Mambo ya Kukumbuka Kuhusu Ukumbusho
Mwaka huu Ukumbusho utaazimishwa Siku ya Kwanza, tarehe 2 mwezi wa 4. Wazee wanapaswa kutolea uangalifu mambo yanayofuata.
◼ Katika kupanga wakati kwa ajili ya mkutano huu, muwe waangalifu kwamba mifano isipitishwe mbele ya jua kutua.
◼ Kila mtu, kutia ndani msemaji, anapaswa kujulishwa kuhusu wakati kamili na mahali ambapo mutafanyia Ukumbusho.
◼ Aina ya mkate unaofaa na divai inayofaa vinapaswa kutafutwa na kutayarishwa mbele ya wakati.—Ona Mnara wa Mlinzi wa tarehe 15/02/2003, ukurasa wa 14-15.
◼ Sahani, bilauri, na meza na nguo ya meza vyenye kufaa vinapaswa kuletwa kwenye jumba na kupangwa mbele ya wakati.
◼ Jumba la Ufalme au mahali pengine ambapo mutafanyia mkutano, panapaswa kusafishwa kabisa mbele ya wakati.
◼ Ndugu wakaribishaji na wale watakaopitisha divai na mkate wanapaswa kuchaguliwa na kupewa maagizo mbele ya wakati kuhusu kazi yao, utaratibu wenye kufaa wa kufuata, na lazima ya kuvaa na kujipamba kwa heshima.
◼ Wazee wanapaswa kuchukua mipango ili kumpelekea mtiwa-mafuta yeyote mkate na divai, yeyote yule aliye kilema au asiye na uwezo wa kuhuzuria.
◼ Ikiwa inapangwa kwamba makutaniko mawili au zaidi yatumie Jumba la Ufalme lilelile, itaomba makutaniko yatengeneze programu vizuri ili kuepuka msongamano usio wa lazima katika ukumbi au kwenye mwingilio wa vijia vya watu wote vilivyo karibu na barabara na kwenye mahali pa kuegeshea magari.