Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Machi: Kitabu kipya Biblia Inafundisha Nini Hasa? kitakaziwa. Fanyeni jitihada ya pekee ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Aprili na Mei: Kazieni nakala mojawapo ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mnapofanya ziara za kurudia kwa watu waliopendezwa, kutia ndani wale wanaohudhuria Ukumbusho na/au matukio mengine ya kitheokrasi lakini ambao hawashirikiani kwa bidii na kutaniko, fanyeni jitihada ya kuwaachia kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Mradi unapaswa kuwa kuanzisha funzo la Biblia katika kitabu hicho. Juni: Toleeni watu kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Ikiwa watu wanasema kwamba hawana watoto, watoleeni kitabu Furaha ya Familia.
◼ Kwa kuwa Aprili ina miisho-juma kamili mitano, utakuwa mwezi bora kwa ajili ya kufanya upainia msaidizi.
◼ Ukumbusho utafanywa Siku ya Tatu, Aprili 12, 2006. Ikiwa kutaniko lenu lina mikutano Siku ya Tatu, mikutano hiyo inapaswa kufanywa siku nyingine ya juma ikiwa Jumba la Ufalme liko huru. Ikiwa hilo haliwezekani na ikiwa Mkutano wa Utumishi wenu unahusika, sehemu ambazo zinahusu kutaniko lenu zinaweza kuingizwa katika Mkutano mwingine wa Utumishi.
◼ Makutaniko yanapaswa kutolea wahubiri magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! mara tu yanapoyapokea. Hilo litaruhusu wahubiri kufahamiana na mambo yaliyo katika magazeti kabla ya kuyatolea watu katika utumishi wa shambani. Huduma Yetu ya Ufalme pia inapaswa kutolewa wahubiri mara tu inapofika. Inaweza kugawanywa kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko.
◼ Programu ya video Noé : Il marchait avec Dieu, itachunguzwa kwenye Mkutano wa Utumishi katika Mei. Ikiwa inahitajiwa, video hiyo inapaswa kufanyiwa ombi kupitia kutaniko mapema zaidi iwezekanavyo.
◼ Ofisi ya tawi haitowi vichapo vinavyoombwa na wahubiri binafsi. Mwangalizi-msimamizi anapaswa kuchukua mipango ili tangazo lifanywe kila mwezi kabla ya ombi la vichapo la kutaniko kutumwa kwenye ofisi ya tawi kusudi wote wanaotaka kupata vichapo vya kibinafsi waweze kumjulisha ndugu anayeshughulika na vichapo. Tafadhali kumbukeni ni vichapo gani vinavyofanyiwa ombi la pekee.
◼ Shule ya mapainia ijayo itafanywa kwa muda wa siku 10 kisha mkusanyiko wa wilaya, kuanzia Siku ya Tano ya juma la kisha mkusanyiko mpaka Siku ya Yenga ya juma lile jingine, katika jiji ambamo mkusanyiko wa wilaya unafanywa. Tutatumia kitabu kipya katika Kifaransa, Lingala, Swahili na Tshiluba. Wale wanaoalikwa watakuwa mapainia wa kawaida ambao bado hawajahudhuria shule na ambao waliwekwa rasmi kama mapainia wa kawaida tangu Agosti 1 2005, au kabla ya tarehe hiyo, na wengine ambao wamekuwa wakitumikia kama mapainia wa kawaida kwa miaka 15 au zaidi ijapokuwa tayari wamekwisha kufaidika na shule hiyo wakati uliopita. Kila painia atajulishwa kibinafsi.