‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
1. Funzo la Biblia la kutaniko litatutolea nafasi gani katika miezi inayokuja?
1 Injili ine zinazungumzia mambo mengi kuhusu Yesu Mwana wa Mungu. Kwa kuwa Wakristo wanapaswa ‘kufuata hatua zake kwa ukaribu,’ tutahitaji kujitayarisha vizuri na kufuata kwa uangalifu tutakapojifunza kitabu ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’ katika luga fulani kwenye funzo la Biblia la kutaniko kuanzia juma tokea tarehe 1 mwezi wa 3. (1 Pet. 2:21; Marko 10:21) Ni jambo la maana kuchunguza kwa njia ya pekee sehemu mbalimbali za maisha ya Yesu ambazo zinaweza kututia moyo katika mahubiri.
2. Namna gani mfano wa Yesu wa uvumilivu unaweza kutusaidia?
2 Mfano Ambao Yesu Alituachia: Je, mutu fulani amekwisha kupinga ujumbe wako ulipokuwa ukihubiri nyumba kwa nyumba? Tunapopingwa hivyo, tunaelewa maana ya maneno haya ya Yesu: “Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa ninyi pia.” (Yoh. 15:20) Kwa kweli, hatuwezi kusema kwamba kila upinzani unatimiza maneno hayo ya Yesu. Hata ikiwa Yesu alipatwa na mateso, ni furaha iliyokuwa mbele yake ndiyo ilimfanya avumilie majaribu yote aliyokutana nayo. Sisi pia tunaweza kujikaza tukubaliwe na Yehova na kupata zawadi kwa sababu ya uaminifu wetu. Hilo litatusaidia ‘tusichoke na kuzimia katika nafsi zetu.’ (Ebr. 12:2, 3; Met. 27:11) Tunapoendelea kuhubiri bila kuacha, sisi pia tunaweza kuwa hakika kwamba Yesu Kristo atatutegemeza.—Mt. 28:20.
3. Namna gani tunaweza kuiga maoni ya Yesu kuhusu kazi ya kuhubiri?
3 “Nilitumwa Kufanya Hivyo”: Kazi ya kuhubiri Ufalme ilichukua nafasi ya kwanza katika maisha ya Yesu. (Luka 4:43) Alijitoa kabisa katika kazi ya kuhubiri. Alijua kwamba kazi hiyo ilipaswa kufanywa kwa uharaka na kila mara alitafuta nafasi ili kuzungumzia wengine kuhusu Ufalme. Kwa kuwa sisi ni wafuasi wa Yesu, mfano wake utatuchochea tufanye nini? Tunapofanya kazi zetu za kila siku, je, tunakutana na watu ambao tunaweza kuhubiria habari njema? Basi, acheni upendo wa Yesu utuchochee kuhubiria watu wengi zaidi kadiri iwezekanavyo!—2 Kor. 5:14.
4. Namna gani tunaweza kufanya namna yetu ya kuhubiri iwe nzuri zaidi?
4 ‘Mutu Mwingine Hajapata Kamwe Kusema Kama Huyu’: Watu waliomsikiliza Yesu walishangazwa na njia yake ya kufundisha. (Yoh. 7:46; Mt. 7:28, 29) Ni jambo gani lililomfanya awe tofauti na walimu wengine? Alipenda kweli alizofundisha, alipenda watu aliofundisha, na alitumia njia mbalimbali za kufundisha. Tunapomwiga Mwalimu Mkuu, tunaweza kufanya namna yetu ya kuhubiri iwe nzuri zaidi.—Luka 6:40.
5. Tunapaswa kuwa na kusudi gani tunapojifunza kitabu ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’?
5 Hayo ni mambo machache ya pekee ambayo tunaweza kujifunza kuhusu Yesu. Ni mambo mengine gani tunayoweza kujifunza kumhusu? Tunapojifunza kuhusu maisha ya Yesu wakati wa Funzo la Biblia la Kutaniko, tuwe na kusudi la “kuujua upendo wa Kristo” kwa kuiga maneno na matendo yake.—Efe. 3:19.