Matangazo
◼ Toleo la vitabu la Mwezi wa 2: Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Mwezi wa 3: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Wahubiri watafikiria kuanzisha mafunzo ya Biblia wanapomtolea mutu kitabu hicho ao ikiwa msikilizaji amekwisha kukipata. Mwezi wa 4 na wa 5: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mnaporudilia watu wenye kupendezwa, kutia ndani wale waliohuzuria Ukumbusho ao matukio mengine ya kitheokrasi lakini hawajiunge sana na kutaniko, mujikaze kuwatolea kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Munapaswa kuwa na kusudi la kuanzisha mafunzo ya Biblia.