Programu ya Mikutano ya Utumishi
Juma Toka Oktoba 10
Wimbo 17
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Tumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (ikiwa yanafaa eneo lenu), ili kuonyesha jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 15 na Amkeni! ya Oktoba 22. Baada ya kila onyesho, kazia sehemu fulani nzuri za utoaji. Kwa kuongezea, vuta uangalifu kwenye makala nyingine katika magazeti hayo zinazoweza kuvutia watu katika eneo.
Dak. 15: Je, Una Mazoea Mazuri ya Kusoma? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea sehemu zilizochaguliwa kutoka kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 21-26. Tunaweza kutia mambo gani katika programu yetu ya usomaji? (uku. 21, kisanduku) Kwa nini ni jambo la maana kwetu kusoma vichapo tunavyoandaliwa? (uku. 23, fu. 2) Ni nini lililo jambo la maana ili kuwa na programu nzuri ya usomaji? (uku. 26, fu. 3-4) Unapangaje wakati ili kusoma magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni!? Umefaidikaje na jambo hilo?
Dak. 20: “Endelea Kusema Neno la Mungu kwa Ujasiri.”* Omba wasikilizaji waeleze kuhusu hali ambazo katika hizo inaweza kuwa vigumu kujipatia ujasiri unaohitajiwa ili kutoa ushahidi. Ni nini ambacho kimewasaidia kufanya hivyo?
Wimbo 78 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Oktoba 17
Wimbo 36
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Ukitumia sehemu ya 3 ya nyongeza katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 2005, rudilia jambo moja au mambo mawili kuhusu jinsi ya kufanya matumizi mazuri ya Maandiko wakati wa kuongoza mafunzo ya Biblia.
Dak. 15: Epuka Hatari za Internet. Hotuba itakayotolewa na mzee, inayotegemea Amkeni! ya Desemba 8, 2004 ukurasa wa 18-21. Ikiwa hakuna internet katika eneo lenu, kazia kanuni za Kimaandiko ili kusaidia ndugu na dada waepuke uasherati na mashirika mabaya kwa njia ya vyombo vya habari.
Dak. 20: “Onyesha Kupendezwa Kibinafsi na Wengine—Kwa Kuwa na Fadhili.”* Omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jinsi tunavyoweza kuonyesha wengine fadhili tunaposhiriki katika huduma ya shambani. Njia nyingine za kuonyesha kupendezwa kibinafsi na wale tunaowahubiria zitazungumziwa katika matoleo ya baadaye ya Huduma Yetu ya Ufalme.
Wimbo 2 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Oktoba 24
Wimbo 68
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Soma ripoti ya akaunti na shukrani kuhusu zawadi. Ukitumia moja ya utoaji mbalimbali uliopendekezwa katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005 au utoaji mwingine unaofaa eneo lenu, onyesha jinsi ya kutolea watu toleo la mwezi la Novemba.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005 uku. 8, fu. 5.
Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko lenu.
Dak. 20: Kuonyesha Viwango vya Kimungu Katika Namna Yetu ya Kuvalia na Kujipamba. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yatakayoongozwa na mzee, yanayotegemea Mnara wa Mlinzi wa Agosti 1, 2002, ukurasa wa 17-19. Alika wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jinsi namna yetu ya kuvalia na kujipamba inavyoweza kututolea nafasi ya kutoa ushahidi.
Wimbo 153 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Oktoba 31
Wimbo 209
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za mwezi wa Oktoba. Mkitumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (ikiwa yanafaa eneo lenu), onyesheni jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa Novemba 1 na Amkeni! ya Novemba 8. Katika utoaji mmoja, weka msingi wa ziara ijayo kwa kuvuta uangalifu kwenye kisanduku “Katika Toleo Linalofuata.”
Dak. 15: Sitawisha Kupendezwa kwa Watu Unaowaachia Magazeti kwa Ukawaida. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji, yanayotegemea Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 2005, ukurasa wa 8. Tunawezaje kuanzisha mpango wa kuachia watu magazeti kwa ukawaida? (fu. 1) Tunawezaje kutayarisha mfululizo wa mazungumzo yenye kukazia andiko moja? (fu. 3) Kwa nini tunahitaji kufanya mengi zaidi ya kusoma tu andiko lililochaguliwa? (fu. 4) Namna gani mpango wa kuachia watu magazeti kwa ukawaida unaweza kutokeza funzo la Biblia? (fu. 5) Tia ndani onyesho la mhubiri akishiriki andiko moja na mtu anayemwachia magazeti kwa ukawaida.
Dak. 20: Vijana Walio Thabiti na Watiifu. Hotuba itakayotolewa na mzee, inayotegemea Mnara wa Mlinzi wa Septemba 15, 2002, ukurasa wa 23-24, chini ya kichwa kidogo “Jiepushe kwa Heshima.” Fanyeni mpango kimbele ili kijana mmoja au vijana wawili watoe maelezo kuhusu magumu wanayopambana nayo shuleni na jambo lililowasaidia wayashinde kwa matokeo.
Wimbo 222 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Novemba 7
Wimbo 39
Dak. 5: Matangazo ya kutaniko lenu.
Dak. 20: Boresha Hali ya Kuwa Mwangalifu Katika Mikutano. Hotuba na mazungumzo yanayotegemea Mnara wa Mlinzi wa Septemba 15, 2002, ukurasa wa 12-14, fungu la 11-14. Rudilia mapendekezo yanayotolewa, na ualike wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jambo ambalo limewasaidia kufaidika zaidi kutoka mikutano ya kutaniko.
Dak. 20: “Sitawisha Uwezo wa Kufikiri Pamoja na Wengine.”* Alika wahubiri uliowachagua watoe maelezo ya jinsi walivyoweza kufikiri pamoja na watu wa malezi mbalimbali katika eneo lenu.
Wimbo 50 na sala ya kumalizia.
* Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu.