Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichotangazwa kabla ya 1986 ambacho kutaniko linaweza kuwa nacho katika stoki. Makutaniko yasiyokuwa na vitabu hivyo yanaweza kutolea watu vitabu La vie : comment est-elle apparue? Évolution ou création? au Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Februari: Siri ya Kupata Furaha ya Familia.
◼ Mnamo Januari na Februari, makutaniko huko Katanga yatagawa broshua Roho za wafu na Mashahidi wa Yehova Katika Karne ya 20. Ombi linaweza kuingizwa kwenye depo ya Lubumbashi.
◼ Waandishi wanatiwa moyo kuandika katika Kifaransa wakati wanapotuma barua kwenye Ofisi ya Tawi. Wanaweza kuandika katika lugha nyingine ikiwa tu hakuna mzee hata mmoja anayejua kuandika Kifaransa.
◼ Wahubiri wote wenye kubatizwa waliopo kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma la Januari 10 wanaweza kupata kadi Instructions médicales/Pas de sang na Carte d’identité kwa ajili ya watoto wao.
◼ Kuanzia Februari, na ikiwa kuchelewa Machi 5, hotuba mpya kwa ajili ya waangalizi wa mzunguko itakuwa “Armagedoni ya Kweli—Kwa Nini na Wakati Gani?”
◼ Makutaniko yangepaswa kuchukua mipango yenye kufaa ili kusherehekea Ukumbusho mwaka huu Siku ya Tatu, Aprili 9, baada ya kutua kwa jua. Ingawa hotuba inaweza kuanza mapema, kupitishwa kwa mifano hakungepaswa kuanza kabla ya kutua kwa jua. Ulizeni watu wa mahali penu ili kujihakikishia wakati ambapo jua hutua kwenu. Ingawa inatamanika kwa kila kutaniko kufanya sherehe yalo lenyewe ya Ukumbusho, hilo huenda lisiwezekane sikuzote. Mahali ambapo makutaniko mengi kwa kawaida hutumia Jumba la Ufalme lilelile, labda kutaniko moja au zaidi linaweza kupata majengo mengine kwa ajili ya jioni hiyo. Mahali ambapo hilo linawezekana, tungependekeza angalau dakika 40 kati ya programu mbalimbali kusudi wote wafaidike kikamili na tukio hilo; dakika hizo zitaruhusu kuwe wakati wa kusalimu wageni na kutia moyo wale waliopendezwa juzijuzi.
◼ Hotuba ya pekee ya watu wote kwa ajili ya kipindi cha Ukumbusho 2000 itatolewa Siku ya Yenga, Aprili 16. Kichwa cha hotuba hiyo kitakuwa “Kwa Nini Wanadamu Wanahitaji Ukombozi.” Muhtasari utatolewa. Yale makutaniko yanayokuwa na ziara ya mwangalizi wa mzunguko, au mkusanyiko wa mzunguko, au kusanyiko la pekee la siku moja mwisho-juma huo yatafanya hotuba ya pekee juma lenye kufuata. Hakuna kutaniko linalopaswa kufanya hotuba ya pekee kabla ya Aprili 16, 2000.