (Luka 22:19; 1 Yo. 5:3) Wakati wowote ule tunapopambana na vizuizi katika maisha yetu, mifano kama hiyo inaweza kututia moyo na kutufanya kuwa na azimio la kuwapo ili kuadhimisha Chakula cha Jioni cha Bwana mnamo Aprili 4. Kwa kufanya hivyo, tunaonyesha kwamba tunashiriki maoni ya mtunga-zaburi aliyeimba: “Enyi washikamanifu wake wote, mpendeni Yehova.”—Zab. 31:23.

3 Tusaidie Wengine Wakue Katika Upendo kwa Mungu: Upendo kwa Mungu pia unatuchochea kualika wengine ili kuadhimisha kifo cha Yesu pamoja nasi. Nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari ilitia moyo kila mmoja wetu kufanya orodha ya wale ambao tunapanga kualika kwenye Ukumbusho. Je, wewe unajitahidi kuendelea kualika kila mtu anayepatikana kwenye orodha yako? Chukua wakati ili kuwafafanulia maana ya tukio hilo. Kuwakumbusha kwa urafiki, siku na wakati Ukumbusho utakapofanywa na, ikiwa ni lazima, kuwasindikiza kunaweza kuwatia moyo wahudhurie.

4 Kwenye mahali pa Ukumbusho, fanya jitihada ya pekee ili kukaribisha wale ambao wamekubali mwaliko wetu, na ufanye wajisikie wenye kukaribishwa. Unawezaje kuwasaidia wakue katika upendo wao kwa Yehova? Uwe tayari kujibu maulizo yao. Uwe tayari kupendekeza funzo la Biblia ikiwa hali ni zenye kufaa. Waalike kuhudhuria mikutano yetu ya kutaniko ya kila juma. Hasa wazee watatoa uangalifu kwa Wakristo wasiotenda wanaohudhuria. Wanaweza kupanga kutembelea watu hao wasiotenda na kuwatia moyo warudilie tena utendaji wao pamoja na kutaniko, labda kwa kuwatolea maelezo zaidi yanayotegemea hotuba hiyo ya Ukumbusho.—Rom. 5:6-8.

5 Tuongeze kwa Kina Kirefu Upendo Wetu kwa Yehova: Kufikiri kwa uzito juu ya zawadi ya fidia kunaweza kuongeza kwa kina kirefu upendo wetu kwa Yehova na Mwana wake. (2 Ko. 5:14, 15) Shahidi mmoja aliyehudhuria Ukumbusho kwa miaka mingi alisema yafuatayo: “Tunatazamia Ukumbusho kwa hamu. Kila mwaka tunauona kuwa wa pekee zaidi. Nakumbuka miaka 20 iliyopita nikisimama katika nyumba ya kushughulikia mazishi, nikimtazama baba yangu mpendwa na kuhisi uthamini wa kweli wenye kutoka moyoni kwa ajili ya ile fidia. Hapo mwanzoni fundisho la fidia lilikuwa maarifa ya kichwani tu. Eh, ni kweli nilijua maandiko yote kuhusu fidia na jinsi ya kuyaeleza! Lakini ni wakati tu nilipohisi jinsi mtu anavyofadhaishwa na kifo ndipo moyo wangu uliporuka kwa shangwe juu ya yale yatakayotimizwa kwa ajili yetu kupitia fidia hiyo yenye thamani.”—Yoh. 5:28, 29.

6 Kwa kuwa tarehe ya Ukumbusho wa mwaka huu inakaribia, chukua wakati wa kutayarisha moyo wako kwa ajili ya tukio hilo. (2 Nya. 19:3) Tafakari juu ya usomaji wa Biblia kwa ajili ya Ukumbusho, ambao unaonyeshwa katika kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2004 na Kalenda 2004. Wengine wanafurahia kurudilia, wakati wa funzo la familia, sura 112-116 katika kitabu Mtu Mkuu Zaidi. Wengine pia wanafanya utafiti zaidi kwa kutumia vichapo vinavyosaidia kwa ajili ya funzo, vinavyoandaliwa kupitia jamii ya mtumwa mwaminifu na mwenye busara. (Mt. 24:45-47) Sisi sote tunaweza kutia zawadi ya fidia katika sala zetu zenye kutoka moyoni. (Zab. 50:14, 23) Kwa kweli, wakati huo wa Ukumbusho, tuendelee kufikiri juu ya upendo wa Yehova kwetu na kutafuta njia mbalimbali za kuonyesha upendo wetu kwake.—Marko 12:30; 1 Yo. 4:10.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine