Mambo ya Kutosahau kwa Ajili ya Ukumbusho
Mwadhimisho wa Ukumbusho mwaka huu utakuwa Siku ya Yenga, Aprili 4. Wazee wanapaswa kutoa uangalifu kwa mambo yafuatayo:
◼ Katika kupanga wakati kwa ajili ya mkutano huu, hakikisheni kwamba mifano haitapitishwa mpaka jua litakapokuwa limetua.
◼ Kila mtu, kutia ndani msemaji, anapaswa kujulishwa kuhusu wakati sahihi na mahali pa mwadhimisho.
◼ Aina yenye kufaa ya mkate na divai inapaswa kupatikana na kuwekwa tayari.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Februari 15, 2003, ukurasa wa 14-15.
◼ Sahani, bilauri, na meza na nguo ya meza yenye kufaa vinapaswa kuletwa kwenye jumba na kupangwa mbele ya wakati.
◼ Jumba la Ufalme au mahali pengine patakapofanywa mkutano panapaswa kusafishwa kikamili mbele ya wakati.
◼ Wakaribishaji na wahudumiaji wanapaswa kuchaguliwa na kupewa maagizo mbele ya wakati kuhusu madaraka yao, utaratibu wenye kufaa wa kufuata, na uhitaji wa kuvaa na kujipamba kwa heshima.
◼ Mipango inapaswa kuchukuliwa ili kuhudumia yeyote kati ya watiwa-mafuta aliye kilema au asiyeweza kuwako.
◼ Ikiwa zaidi ya kutaniko moja linapangwa ili kutumia Jumba la Ufalme lilelile, kunapaswa kuwe usimamizi mzuri kati ya makutaniko ili kuepuka msongamano usio wa lazima katika sebule au mwingilio, kwenye vijia vya watu wote vya kando ya barabara, na mahali pa kuegeshea magari.