Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/00 uku. 2
  • Programu ya mikutano ya utumishi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu ya mikutano ya utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Vichwa Vidogo
  • Juma Toka Novemba 13
  • Juma Toka Novemba 20
  • Juma Toka Novemba 27
  • Juma Toka Desemba 4
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 11/00 uku. 2

Programu ya mikutano ya utumishi

Juma Toka Novemba 13

Wimbo 4

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme.

Dak. 13: Kisanduku cha Maulizo. Hotuba inayotolewa na mzee.

Dak. 22: “Tukuze Kupendezwa Kulikoamshwa na Habari za Ufalme Na. 36.” Mazungumzo ya maulizo na majibu ya mafungu 1-5. Toa kwa kifupi mipango ya mahali penu kwa ajili ya kutembelea eneo lolote ambalo halijatumikwa. Rudilieni utoaji katika mafungu 7 na 8 kwa ajili ya ziara za kurudia, na mfanye onyesho la kila utoaji. Kazieni umaana wa kufuatia kila kupendezwa, na kujitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Malizieni kwa kuzungumzia fungu 9 na maandiko yenye kutajwa.

Wimbo 63 na sala ya kumalizia.

Juma Toka Novemba 20

Wimbo 111

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti.

Dak. 15: Mambo Yaliyoonwa Katika Kugawa Habari za Ufalme Na. 36. Toa ripoti kuhusu mafanikio katika kutembelea eneo. Je, mtu yeyote katika kutaniko alishiriki katika utumishi kwa mara ya kwanza? Toa habari kuhusu maelezo mazuri yaliyotolewa na wenye-nyumba. Je, wahubiri fulani waliweza kuanzisha mafunzo ya Biblia? Ikiwa ndiyo, waombe waeleze au kucheza upya jinsi walivyofanya jambo hilo. Kumbusha wote wakomaze kupendezwa kulikopatikana.

Dak. 20: “Tuendelee Kuhubiri!” Hotuba na mahojiano. Watu fulani wamekuwa wakishirikiana na tengenezo la Yehova, nao wamedumu katika kazi ya kuhubiri muda wa maisha yao yote. Wakiwa na mwelekeo wenye kutazamia mema, wamepata furaha kwa kufanya hivyo. (Ona kitabu Ujuzi, ukurasa 179, fungu 20, na Mnara wa Mlinzi wa Mei 1, 1992, kurasa 21-2, mafungu 14-15.) Alika mhubiri ambaye amekuwa mwenye kutenda kwa miaka mingi aeleze kwa nini alidumu katika kazi ya kuhubiri.

Wimbo 141 na sala ya kumalizia.

Juma Toka Novemba 27

Wimbo 153

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Novemba. Toleo la vichapo la Desemba ni kitabu Ujuzi pamoja na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Eleza jinsi Mashahidi wa Yehova walivyotimiza fungu la maana katika kutoa Biblia katika lugha nyingi.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 15, 1997, kurasa 11-12.

Dak. 20: Fanyeni Matumizi Mazuri ya Kitabu Kutoa Sababu. Mazungumzo ya maulizo na majibu ya kurasa 7-8. Onyesha jinsi kitabu hicho kinavyokusudiwa ili kutusaidia kujitayarisha kwa ajili ya kushiriki kwa matokeo zaidi katika huduma. Eleza jinsi kitabu hicho kinavyoweza kutumiwa wakati wa kutoa ushahidi kwa njia ya simu. Fanyeni onyesho la jinsi ya kupata habari yenye kusaidia ili kujibu ulizo fulani. Himiza wote wafahamiane na kitabu hicho, wakichunge katika mfuko wao wa mahubiri, na kukitumia kikawaida.

Dak. 15: Ninawezaje Kudhibiti Mazoea Yangu ya Kutazama Televisheni? Mzee mmoja anazungumza na ndugu aliye kijana ambaye anapitisha saa nyingi kila siku akitazama televisheni. Kwanza, ndugu anasisitiza kwamba hakuna hasara yoyote katika jambo hilo. Anasema kwamba hiyo ni aina tu ya kiburudisho na kwamba hapatwi na uvutano mbaya wowote. Mzee anarudilia nukta kubwa katika sura ya 36 ya kitabu Vijana Huuliza. Anaeleza kwamba kutazama televisheni kupita kiasi kunakula wakati wa thamani ambao mtu anaweza kutumia kwa njia nyingine akifanya funzo la kibinafsi, akienda katika huduma, au akisaidia katika mahitaji ya kutaniko. Ndugu yule kijana anaonyesha uthamini kwa ajili ya shauri, naye anasema kwamba, kwa ajili ya faida yake ya kiroho, atabadili mazoea yake ya kutazama televisheni.

Wimbo 175 na sala ya kumalizia.

Juma Toka Desemba 4

Wimbo 189

Dak. 10: Matangazo ya kwenu.

Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko.

Dak. 20: “Neno Linalosemwa kwa Wakati Wenye Kufaa.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji, na maonyesho. Wengi hujisikia kuwa wasio na uwezo wa kutosha wakati wanapojaribu kuanzisha mazungumzo, wakifikiri kimakosa kwamba wanahitaji ufundi wa pekee ili kupata matokeo. Eleza jinsi sisi sote, kutia ndani wahubiri wapya na vijana, tunavyoweza kuanzisha mazungumzo kwa kutumia jitihada yenye kiasi. Rudilieni utoaji mbalimbali uliopendekezwa, mkikazia wepesi wake, na mwombe wahubiri wawili au watatu wafanye maonyesho ya utoaji huo mbalimbali. Jielekezeni kwenye Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 1998, kwa ajili ya utoaji wa ziada ambao unaweza kutumiwa. Himizeni wote wawe wenye kutazamia mema ili wapate furaha nyingi zaidi katika huduma.

Wimbo 218 na sala ya kumalizia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine