Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/08 uku. 2
  • Programu ya Mikutano ya Utumishi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu ya Mikutano ya Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Vichwa Vidogo
  • Juma Tokea Tarehe 11/02
  • Juma Tokea Tarehe 18/02
  • Juma Tokea Tarehe 25/02
  • Juma Tokea Tarehe 3/03
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 2/08 uku. 2

Programu ya Mikutano ya Utumishi

Juma Tokea Tarehe 11/02

Wimbo 168

Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Kwa kutumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 ao utoaji mwingine wowote wenye kufaa eneo lenu, fanyeni onyesho la jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1/02 na Amkeni! ya mwezi wa 2.

Dak. 15: Je, Unaweza Kutumikia Mahali Penye Uhitaji Mkubwa? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yenye kuchukuliwa katika Mnara wa Mlinzi wa tarehe 15/07/03, ukurasa wa 20. Tia ndani maelezo ya kitabu Tengenezo, ukurasa wa 111, fungu 1, mpaka ukurasa 112, fungu 1. Uliza kwa kifupi mtu yeyote ambaye amehamia mahali ambako kuna uhitaji mkubwa. Ni matatizo gani walipata, na namna gani walishindana nayo? Ni baraka gani walizopata?

Dak. 20: Muwasaidie Wahubiri Wapya Kufanya Maendeleo. Kisha maneno ya utangulizi yasiyofikia dakika moja, ongoza mazungumzo ya maulizo na majibu yenye kutegemea Mnara wa Mlinzi wa tarehe 01/12/05, ukurasa wa 31, ukitumia maulizo ya funzo yanayotolewa. Mukiisha kuzungumzia fungu la 18, fanyeni onyesho. Katika onyesho hilo, msikilizaji anapinga maneno ya mhubiri mpya anayetumika pamoja na mhubiri mwenye uzoefu mwingi. Msikilizaji hatosheke na jibu la mhubiri mpya, na anakatiza mazungumzo. Wanapoondoka, mhubiri mwenye uzoefu anamshukuru kwa shauku mhubiri mpya kwa kuwa alijikaza, na kisha anamwonyesha jinsi ya kutumia kitabu Kutoa Sababu ili kushinda kizuia-mazungumzo hicho wakati ujao.

Wimbo 50

Juma Tokea Tarehe 18/02

Wimbo 17

Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Matangazo yaliyochaguliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme.

Dak. 10: Mahitaji ya kutaniko lenu.

Dak. 25: “Wanaonyesha Imani Yenye Nguvu!”* Itolewe na mwangalizi wa utumishi. Malizia kwa kurudilia mambo yenye kutia moyo ambayo kutaniko limetimiza mwaka wa utumishi uliopita.

Wimbo 194

Juma Tokea Tarehe 25/02

Wimbo 81

Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za mahubiri za mwezi wa 2. Soma ripoti ya feza na shukrani kuhusu michango. Mufanye onyesho la jinsi ya kutumia kikaratasi cha mwaliko ili kualika mshiriki wa familia ao jirani kwenye Ukumbusho.

Dak. 20: “Kukumbuka kwa Shukrani Fidia.”* Ikiwa wakati unaruhusu, omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yaliyotajwa.

Dak. 15: Jitayarishe Kutolea watu Magazeti ya Sasa. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Baada ya kutoa maelezo mafupi kuhusu Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1/03 na Amkeni! ya mwezi wa 3, uliza wasikilizaji habari ambazo zinaweza kuvutia watu katika eneo na kwa nini. Omba wasikilizaji watokeze mawazo fulani yaliyo katika habari wanazopanga kukazia. Ni ulizo gani linaloweza kutokezwa ili kuanzisha mazungumzo? Ni andiko gani katika habari linaloweza kusomwa? Kwa kutumia mapendekezo, Mufanye onyesho la jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1/03 na Amkeni! ya mwezi wa 3.

Wimbo 119

Juma Tokea Tarehe 3/03

Wimbo 223

Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Chunguzeni mambo makuu katika kisanduku “Mambo ya Kukumbuka Kuhusu Ukumbusho.”

Dak. 20: Je, Unaweza Kuanzisha Funzo la Biblia Katika Mwezi wa 3? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Katika mwezi wa 3, tutatolea watu kitabu Biblia Inafundisha, tukiwa na mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia. Muzungumzie mambo fulani yenye kutokeza ya kitabu hicho. Mwonyeshe jinsi tunaweza kutoa kitabu hicho tunapotembelea mtu aliyependezwa wakati tulimtolea kikaratasi cha mwaliko kwenye Ukumbusho, tunaporudilia mtu tuliyemwachia magazeti, na tunapotolea watu magazeti nyumba kwa nyumba kisha tarehe 22 mwezi wa 3. (Ona km 8/07 uku. 3; km 3/06 uku. 1, fu. 3; km 1/06 uku. 3-6.) Mufanye onyesho moja ao maonyesho mawili ya utoaji huo mbalimbali.

Dak. 15: Tumia Biblia Unapojibu Maulizo. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yenye kuchukuliwa katika kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 143-144. Tia ndani onyesho fupi la mhubiri anayeulizwa ulizo lenye kutokezwa mara nyingi katika eneo lenu na kisha anatumia Biblia ili kujibu.

Wimbo 145

* Maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine