Mambo ya Kukumbuka Kuhusu Ukumbusho
Mwaka huu Ukumbusho utaadhimishwa Siku ya Tatu, Aprili 12. Wazee wanapaswa kutolea mambo yafuatayo uangalifu.
◼ Katika kupanga wakati kwa ajili ya mkutano huu, hakikisheni kwamba mifano haitapitishwa mpaka jua litakapokuwa limetua.
◼ Kila mtu, kutia ndani msemaji, anapaswa kujulishwa kuhusu wakati sahihi na mahali pa mwadhimisho.
◼ Aina ya mkate unaofaa na divai inayofaa vinapaswa kupatikana na kuwa tayari.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Februari 15, 2003, ukurasa wa 14-15.
◼ Sahani, bilauri, na meza na nguo ya meza yenye kufaa vinapaswa kuletwa kwenye jumba na kupangwa mbele ya wakati.
◼ Jumba la Ufalme au mahali pengine patakapofanywa mkutano huo panapaswa kusafishwa kikamili mbele ya wakati.
◼ Ndugu wakaribishaji na wale watakaopitisha mifano wanapaswa kuchaguliwa na kupewa maagizo mbele ya wakati kuhusu kazi yao, utaratibu wenye kufaa wa kufuata, uhitaji wa kuvaa na kujipamba kwa heshima.
◼ Mipango inapaswa kuchukuliwa ili kuhudumia yeyote kati ya watiwa-mafuta aliye kilema na asiyeweza kuhudhuria.
◼ Ikiwa inapangwa kwamba zaidi ya kutaniko moja litumie Jumba la Ufalme lilelile, kunapaswa kuwe usimamizi mzuri kati ya makutaniko ili kuepuka msongamano usio wa lazima katika sebule au mwingilio, kwenye vijia vya watu wote vya kando ya barabara, na mahali pa kuegeshea magari.