Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/08 uku. 2
  • Programu ya Mikutano ya Utumishi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu ya Mikutano ya Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Vichwa Vidogo
  • Juma Tokea Tarehe 14/01
  • Juma Tokea Tarehe 21/01
  • Juma Tokea Tarehe 28/01
  • Juma Tokea Tarehe 4/02
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 1/08 uku. 2

Programu ya Mikutano ya Utumishi

Juma Tokea Tarehe 14/01

Wimbo 41

Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Matangazo yaliyochaguliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Kwa kutumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 ao utoaji mwingine wowote wenye kufaa eneo lenu, fanyeni onyesho la jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1/01 na Amkeni! ya mwezi wa 1.

Dak. 15: “Tumia Vizuri Zaidi Wakati Wako Katika Kazi ya Kuhubiri.”* Uliza ndugu mmoja anayeonyesha mfano mzuri kupitia namna yake ya kuongoza mikutano kwa ajili ya mahubiri. Anafanya nini ili kujitayarisha kuongoza mikutano hiyo na kutayarisha watu watumie vizuri zaidi wakati wanaopitisha katika kazi ya kuhubiri?

Dak. 20: “Maneno Yenu na Yawe . . . Yenye Kukolezwa Chumvi.”* Munapozungumzia fungu la 2, someni Yohana 4:7-15, 39.

Wimbo 85

Juma Tokea Tarehe 21/01

Wimbo 215

Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Julisha kitabu cha kutolea watu katika mwezi wa 2 na mufanye onyesho moja. Tia moyo kila mmoja aangalie video Soigner sans transfuser — Besoins et droits du patient ili kujitayarisha kwa ajili ya mazungumzo yatakayofanywa katika Mkutano wa Utumishi wa juma tokea tarehe 4 mwezi wa 2.

Dak. 10: Je, Unatumia Kitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yenye kutegemea maneno ya utangulizi ya kitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2008. Zungumzia umaana wa kuchukua kila siku wakati wa kuchunguza Andiko la siku na maelezo yake. Omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jinsi wanavyochunguza andiko kwa ukawaida na jinsi wanavyofaidika kwa kufanya hivyo. Mtu mmoja ao wawili wanaweza kutayarishwa mbele ya wakati ili kutoa maelezo. Zungumzia kwa kifupi andiko la mwaka 2008.

Dak. 25: “Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema.”* (fu. 1-10) Itolewe na mwangalizi wa utumishi. Uliza mhubiri mmoja ao wawili ambao walifanya kazi ya upainia msaidizi muda fulani katika mwaka uliopita ijapokuwa walikuwa na mambo mengi ya kufanya ao uzaifu wa kimwili. Namna gani waliweza kufanya hivyo? Walipata furaha gani? Munapozungumzia fungu la 7, julisha programu ya mikutano kwa ajili ya mahubiri katika mwezi wa 3, wa 4 na wa 5.

Wimbo 177

Juma Tokea Tarehe 28/01

Wimbo 52

Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za mahubiri za mwezi wa 1. Soma ripoti ya feza na shukrani kuhusu michango. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yenye kutegemea Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1/02/08 na Amkeni! ya mwezi wa 2. Baada ya kutoa maelezo mafupi kuhusu kila toleo, uliza wasikilizaji habari ambazo zinaweza kuvutia watu katika eneo na kwa nini. Omba wasikilizaji watokeze mawazo fulani yaliyo katika habari wanazopanga kukazia. Ni ulizo gani linaloweza kutokezwa ili kuanzisha mazungumzo? Ni andiko gani katika habari linaloweza kusomwa? Namna gani andiko hilo linaweza kuambatanishwa na habari? Kwa kutumia utoaji mbalimbali wenye kupendekezwa kwenye ukurasa wa 8, fanyeni onyesho kuhusu jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa.

Dak. 20: “Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema.”* (Fu. 11-17) Ikiwa vikaratasi vya mwaliko wa pekee kwenye Ukumbusho vinapatikana, mutolee kila mtu kati ya wasikilizaji kikaratasi kimoja munapozungumzia fungu la 14. Julisha mipango ya kutaniko lenu ili kutolea kila mtu kikaratasi cha mwaliko katika eneo lenu.

Dak. 15: “Saidia Wanafunzi wa Biblia Wawe Wahubiri wa Habari Njema ya Ufalme.”* Ikiwa wakati unaruhusu, omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu Maandiko yanayotajwa.

Wimbo 22

Juma Tokea Tarehe 4/02

Wimbo 161

Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Chunguzeni Kisanduku cha Maulizo.

Dak. 10: Mahitaji ya kutaniko lenu.

Dak. 25: “Je, Umekawia?” Itolewe na mzee. Kwa kutumia maulizo yanayotolewa katika habari, anza mara moja mazungumzo pamoja na wasikilizaji kuhusu video Besoins et droits du patient. Kwa kumalizia, soma fungu la mwisho na kutia moyo wote wachunguze kwa uangalifu habari zinazotajwa katika Mnara wa Mlinzi na Huduma Yetu ya Ufalme. Fasiria jinsi ambavyo kila mtu ambaye hajajaza bado kadi hiyo anaweza kutumia karatasi zenye kusaidia za maulizo na majibu zilizo katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 11, 2006, ili kufanya maamuzi yake mwenyewe kuhusu sehemu za damu na namna mbalimbali za matunzo, na kisha kuandika maamuzi hayo kwenye kadi ya kiganga DPA. Wale ambao wamekwisha kujaza kadi zao za kiganga DPA wanaweza kuchunguza tena maamuzi yao ya mbele, na kujaza kadi mpya ikiwa ni lazima.

Wimbo 4

* Maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine