Matangazo
◼ Toleo la vitabu la mwezi wa 3: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Mujikaze sana kuanzisha mafunzo ya Biblia. Mwezi wa 4 na wa 5: Magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Tunaporudilia watu wenye kupendezwa, kutia ndani wale waliohuzuria Ukumbusho ao matukio mengine ya kitheokrasi lakini hawajiunge sana na kutaniko, tutajikaza sana kuwatolea kitabu kipya Biblia Inafundisha Nini Hasa? Kusudi letu linapaswa kuwa kuanzisha mafunzo ya Biblia katika kitabu hicho. Mwezi wa 6: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa msikilizaji amekwisha kupata kitabu hicho, mhubiri anaweza kumtolea kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa mbele ya mwaka wa 1992.
◼ Makutaniko yanapaswa kutolea watu magazeti mapya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! mara tu yanapoyapata. Hilo litasaidia wahubiri kujua mambo yaliyo katika magazeti hayo mbele ya kuyatolea watu katika mahubiri.