Matangazo
◼ Toleo la vitabu la mwezi wa 5: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Munaporudilia watu wenye kupendezwa, kutia ndani wale waliohuzuria Ukumbusho ao matukio mengine ya kitheokrasi lakini hawajiunge sana na kutaniko, mujikaze kuwatolea kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? mukiwa na kusudi la kuanzisha funzo la Biblia. Mwezi wa 6: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Mahali ambapo msikilizaji amekwisha kupata kitabu hicho, mhubiri anaweza kumtolea kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa mbele ya mwaka wa 1995.
◼ Kwenye mkutano wa utumishi wa juma tokea tarehe 10 mwezi wa 5, mzee mmoja atasoma tena barua ya tarehe 7 mwezi wa 12, 2009 inayohusu kuchunguza tena ‘azimio kwa ajili ya Jumba la Ufalme.’ Kwenye mkutano wa utumishi wa juma tokea tarehe 17 mwezi wa 5, mratibu wa baraza la wazee atapendekeza azimio jipya kwa kutaniko. Kisha hapo, atatuma kopi ya azimio mpya kwenye biro ya tawi.
◼ Siku ya Posho tarehe 29 mwezi 5, 2010 familia ya Betheli itakuwa na utendaji wa pekee na Siku ya Posho tarehe 12 mwezi wa 6, 2010, kutakuwa usafishaji wa Betheli. Kwa hiyo, tunawaomba tafazali, musipange kutembelea kwenye Betheli ao kutembelea Wanabetheli siku hizo mbili.
◼ Tunafanya mipango ili kutumia kila kutaniko programu inayoonyesha mahali mbalimbali ambapo mikusanyiko ya wilaya itafanywa; tutatumia kila kutaniko bahasha moja iliyo na fomu za 2011. Mwandishi wa kutaniko atahakikisha kwamba kutaniko limepata bahasha hiyo.
◼ Tunajulisha makutaniko kwamba vichapo vinavyofuata vinapatikana katika luga ya Lhukonzo: Biblia Inafundisha Nini Hasa?, Mungu Anataka Tufanye Nini?, Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu, Siri ya Kupata Furaha ya Familia, na trakti T-15, T-16, T-21, T-23, T-26, T-27. Kwa kuwa, kwa kawaida watu wanaozungumza Kinande wanaelewa Lhukonzo, tunatia moyo makutaniko yanayotaka yafanye ombi la vichapo hivyo, zaidi sana kitabu Biblia Inafundisha.