Programu ya Mikutano ya Utumishi
Juma Tokea Tarehe 8/01
Wimbo 12
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Tia moyo kila mtu aangalie video Pas de sang : la médecine relève le défi ili kujitayarisha kwa ajili ya mazungumzo yatakayofanywa kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma tokea tarehe 22 mwezi wa 1. Mkitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au utoaji mwingine mbalimbali wenye kufaa eneo lenu, onyesheni jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa tarehe 15/1 na Amkeni! ya mwezi wa 1. Katika utoaji moja, onyesheni jinsi ya kushugulikia kizuia-mazungumzo “Nina shughuli (kazi nyingi).”—Ona kitabu Kutoa Sababu, uku. 19-20.
Dak. 15: Faidika na kitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yenye kutegemea maneno ya utangulizi ya kitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2007. Zungumzieni jambo la kwamba ni lazima kila mtu achukue dakika chache kila siku ili kuchunguza Andiko na maelezo ya kitabu hicho. Tayarisha mbele ya wakati mtu mmoja au wawili ili waeleze jinsi wanavyochunguza andiko kwa kawaida na jinsi wanavyofaidika kwa kufanya hivyo. Malizia kwa kuzungumzia kwa kifupi andiko la mwaka 2007.
Dak. 20: Fikishia Kila Mtu Habari Njema. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji, yenye kutegemea kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, ukurasa wa 92 mpaka kichwa kidogo kwenye ukurasa wa 102.
Wimbo 165 na sala ya kumalizia.
Juma Tokea Tarehe 15/01
Wimbo 93
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Matangazo yaliyochaguliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 15: Je, Kuna Jambo Linalokuzuia? Hotuba itakayotolewa na mzee, yenye kutegemea Mnara wa Mlinzi wa 1/04/02, ukurasa wa 13-15.
Dak. 20: “Mimi Sipendezwi.”* Mnapozungumzia fungu la 4, uliza wasikilizaji ni mambo gani yenye kuhangaisha watu katika eneo lenu. Fanyeni maonyesho mawili mafupi yenye kuonyesha jinsi ya kushugulikia kizuia-mazungumzo “Mimi sipendezwi.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, uku. 16.
Wimbo 135 na sala ya kumalizia.
Juma Tokea Tarehe 22/01
Wimbo 224
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Soma ripoti ya feza za kutaniko na shukrani kuhusu michango. Mkitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au utoaji mwingine mbalimbali wenye kufaa eneo lenu, onyesheni jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1/02 na Amkeni! ya mwezi wa 2. Katika utoaji mmoja, onyesheni jinsi ya kurudilia watu tunaowaachia magazeti kwa ukawaida.
Dak. 10: Mahitaji ya kutaniko lenu.
Dak. 25: “Ni Aina Gani ya Matunzo ya Kiganga Iliyo Bora Zaidi?” Itolewe na mzee. Anzeni mara moja kuzungumzia video Pas de sang pamoja na wasikilizaji, mkitumia maulizo yaliyo katika habari hiyo. Malizia kwa kusoma fungu la mwisho na kutia moyo wasikilizaji wote wasome kwa uangalifu habari za Mnara wa Mlinzi zinazotajwa. Ikiwa hamuna video hiyo katika kutaniko lenu, mnaweza kutumia Amkeni! ya mwezi wa 8, 2000, ukurasa wa 7-11 na broshua Damu Yaweza Kuokoaje Uhai Wako, ukurasa 8-15, 18.
Wimbo 188 na sala ya kumalizia.
Juma Tokea Tarehe 29/01
Wimbo 55
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za mahubiri za mwezi wa 1. Taja kitabu cha kutolea watu katika mwezi wa 2, na fanyeni onyesho moja.
Dak. 20: “Je, Unajitayarisha kwa Ajili ya Misiba?”* Itolewe na mzee. Tia ndani maelezo ya Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 11, 2005, ukurasa wa 3.
Dak. 15: Ikiwa Uliahidi Kurudilia Mtu Katika Mahubiri, Umrudilie. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji, yenye kutegemea Mnara wa Mlinzi wa 15/09/99, ukurasa wa 11. Omba wasikilizaji waeleze mambo waliyoona yenye kuonyesha jinsi walivyobarikiwa kwa kurudilia watu kama walivyoahidi.
Wimbo 137 na sala ya kumalizia.
Juma Tokea Tarehe 5/02
Wimbo 3
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu.
Dak. 15: Jitambulishe! Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Vijana wengine wanasita kujitambulisha kwamba wao ni Mashahidi wa Yehova, kwa kuwa wanaona kwamba wenzao wanaweza kuwacheka. Lakini, kuna sababu nzuri ya kujitambulisha. Walimu wanaojua mambo mnayoamini wataweza kuyaheshimu nao hawatawalazimisha kufanya mambo yasiyofaa. Vijana wasiofuata kanuni za mwenendo safi watasita kuwaalika ninyi kujiunga nao katika kufanya mambo mabaya. Wengine wataelewa bila magumu maamuzi yenu kuhusu mambo kama vile urafiki wa kimapenzi au michezo kwenye masomo, na pia mambo mengine yanayofanyika kisha saa za masomo. Pia hamutasikia woga wa kuhubiri kwenye masomo au woga wa kukutana na wanafunzi wengine munapohubiri katika eneo lenu. (g02 3/22 uku. 12) Omba wasikilizaji waeleze jinsi walivyopata faida kwa kujitambulisha kwenye masomo yao kwamba wao ni Mashahidi wa Yehova. Mnaweza kutayarisha mbele ya wakati mtu mmoja au watu wawili ili kutoa maelezo.
Dak. 20: “Upendo—Siri ya Kupata Matokeo Mazuri Katika Mahubiri.”* Tia ndani maelezo ya Mnara wa Mlinzi wa 1/02/03, ukurasa wa 23, fungu la 16-17.
Wimbo 83 na sala ya kumalizia.
* Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu.