Programu ya mikutano ya utumishi
Juma Toka Septemba 11
Wimbo 139
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Chunguzeni ripoti za Aprili 2000 za nchi ya Congo-Brazzaville na Congo-Kinshasa, na pia habari “Je, Tunaweza Kufanya Vizuri Zaidi?”
Dak. 15: “Baraka ya Yehova Hututajirisha.” Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu.—Ona Étude Perspicace, Buku 2, ukurasa 798, mafungu 12-3.
Dak. 20: “Tumieni Matukio ya Sasa ili Kuamsha Kupendezwa.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji na maonyesho. Taja matukio mbalimbali ya sasa ambayo yalitokeza kupendezwa mahali penu. Matukio hayo yametokeza mahangaiko gani kuhusu wakati ujao? Kwa kutumia kitabu Kutoa Sababu, ukurasa 12, toa madokezo fulani juu ya jinsi ya kutayarisha utangulizi utakaoongoza kwenye mazungumzo ya Biblia. Fanyeni maonyesho mawili yenye kutumika na yaliyotayarishwa vema.
Wimbo 224 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Septemba 18
Wimbo 2
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti.
Dak. 15: Tulifanya Nini Mwaka Uliopita? Hotuba inayotolewa na mwangalizi wa utumishi. Rudilia mambo makuu kutoka katika ripoti ya kutaniko ya mwaka wa utumishi wa 2000. Toa pongezi kwa mambo mazuri yaliyotimizwa. Onyesha mahali ambapo mambo yanahitaji kufanywa kuwa bora. Kazia yale ambayo kutaniko lilifanya kuhusiana na kuhudhuria mikutano, kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia, na kuwa kawaida katika utumishi wa shambani. Onyesha kwa kifupi miradi yenye kufaa kwa ajili ya mwaka unaokuja.
Dak. 20: “Uhai wa Watu Ni Katika Hatari!” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Kazia maandiko yanayotajwa katika makala.
Wimbo 30 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Septemba 25
Wimbo 93
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti ya utumishi wa shambani ya Septemba. Rudilia Kisanduku cha Maulizo.
Dak. 15: “Je, Mmefahamu Maana Yake?” Mazungumzo ya maulizo na majibu yanayoongozwa na mwangalizi wa utumishi. Fanyeni matumizi kulingana na mahitaji ya kutaniko.
Dak. 15: “Namna Nyepesi Zaidi ya Kugawa Vichapo.” Mazungumzo kati ya mwangalizi-msimamizi na mwandishi.
Wimbo 115 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Oktoba 2
Wimbo 169
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Julisheni kutaniko kuhusu ugawaji wa pekee uliopangwa wa Habari za Ufalme Na. 36, ambao utaanza Siku ya Kwanza, Oktoba 16, na kuendelea mpaka Siku ya Tano, Novemba 17. Sihi wote, kutia ndani vijana na wapya, wajitahidi kushiriki kikamili. Viongozi wa Funzo la Kitabu wanapaswa kuanza sasa kutia moyo na kupanga wote katika kikundi chao ili kushiriki kwa bidii zaidi iwezekanavyo. Tia ndani mambo yaliyoonwa yenye kujenga yanayotokana na ugawaji uliopita wa Habari za Ufalme.
Dak. 15: “Je, Ninapaswa Kuhama?” Hotuba inayotolewa na mzee. Eleza kwa nini kuna uhitaji wa kuonyesha utambuzi katika kuchukua uamuzi wa kuhamia mahali pengine. Zungumzia jinsi ya kutumia shauri linalopatikana kwenye Mezali 22:3. Tia ndani maonyo yanayopatikana katika Mnara wa Mlinzi wa Agosti 15, 1988, ukurasa 22.
Dak. 15: Mambo Yaliyoonwa Katika Kuanzisha Mazungumzo. Katika programu ya Mkutano wa Utumishi ya juma toka Septemba 11, ilipendekezwa kwamba tutoe matangulizi kuhusu matukio ya sasa ili kuamsha kupendezwa na kuanzisha mazungumzo katika huduma. Omba wasikilizaji waeleze matokeo mazuri ambayo wamefurahia mpaka sasa kwa kutumia madokezo hayo.
Wimbo 205 na sala ya kumalizia.