Programu ya Mikutano ya Utumishi
Juma Toka Mei 10
Wimbo 193
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ikiwa mapendekezo kwenye ukurasa wa 4 ni yenye kufaa eneo la kutaniko lenu, yatumieni ili kuonyesha jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa Mei 15 na Amkeni! ya Mei 22.# Maonyesho mengine yanaweza kutumiwa. Katika kila onyesho, onyesha njia tofauti ya kushughulikia kizuia-mazungumzo “Nina dini yangu mwenyewe.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 18-19.
Dak. 15: Je, Umekwisha Kuzungumza na Bwana Wako wa Kazi? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yatakayoongozwa na mzee, yenye kutegemea makala “Je, Wewe Utakuwako?” katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 2000, ukurasa wa 1. Tia ndani maelezo ya kitabu Shule ya Huduma ukurasa wa 67.
Dak. 20: “Panukeni.”* Tia ndani maelezo ya kitabu Mwabudu Mungu, ukurasa wa 150, fungu la 14.
Wimbo 18 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Mei 17
Wimbo 188
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: “Onyesha Shukrani Yako.”* Wakati ukiruhusu, omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yanayotajwa. Mnapozungumzia fungu la 3, omba mtu mmoja au wawili waliotumikia karibuni wakiwa mapainia wasaidizi waeleze kuhusu baraka walizopata kwa kufanya hivyo.
Dak. 20: Tunahangaikiana. (1 Kor. 12:25, 26) Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 157-9, chini ya kichwa “Kuhangaikiana.” Ijapokuwa watu wa Yehova wanaishi katika sehemu zote za dunia, sisi ni wenye umoja kabisa. Sote tunapaswa kusali kwa ajili ya ndugu zetu kila siku. Sisi pia tunaitikia kwa uharaka kutoa msaada wa kimwili wakati kuna mahitaji ya haraka. Soma na kuzungumzia maandiko ya msingi, na tia ndani jambo moja au mawili yaliyoonwa kutoka katika vichapo vyetu.
Wimbo 100 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Mei 24
Wimbo 128
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti. Fanyeni onyesho kuhusu jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi wa Juni 1 na Amkeni! ya Juni 8.# Patanisheni kila onyesho na jinsi ya kuvutia mtu fulani wa dini ya mahali penu.
Dak. 15: “Muziki Wenye Kuburudisha.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tia ndani maelezo ya Kitabu-Mwaka 2002, ukurasa wa 175, na Mnara wa Mlinzi wa Februari 1, 1997 ukurasa wa 27, fungu la 1-2.
Dak. 18: Iweni Tayari Kutoa Ushahidi wa Vivi Hivi. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 2003, ukurasa wa 3. Panga kimbele ili watu wachache kati ya wasikilizaji waeleze mambo ambayo wamejionea walipokuwa wakitoa ushahidi wa vivi hivi. Onyesheni kwa kifupi jinsi trakti Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? na kijitabu Habari Njema Kwa Mataifa Yote vinavyoweza kutumiwa tunapotoa ushahidi wa vivi hivi.
Wimbo 211 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Mei 31
Wimbo 26
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Mei.
Dak. 17: Uzima—Zawadi Inayopaswa Kuthaminiwa. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 395-397. Tia ndani maelezo ya Amkeni! ya Mei 22, 1993, ukurasa wa 10-11. Utaelezaje maoni ya Yehova kuhusu utoaji mimba kwa mtu anayefikiri kwamba mwanamke ana haki ya kuamua mambo yanayohusu mwili wake mwenyewe? Eleza jambo lililoonwa linalopatikana katika Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 2000, ukurasa wa 4, fungu la 4-5.
Dak. 20: “Tutolee Watu Kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu.” Mnamo Juni tutatolea watu kichapo hicho. Onyesha mambo yanayofafanuliwa kwenye ukurasa wa 7, fungu la 1-3, la kitabu. Fanya wasikilizaji watoe maelezo kuhusu yale wanayopendezwa nayo kuhusu kitabu hicho. Rudilia utoaji mbalimbali uliopendekezwa. Onyesha jinsi ya kukazia picha unapotolea watu kitabu hicho. Omba kijana mmoja afanye onyesho la utoaji wa kwanza, na mtu mwenye umri mkubwa afanye onyesho la utoaji mwingine. Ikiwa njia tofauti inaweza kuwa na matokeo mazuri katika eneo lenu, hiyo inaweza kutumiwa katika onyesho ikichukua nafasi ya moja ya maonyesho mawili ya mwisho.
Wimbo 24 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Juni 7
Wimbo 136
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Zungumzia mambo makuu ya “Kituo cha Habari Kinachosaidia Watu.” Taja lugha fulani zinazopatikana katika eneo lenu.
Dak. 15: Tumsifu Mungu kwa Kuimba kwa Utaratibu. Usomaji wa barua ya Februari 1, 2004, ukifuatwa na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yatakayoongozwa na mzee kuhusu habari inayopatikana ndani ya barua.
Dak. 20: Tumia Mifano Yenye Matokeo Unapofundisha. Hotuba na mazungumzo yanayotegemea Mnara wa Mlinzi wa Septemba 1, 2002, ukurasa wa 22-4. Ni mambo gani manne yanayofanya mfano uwe wenye matokeo? Kwa nini ni jambo lenye faida kufanya mfano uwe rahisi? Tunaweza kupata mifano mizuri wapi? Zungumzia mifano fulani katika kisanduku kwenye ukurasa wa 23, na mzungumzie kile kinachofanya kila mfano kuwa na matokeo.
Wimbo 133 na sala ya kumalizia.
* Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu.
# Tafadhali tumieni mapendekezo yaliyotolewa kuhusu magazeti ya karibuni zaidi yanayopatikana.