Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 7/04 uku. 2
  • Programu ya Mikutano ya Utumishi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu ya Mikutano ya Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Vichwa Vidogo
  • Juma Toka Julai 12
  • Juma Toka Julai 19
  • Juma Toka Julai 26
  • Juma Toka Agosti 2
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 7/04 uku. 2

Programu ya Mikutano ya Utumishi

Juma Toka Julai 12

Wimbo 108

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Kwa kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 4, onyesheni jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa Julai 15 na Amkeni! ya Julai 22.# Katika onyesho moja, onyesha jinsi ya kutolea mtu gazeti barabarani, mtu ambaye hazungumzi lugha yako vizuri.

Dak. 18: “Tuige Haki ya Yehova.”* Wakati ukiruhusu, omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yanayotajwa.

Dak. 15: Biblia—Kitabu cha Matabiri Yenye Kutegemeka. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, ukurasa wa 27-29. Katika huduma yetu, tunakutana mara nyingi na watu wenye kupendezwa na wakati ujao. Biblia inatoa habari yenye kutegemeka inayoeleza kuhusu wakati ujao wenye kufurahisha kwa ajili ya wanadamu watiifu. Zungumzieni unabii mbalimbali wa Biblia unaoimarisha uhakika katika matabiri ya Biblia kuhusu wakati ujao. Mhubiri fulani afanye onyesho kwa kifupi kuhusu jinsi matukio ya Biblia yanavyoweza kutumiwa ili kusaidia mtu anayependezwa aitumaini Biblia.

Wimbo 16 na sala ya kumalizia.

Juma Toka Julai 19

Wimbo 83

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Zungumzieni umaana wa kudumisha programu ya kawaida ya usomaji wa Biblia wa kila siku. Tia ndani maelezo yanayochukuliwa katika Mnara wa Mlinzi wa Agosti 15, 2000, ukurasa wa 32.

Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko.

Dak. 20: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo—Sehemu 1.” Hotuba itakayotolewa na mwangalizi wa utumishi. Omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu habari iliyo katika kitabu Wapiga-Mbiu, ukurasa wa 572-574, habari inayoonyesha maendeleo ya kazi ya kuongoza mafunzo la Biblia mnamo nyakati za kisasa. Chochea hamu kuhusu mfululizo wa makala zijazo. Vichwa vitakavyochunguzwa vitazungumzia jinsi ya kujitayarisha ili kuongoza funzo, jinsi ya kusaidia mwanafunzi kujitayarisha, kiasi cha habari ya kujifunza na mtu, jinsi ya kutumia maandiko kwa matokeo, jinsi ya kushugulikia maulizo yanayotokezwa na mwanafunzi, wakati gani kuanza kusali na mtu, na jinsi ya kuelekeza mwanafunzi kwenye tengenezo. Tia wote moyo watumie mapendekezo yanayotolewa na kulinda makala hizo ili kuzitumia wakati ujao.

Wimbo 10 na sala ya kumalizia.

Juma Toka Julai 26

Wimbo 216

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Julai. Kwa kutumia mapendekezo yanayopatikana kwenye ukurasa wa 4, fanyeni onyesho kuhusu jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi wa Agosti 1 na Amkeni! ya Agosti 8.# Katika kila onyesho, onyesha njia tofauti ya kushughulika na kizuia-mazungumzo “Mbona ninyi mnatembelea watu mara nyingi mno?”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 20.

Dak.  8: “‘Kuandika Maneno Sahihi ya Kweli.’” Itatolewa na mzee. Soma na kuzungumzia makala nzima.

Dak. 25: “Jinsi ya Kuhubiri Katika Eneo la Biashara.”* Sema kuhusu mipango inayochukuliwa na kutaniko lenu ili kuhubiri katika eneo la biashara. Fanyeni kwa ufupi maonyesho mawili kuhusu utoaji mbalimbali katika fungu la 4-5 au utoaji mwingine ambao umekuwa wenye matokeo katika eneo lenu. Wakati ukiruhusu, omba wasikilizaji wasimulie mambo yenye kutia moyo waliyoona walipokuwa wakihubiri katika eneo la biashara.

Wimbo 173 na sala ya kumalizia.

Juma Toka Agosti 2

Wimbo 60

Dak.  8: Matangazo ya kwenu.

Dak. 22: Je, Unatoa Sababu? Hotuba na mazungumzo yanayotegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 254, fungu la 1-2. Tunapoeleza na kutumia maandiko katika huduma ya shambani na kutoka jukwaani, kufundisha kwetu kutakuwa kwenye matokeo zaidi ikiwa tunatoa sababu ya mambo tunayosema badala ya kusisitiza kwamba ni hivyo tu. Kwa kutumia mifano kutoka kitabu Kutoa Sababu au vichapo vingine vyenye kufaa eneo lenu, onyesheni jinsi ya (1) kuchagua na kueleza maneno makuu katika andiko, (2) kuonyesha uhakikisho wenye kutegemeka kutoka muktadha (contexte) au kutoka andiko lingine lenye kusemea habari hiyo, (3) kutumia mfano ili kuonyesha sababu iliyo ya kweli kuhusu yale ambayo umesema, na (4) kutumia maulizo ili kusaidia wasikilizaji kufikiri juu ya habari hiyo. Kazia faida za kutumia utoaji wenye kumfanya mtu afikiri.

Dak. 15: Mambo yaliyoonwa katika eneo lenu. Omba wasikilizaji wasimulie mambo fulani yenye kujenga yanayohusiana na uhudhuriaji wa mkusanyiko wa wilaya, upainia msaidizi, au utendaji mwingine mbalimbali wa kiroho mpaka wakati huu.

Wimbo 32 na sala ya kumalizia.

* Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu.

# Tafadhali tumieni mapendekezo yaliyotolewa kuhusu magazeti ya karibuni zaidi yanayopatikana.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine