Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 12/00 uku. 1
  • Ogopeni Yehova mchana kutwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ogopeni Yehova mchana kutwa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 12/00 uku. 1

Ogopeni Yehova mchana kutwa

1 “Woga wa BWANA [Yehova, NW] ni mwanzo wa akili.” (Zab. 111:10) Huo unatuchochea kufanya kazi nzuri, na unatusaidia kugeuka mbali kutoka lile lililo baya. (Mez. 16:6) Woga huo ni heshima yenye kina kirefu kuelekea Muumba wetu, ukituchochea tuepuke kumchukiza na kukosa kumtii yeye. Ni kitu ambacho tunahitaji kukomaza na kuonyesha mchana kutwa.—Mez. 8:13.

2 Kila siku, roho ya ulimwengu wa Shetani inatia mkazo wa ajabu juu yetu ili tujipatanishe na njia zake mbovu. (Efe. 6:11, 12) Mwili wetu usiokamilika ni wenye dhambi, nao kwa kawaida unaelekea kufanya lililo baya. (Gal. 5:17) Kwa hiyo, ili kutii amri za Yehova, kuwa wenye furaha, na kupata uzima, tunapaswa kumwogopa yeye mchana kutwa.—Kum. 10:12, 13.

3 Kwenye Waebrania 10:24, 25, tunashauriwa kukusanyika pamoja ili kutiana moyo “zaidi sana” katika nyakati hizi tunamoishi. Kuhudhuria mikutano kikawaida ni kwa lazima sana ikiwa tutaokoka siku hizi za mwisho. Woga wetu wa kumchukiza Mungu unatuchochea tuhudhurie mikutano na kuthamini sana kusudi layo. Wale wanaomwogopa Mungu huona kushiriki katika mikutano ya Kikristo kuwa pendeleo takatifu.

4 Kutii amri ya kuhubiri habari njema ya Ufalme ni njia nyingine ambayo kwa hiyo tunaonyesha woga wetu kuelekea Mungu. (Mt. 28:19, 20; Mdo. 10:42) Kusudi la kwanza la kazi yetu ya kuhubiri ni kusaidia wengine wakomaze woga wa Yehova na kujitiisha chini ya mapenzi yake. Tunatimiza hilo kwa kufanya ziara za kurudia, kwa kujitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani, na kisha kwa kufundisha wengine amri zote za Mungu. Kwa njia hiyo, tunaonyesha woga wetu kuelekea Yehova na upendo wetu kwa jirani.—Mt. 22:37-39.

5 Wale wasiomwogopa Mungu hushindwa kukomaza mwelekeo wenye uthamini kuelekea mambo ya kiroho, nao hushindwa na roho ya ulimwengu, au mwelekeo wa akili, wenye kuua. (Efe 2:2) Acheni azimio letu liwe la “kutolea Mungu . . . utumishi mtakatifu kwa hofu ya kimungu na [woga].” (Ebr. 12:28) Hivyo, tutavuna baraka wanazopata wale wanaomwogopa Yehova mchana kutwa.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine