Programu ya mikutano ya utumishi
Juma toka Januari 10
Wimbo 107
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 15: “Kufanya Jina la Yehova Lijulikane Katika Dunia Yote.” Mazungumzo ya maulizo na majibu. Tia ndani maelezo kutoka katika kitabu Huduma Yetu, kurasa 93-4, kuhusu kutoa ushahidi wa vivi hivi.
Dak. 20: Kufanya Uchaguzi wa Kisheria wa Matunzo ya Afya Yasiyotumia Damu. (Mdo. 15:28, 29) Hotuba inayotolewa na mzee mwenye ustadi. Taja barua ya Desemba 20, 1996, inayofasiria jinsi ya kutumia hati “ Attestation prévisionnelle. ” Baada ya mkutano huu, Mashahidi wenye kubatizwa wanaweza kupata kadi mpya Instructions médicales/Pas de sang, na wale walio na watoto wadogo wasiobatizwa wanaweza kupokea Carte d’identité kwa ajili ya kila mtoto. Kadi hizo hazipaswi kujazwa usiku huu. Hizo zingepaswa kujazwa kwa uangalifu nyumbani, lakini HAPANA kuzitia sahihi. Kutiwa sahihi, majina ya mashahidi na tarehe kwenye kadi zote kutafanywa baada ya Funzo la Kitabu lijalo, kukiwa msaada wa kiongozi wa funzo la kitabu, ikiwa huo unahitajiwa. Kabla ya kutia sahihi, hakikisha kwamba kadi zinajazwa kikamili. Wale wanaotia sahihi wakiwa mashahidi wangepaswa kwelikweli kuona mwenye-kadi akitia hati hiyo sahihi. Kwa kupatanisha maneno ya kadi hii na hali na imani zao wenyewe, wahubiri wasiobatizwa wanaweza kuandika mwongozo wa kutumia kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya watoto wao. Viongozi wa Funzo la Kitabu wangepaswa kuhakikisha kwamba wale wote walio sehemu ya kikundi chao wanapata msaada wanaotaka ili kujaza kadi Instructions médicales/Pas de sang.
Wimbo 155 na sala ya kumalizia.
Juma toka Januari 17
Wimbo 12
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti.
Dak. 15: Mwandishi anarudilia barua ya Septemba 15, 1999, iliyotumwa kwa makutaniko yote. Maagizo hayo ni ya kisasa tena zaidi kwa kuwa hatuombi tena malipo kwa ajili ya vichapo vyetu. Bidhaa ambazo hufanyiwa ombi la pekee zitakuja kupitia kutaniko. Kazia kwamba wote wanaweza kufikia kupata ujuzi sahihi. Huo hautegemei mali ya kila mtu. Bidhaa ambazo hufanyiwa ombi la pekee si za lazima ili kusaidia wapya wapate uhusiano mzuri pamoja na Mungu.
Dak. 20: “Tumieni Trakti ili Kuanzisha Mazungumzo.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Rudilia trakti nne zozote zinazotumiwa kwa kawaida katika eneo. Uliza ulizo linalojibiwa katika kila trakti. Alika wasikilizaji waseme jinsi ulizo hilo lingeweza kutumiwa ili kuanzisha mazungumzo na kuongoza iwezekanavyo kwenye funzo la Biblia. Kwa kutumia trakti mbili, fanyeni onyesho la jinsi hilo linaweza kufanywa. Ndugu anayeongoza sehemu hii atakazia kwamba wahubiri wote wangepaswa kujifunza kuanzisha mazungumzo kwa kutumia trakti. Mpango mpya uliorahisishwa kuhusiana na zawadi unataka kwamba tuzungumze na mtu kabla ya kumtolea kichapo, ili kutambua jinsi anavyopendezwa na ujumbe. Trakti ndivyo vyombo vinavyofaa.
Wimbo 57 na sala ya kumalizia.
Juma toka Januari 24
Wimbo 110
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: “Chunguzeni Neno la Yehova Kila Siku!” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tia moyo kila mmoja afanye matumizi mazuri ya Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2000. Tia ndani maelezo kutoka dibaji, kurasa 3-4. Alika wahubiri waeleze jinsi wanavyofanya jitihada ya pekee ili kuchunguza andiko na maelezo kwa uaminifu kila siku wakiwa watu mmoja-mmoja na wakiwa familia.
Dak. 25: “Tutumie Vichapo kwa Hekima.” Mazungumzo ya maulizo na majibu, yakiongozwa na mwangalizi wa utumishi. Baada ya kuchunguza fungu 7, fanyeni maonyesho mawili au matatu yenye kutayarishwa vizuri, yakionyesha jinsi ya kufuata madokezo fulani yanayotolewa kwenye mafungu 4 hadi 7. Viongozi wanatiwa moyo kurudilia nukta hizo wakati wa mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani.
Wimbo 157 na sala ya kumalizia.
Juma toka Januari 31
Wimbo 16
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote watoe ripoti ya utumishi wa shambani ya Januari. Taja toleo la vichapo la Februari: kitabu Furaha ya Familia. Fanyeni onyesho la jinsi yale maulizo matatu katika kisanduku kwenye ukurasa 12 wa kitabu hicho yanavyoweza kutumiwa yakiwa msingi wa kuhusisha mtu katika mazungumzo.
Dak. 15: Jibu la Ulizo Kuhusu ‘Kutia Alama.’ Hotuba inayotolewa na mzee, ikiwa na msingi juu ya Mnara wa Mlinzi wa Julai 15, 1999, kurasa 29-31.
Dak. 18: Jinsi ya Kusaidia Wengine Watambue Dini ya Kweli. Mazungumzo kati ya mtumishi wa huduma mwenye sifa na wahubiri wawili au watatu wenye uwezo, kuhusu jinsi huenda watu wakaguswe moyo na Mashahidi wa Yehova lakini wasielewe waziwazi tofauti kati ya dini nyinginezo na ile yetu. Rudilia zile nukta kumi zinazozungumziwa kwenye ukurasa 20 wa Amkeni! ya Mei 8, 1995. Fasiria jinsi kujua mambo hayo kunavyoweza kusaidia mtu mwenye unyofu kuona tofauti kati ya ibada ya kweli na ile isiyo ya kweli, na uhitaji wa kujifunza kutoka kwa watu wa Yehova na kushirikiana nasi.
Wimbo 60 na sala ya kumalizia.
Juma toka Februari 7
Wimbo 113
Dak. 8: Matangazo ya kwenu.
Dak. 17: Sikiliza Unabii wa Danieli! Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Rudilia mambo makuu ya kitabu hicho kipya: Vichwa vya sura vyenye kuvutia, picha zenye kupendeza, visanduku vyenye maulizo yanayoomba kufanyiwa utafiti mwishoni mwa kila mazungumzo, ramani zinazofanya mambo madogo-madogo yaeleweke zaidi. Zungumzia mafasirio yenye kutia moyo kuhusu jinsi Mikaeli atakavyosimama kwa njia ya pekee. (Kurasa 288-90) Zungumzia umaana wa kuvumilia kwetu tukiwa wafundishaji wa Neno la Mungu. (Kurasa 311-12) Sisi sote tungepaswa kusoma kitabu hicho kwa uangalifu na kusihi wale wenye kupendezwa wafanye vivyo hivyo.
Dak. 20: Walifanya Uchaguzi Wenye Hekima. Hotuba yenye msingi juu ya Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 15, 1997, kurasa 19-21, mafungu 3-16. Eleza maneno ya mapainia wenye shauku, yakionyesha kwa nini wao wanafikiri kwamba maisha zao zimepitishwa kwa namna yenye kuthawabisha na yenye mafaa zaidi, yakiwaletea furaha na kutosheka kwingi zaidi. Tia moyo wote kati ya wasikilizaji wafikiri juu ya mambo hayo yaliyoonwa na kukadiria mataraja yao wenyewe ya kupainia.
Wimbo 182 na sala ya kumalizia.