Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa kabla ya 1988 kinaweza kutolewa. Makutaniko ambayo hayana kitabu cha zamani chenye kurasa 192 yanaweza kutolea watu kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? au Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Februari: Kile kitabu kipya chenye kichwa Mkaribie Yehova kitatolewa. Machi: Toleeni watu kitabu Ujuzi. Jitihada ya pekee itafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Aprili na Mei: Toleeni watu nakala za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mnapofanya ziara za kurudia kwa watu waliopendezwa, ambao huenda wakatia ndani wale waliohudhuria Ukumbusho na/au matukio mengine ya kitheokrasi lakini ambao hawashirikiani kwa bidii na kutaniko, kazeni fikira juu ya kuwaachia kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli. Kila jitihada inapaswa kufanywa ili kuanzisha funzo la Biblia la nyumbani, zaidi sana ikiwa watu fulani wamekwisha kujifunza kitabu Ujuzi na broshua Anataka.
◼ Kuanzia Februari, wala si baada ya Machi 2, hotuba mpya ya watu wote itakayotolewa na waangalizi wa mzunguko itakuwa yenye kichwa “Kuokolewa Kutoka Ulimwengu wa Giza.”
◼ Makutaniko yanapaswa kuchukua mipango yenye kufaa ili kuadhimisha Ukumbusho mwaka huu, Siku ya Tatu, Aprili 16, baada ya jua kutua. Ingawa hotuba inaweza kuanza mapema, kupitishwa kwa mifano hakupaswi kuanza mpaka jua linapokuwa limetua. Ulizeni watu wa mahali penu ili kujua wakati ambapo jua hutua katika eneo lenu. Ingawa ni vizuri kila kutaniko lifanye mwadhimisho walo lenyewe wa Ukumbusho, huenda hilo lisiwezekane sikuzote. Mahali ambapo makutaniko mengi hutumia kwa kawaida Jumba la Ufalme lilelile, labda kutaniko moja au zaidi yanaweza kupata kibali cha kutumia jengo lingine jioni hiyo. Mahali ambapo inawezekana, tungependekeza afadhali kuwe na dakika 40 kati ya programu mbalimbali kusudi wote wafaidike kikamili na tukio hilo. Ufikirio unapaswa pia kutolewa kuhusiana na hali za usafiri na uegeshaji wa magari, kutia ndani kuacha na kutwaa wasafiri. Baraza la wazee linapaswa kuamua ni mipango gani inayoweza kuwa bora zaidi mahali pao.
◼ Kuanzia toleo hili, orodha ya vichapo vipya vinavyopatikana haitaonekana tena katika Huduma Yetu ya Ufalme. “Tangazo kwa Makutaniko Yote” lenye kuwa na habari hii litaendelea kutumwa katika barua kwa makutaniko yote kila mwezi. Tunawakumbusha kwamba mara tu “Tangazo kwa Makutaniko Yote” litakapopokewa, tangazo linapaswa kufanywa kwenye Mkutano wa Utumishi wenye kufuata kuhusu vichapo vinavyoweza kupendeza kutaniko lenu. Kisha, tangazo hilo linaweza kutiwa kwenye ubao wa matangazo. Baadaye, ndugu anayehusika na vichapo ataichunga katika faili yake.