Mikutano ya utumishi ya Oktoba
Juma toka Oktoba 4
Wimbo 147
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 17: “Neno la Mungu la Kiunabii Lote Litatimizwa!” Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, na uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu. Vuta uangalifu juu ya mambo fulani madogo-madogo kutoka katika kile kitabu kipya ambacho kinaonyesha maana ya nyakati zetu.
Dak. 18: Iweni Wenye Kuhangaikia Magazeti! Sema hesabu ya jumla ya magazeti ambayo kutaniko liliachia watu mwezi uliopita. Hiyo inalinganaje na hesabu iliyopokewa kutoka kwa Sosaiti? Ikiwa kuna tofauti kubwa, ni jambo gani linapasa kufanywa? Alika wasikilizaji watoe maelezo juu ya mambo yafuatayo: (1) Kila mhubiri angepaswa kuagiza kiasi chenye kutosha lakini chenye kufaa. (2) Oneni kila Siku ya Posho kuwa Siku ya Magazeti. (3) Pangeni programu yenu binafsi ya utumishi ili kutia ndani utendaji fulani wa kugawa magazeti kila mwezi. (4) Pangeni kutoa ushahidi wa vivi hivi mwingi zaidi huku mkitumia magazeti ili kuanzisha mazungumzo. (5) Pelekeni makala ya pekee kwa wafanya-biashara na watu wanaofanya kazi ya ufundi, ambao wanaelekea zaidi kupendezwa nayo. (6) Dumisheni maandishi sahihi kuhusu magazeti mliyoachia watu, na msitawishe njia ya kugawa magazeti, mkirudia kikawaida na magazeti ya karibuni zaidi. (7) Fanyeni matumizi mazuri ya magazeti yoyote ya zamani ili yasirundikwe. Onyesha magazeti ya karibuni, na uonyeshe makala ambayo yanaelekea kuamsha kupendezwa. Omba mtu mwenye umri mkubwa na kijana mmoja wafanye kila mmoja onyesho la utoaji mfupi wa magazeti.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 1999, ukurasa 7.
Wimbo 105 na sala ya kumalizia.
Juma toka Oktoba 11
Wimbo 194
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti.
Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 20: “Jinsi ya Kupata Furaha Nyingi Zaidi Kutokana na Mikutano.” Maulizo na majibu. Taja mifano halisi kuhusu jinsi tunavyoweza kuonyesha ufikirio na kuwa wenye kutiana moyo kwenye mikutano. Alika wasikilizaji waeleze mifano kutoka mambo waliyojionea wenyewe.
Wimbo 152 na sala ya kumalizia.
Juma toka Oktoba 18
Wimbo 196
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na mambo yaliyoonwa katika utumishi wa shambani.
Dak. 13: “Je! Wewe Unapanga Kuhama?” Hotuba yenye kutia moyo inayotolewa na mwandishi. Wakati wahubiri wanapoona kuwa jambo la lazima kuhamia kutaniko jingine, ni jambo la maana kwamba wajulikane vizuri katika mazingira yao mapya ili kuepuka kushuka kiroho. Tia mkazo juu ya uhitaji wa kujulisha wazee kuhusu mipango kama hiyo na kuomba msaada wao katika kupashana habari na kutaniko jipya.
Dak. 22: “Utasema Nini kwa Myahudi?” Maulizo na majibu. Fasiria tofauti kati ya Dini ya Kiyahudi ya Orthodox, ya Reform, na ya Conservative. (Ona Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, kurasa 226-7.) Vuta uangalifu juu ya mahali ambapo tunaelekea kusitawisha uwanja wa makubaliano na Myahudi. Fanyeni onyesho la utoaji uliotayarishwa vema. Ili kupata habari zaidi kuhusu Dini ya Kiyahudi, ona nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1998; kitabu Kutoa Sababu, kurasa 22-3; na Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, ukurasa 9.
Wimbo 142 na sala ya kumalizia.
Juma toka Oktoba 25
Wimbo 179
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Saidia wote wajitayarishe kutolea watu broshua Anataka au kitabu Ujuzi mnamo Novemba. Fasiria jinsi ya kutayarisha utoaji wenye kutia mkazo juu ya ulizo, “Je! Mungu hujibu sala?” Tumia nukta kutoka somo 7 katika broshua au sura 16, mafungu 12-14, katika kitabu. Fanyeni onyesho la utoaji rahisi ambao unatia ndani andiko moja.
Dak. 15: Kupata Majibu ya Maulizo ya Biblia. Mhubiri ambaye alikuta mtu mwenye kupendezwa aliye na ulizo la Biblia anamkaribia mtumishi wa huduma. Badala ya kutoa jibu, mtumishi wa huduma anafasiria jinsi ya kulipata. Kwanza, anarudilia madokezo yanayopatikana katika Kiongozi cha Shule, somo 7, mafungu 8-9. Kisha, wanatafuta pamoja ulizo linaloulizwa kwa kawaida katika eneo la kwao. Wanatafuta vichapo vinavyozungumzia habari hiyo na wanapata nukta zenye kusadikisha ambazo huelewesha sababu ya msingi ya jibu la Biblia. Tia moyo wasikilizaji wafanye aina hiyo ya funzo lenye kuthawabisha ili kutafuta maulizo ya Biblia.
Dak. 15: Miradi Tunayoweza Kujiwekea. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Rudilia miradi yenye mafaa inayoonyeshwa katika kisanduku kwenye ukurasa 11 wa Mnara wa Mlinzi wa Machi 15, 1997. Tia ndani kitia-moyo cha kushiriki katika utumishi wa painia msaidizi au wa painia wa kawaida. Fasiria jinsi kutimiza miradi hiyo kunavyoweza kutufaidi sisi binafsi. Alika wasikilizaji waeleze baadhi ya furaha walizopata wakati walipokuwa na uwezo wa kutimiza miradi fulani ya kitheokrasi.
Wimbo 151 na sala ya kumalizia.