Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/03 uku. 2
  • Programu Ya Mikutano Ya Utumishi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu Ya Mikutano Ya Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 1/03 uku. 2

Programu Ya Mikutano Ya Utumishi

Juma Toka Januari 13

Wimbo 69

Dak. 10:Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Kwa kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 4, fanyeni maonyesho mawili tofauti kuhusu jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi wa Januari 15 na Amkeni! ya Januari 22. Katika kila tamasha, magazeti mawili yanapaswa kutolewa yakiwa pamoja, hata ingawa ni moja tu ndilo linaloonyeshwa.

Dak. 15:Wamevutwa Bila Neno. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Mwenendo bora wa Kikristo ni ushahidi wenye nguvu. Umechochea wenzi fulani wasioamini wawe waabudu wa Yehova. (1 Pet. 3:1, 2) Simulieni mambo yaliyoonwa yanayopatikana katika Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1999, ukurasa wa 4; Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 1, 1995, ukurasa wa 10-11; na Kitabu-Mwaka 1995, ukurasa wa 46. Chukueni mipango kimbele ili wasikilizaji wawili au watatu watoe maelezo kuhusu matokeo yenye kufaa ambayo wameona yakitokana na kufuata shauri la Biblia katika njia hiyo.

Dak. 20:“Tuishi Kulingana na Wakfu Wetu.”* Baada ya kuchunguza fungu la 3, hoji kwa kifupi kijana aliyebatizwa. Ni majaribu gani ambayo amekutana nayo tangu alipobatizwa? Ni nini kilichomsaidia apambane na majaribu hayo kwa matokeo? Amefaidikaje na kuweka maisha yake wakfu kwa Yehova?

Wimbo 22 na sala ya kumalizia.

Juma Toka Januari 20

Wimbo 44

Dak. 8:Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti.

Dak. 15:Je, Mnachunguza Maandiko Kila Siku? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tia wote moyo wafanye matumizi mazuri ya broshua Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2003. Zungumzieni maelezo kutoka dibaji, ukurasa wa 3-4. Toeni mapendekezo kuhusu jinsi familia zinavyoweza kuzungumzia andiko pamoja. Ili kuonyesha faida zinazotokana na kuchunguza andiko kila siku, zungumzieni mifano miwili au mitatu ya andiko na maelezo yanayopangwa kuchunguzwa mwezi ujao. Tieni ndani onyesho fupi la mume na mke wakichunguza pamoja andiko la siku ya leo na maelezo yake.

Dak. 22:“Fundisheni Wengine Lugha Safi.”* Baada ya kuchunguza fungu la 6, omba mhubiri mmoja mwenye uwezo afanye onyesho la jinsi ya kuanzisha funzo la Biblia linaloongozwa kwenye mlango wa mtu anapofanya ziara ya kurudia, akitumia mmoja wa ule utoaji mbalimbali katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002, ukurasa wa 4. Tia ndani uchunguzi wa fungu moja katika broshua Anataka. Omba mhubiri amalizie kwa kutokeza ulizo kuhusu fungu lifuatalo na kuchukua mipango ili kulijibu kwenye ziara ijayo. Tia wote moyo waangalie ikiwa mtu yeyote kati ya wale wanaowatembelea anaweza kuwa tayari kujifunza Biblia kwa namna hiyo.

Wimbo 68 na sala ya kumalizia.

Juma Toka Januari 27

Wimbo 92

Dak. 10:Matangazo ya kwenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani. Kwa kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 4, fanyeni maonyesho mawili tofauti kuhusu jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi wa Februari 1 na Amkeni! ya Februari 8. Eleza kwa kifupi jinsi tunavyoweza kurudilia watu tuliowaachia magazeti.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Agosti 2002,ukurasa wa 8, fungu la 10.

Dak. 15:Je, Mnaheshimu Mahali Penu pa Ibada? * (w93-SW 6/15 uku. 28-31) Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji, yakiongozwa na mzee. Tieni ndani maelezo kutoka katika kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 61-62, na Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 1999, ukurasa wa 7.

Dak. 20:Saidieni Wengine Wamkaribie Yehova. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tutatolea watu kile kitabu kipya mnamo Februari. Zungumzia taarifa kwa wasomaji kwenye ukurasa wa 3, na ukazie sehemu fulani za kitabu hicho zenye kutokeza. Kila moja ya zile sehemu nne inakazia ya zile sifa kubwa za Yehova. Sura yenye kufafanua jinsi Yesu alivyoonyesha sifa hiyo na sura yenye kuzungumzia jinsi tunavyoweza kuionyesha inatiwa ndani. Kuna picha 17 za maonyesho ya Kibiblia zenye kuchukua ukurasa nzima. Yale “Maswali ya Kutafakari” yanatusaidia kufikiri juu ya sehemu za maana za habari. Rudilia kisanduku “Utoaji Mbalimbali Uliopendekezwa kwa Ajili ya Kutoa Kitabu Mkaribie Yehova,” na uombe mhubiri mwenye uwezo afanye onyesho la mmoja wa utoaji huo.

Wimbo 124 na sala ya kumalizia.

Juma Toka Februari 3

Wimbo 9

Dak. 15:Matangazo ya kwenu. Rudilia Kisanduku cha Maulizo.

Dak. 12:Igeni Imani Yao. Hoji mzee moja ambaye ametumikia Yehova kwa unyenyekevu na kwa uaminifu kwa miaka mingi. (Ebr. 13:7) Alijifunzaje kweli? Ni vizuizi gani alivyolazimika kushindana navyo kwa ajili ya kweli? Ni kitia-moyo au maandalizi gani ya kiroho yaliyomsaidia aendelee mbele? Alifanya nini ili kufikia daraka la mwangalizi katika kutaniko? (1 Tim. 3:1) Ni nini kimemsaidia kusawazisha madaraka ya kutaniko na wajibu mbalimbali wa kimwili na wa kifamilia? (1 Tim. 5:8) Anaonaje lile pendeleo la kusaidia wengine katika kutaniko?

Dak. 18:“Kazi Inayoomba Unyenyekevu.”* Mnapozungumzia fungu la 3, alika wasikilizaji watoe mapendekezo kuhusu jinsi ya kuitikia ikiwa mtu fulani katika eneo anajaribu kutudhihaki au ni mwenye kukosa adabu, mbishi, au mwenye hasira. Mnapozungumzia fungu la 4, tieni ndani maelezo kuhusu Étude Perspicace, Buku 1, ukurasa wa 1158, fungu la 2. Kazia kwamba kazi ya kuhubiri inaomba unyenyekevu ijapokuwa watu kwa kawaida ni wepesi kukaribia katika eneo letu.—w02-SW 8/15 uku. 19.

Wimbo 133 na sala ya kumalizia.

* Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine